Logo
Chapisha ukurasa huu

Afisi ya Habari
Wilayah Misri

H.  27 Muharram 1447 Na: 1447/05
M.  Jumanne, 22 Julai 2025

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Hasira ya Watu wa Gaza kutoka Ng'ambo za Bahari Inataka Mzingiro Uvunjwe... Watu wa Misri na Jeshi lake Watakasirika Lini? Lini Hasira yao Itakuwa Moto wenye Kuteketeza Umbile la Kiyahudi na Tawala za Mamluki Zinazolilinda?
(Imetafsiriwa)

Wakati Gaza ikiwa inakufa kwa njaa, ikizingirwa kwa kimya cha aibu cha Waarabu na njama ya wazi ya kimataifa, kijana mmoja wa Kimisri kutoka ng'ambo, Anas Habib, alifunga milango ya ubalozi wa Misri nchini Uholanzi na kumwaga unga kwenye kizingiti chake. Alipiga kelele kwa jina la watu waliozingirwa wa Gaza na kuliita jeshi lake nchini Misri kuvunja mzingiro, kufungua kivuko, na kumaliza njaa ya kupangwa... Kilio kutoka nchi ya mbali kilisikika ndani ya nyoyo huru. Je, kuna yeyote kati ya watu wa Misri atakayejibu? Je, kuna ulinzi wowote katika nyoyo za watu wa jeshi la Kinana? Au kufuli zilizowekwa kwenye ubalozi wa Misri jijini The Hague ni za kikatili kidogo kuliko kufuli zilizowekwa kwenye utashi na silaha zao?!

Enyi Watu wa Kinana! Enyi jeshi lake hodari, Gaza inakulilieni, je, kuna yeyote anayeweza kusaidia?

Kinachotokea Gaza ni jinai kamili, ambayo kwayo kila mtu aliyekaa kimya, kuafiki, na kujisalimisha anashiriki. Kivuko cha Rafah, njia pekee ya uhai kwa wakaazi waliosalia, kimefungwa kwa amri ya sera inayotii Mayahudi. Chakula, dawa, na maji haviruhusiwi kuingia kwa njia hiyo, na usaidizi wa kweli unanyimwa, yote hayo ni huku kukiwa na utiifu serikali na kutochukua hatua kwa majeshi!

Wakati ambapo watu wa Gaza walikuwa wakingojea watu wao wa karibu zaidi—watu wa Misri, ambao wanashirikiana katika Uarabu, Uislamu, na damu yao—wachukue hatua ya kuondoa mzingiro na kukomesha dhulma, hatua hiyo ilitoka Uholanzi! Ndiyo, kutoka kwa kijana, mgeni katika ardhi ya kigeni ... Hisia zake zilichochewa na ulinzi wake uliamshwa. Alifunga ubalozi wa Misri na kupiga kelele: "Fungueni kivuko cha Rafah!" "Okoeni Gaza!" "Ondoeni mzingiro!" Je, bado mungali na uungwana wowote enyi watu wa Misri?

Wajibu wa kidini unaovuka wajibu mwengine wote ni kuwanusuru wanaodhulumiwa na kuikomboa ardhi hiyo iliyo nyakuliwa. Huu ni wajibu ulilowekwa juu ya majeshi ya Waislamu, sio tu juu ya watu, kwa sababu wanamiliki silaha na uwezo, na wao ndio wanaobeba faradhi kubwa ya jihad katika njia ya Mwenyezi Mungu. Al-Nawawiy asema: “Kama makafiri (makafiri) wakiingia katika mji wa Kiislamu au kuizingira nchi, jihadi inakuwa ni faradhi ya mtu binafsi kwa walio karibu nao zaidi, kisha walio karibu zaidi. Al-Qurtubi amesema: "Ikiwa jihad ni faradhi, basi hakunna anayeweza kubaki nyuma isipokuwa kwa udhuru ulio wazi. Mwenye kubaki amefanya dhambi kubwa." Ibn Qudamah amesema: "Iwapo adui atashambulia uwanja wa mji au imam akawaita watu wakusanyike, ni faradhi kwa kila mtu kutoka nje, na hakuna atakayebaki nyuma."

Enyi askari wa Misri, je, adui hajatua Gaza, akaizunguka, kuishambulia kwa mabomu, na kuipa mateso ya kutisha? Je, Al-Aqsa, sio sehemu ya Safari ya Usiku ya Mtume wenu (saw), je haiko chini ya uvamizi? Je! watu wa Gaza sio ndugu zenu? Je, muna udhuru gani wakati munamiliki majeshi yenye nguvu zaidi katika kanda hii na kivuko cha Rafah kiko mikononi mwenu?

Ewe jeshi nyoofu la Kinana: Nyinyi ni watoto wa watu hawa wa kweli, watoto wa wakombozi. Mumepewa nguvu ya kuikomboa Al-Quds ndani ya siku chache, ikiwa mutatenda kwa mujibu wa Aqidah (itikadi) ya Uislamu, sio kwa utiifu wa Magharibi na vibaraka wake, kwa mujibu wa sheria ya Mwenyezi Mungu, sio sheria za Magharibi, na chini ya bendera ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), sio bendera ya Sykes-Picot.

Enyi askari wa Kinanah: Nyinyi sio zana katika mikono ya utawala kibaraka unaotekeleza makubaliano ya aibu na yanayoifurahisha Marekani na umbile la Kiyahudi kwa gharama ya Ummah wenu. Bali nyinyi ni wenye kuhisabiwa mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na mtaulizwa Siku ya Kiyama: Kwa nini hamkuchukua hatua? Kwa nini mulikubali mipaka na makubaliano? Kwa nini hamkuwanusuru watu wenu mjini Gaza?! Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema: «مَا مِنْ امْرِئٍ يَخْذُلُ امْرَأً مُسْلِماً عِنْدَ مَوْطِنٍ تُنْتَهَكُ فِيهِ حُرْمَتُهُ وَيُنْتَقَصُ فِيهِ مِنْ عِرْضِهِ إِلَّا خَذَلَهُ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ فِي مَوْطِنٍ يُحِبُّ فِيهِ نُصْرَتَهُ» “Hakuna Muislamu ambaye atamtelekeza Muislamu mwengine katika sehemu ambayo utukufu wake unakiukwa na heshima yake inavunjwa isipokuwa Mwenyezi Mungu (swt) naye atamtelekeza katika sehemu ambayo angependa nusra yake;” Leo, heshima ya Gaza inavunjwa, utukufu wake unakiukwa, na wanawake na watoto wake wanauawa mbele ya macho yenu. Je, mutakubali kwamba Mwenyezi Mungu akuacheni mahali mungependa nusra?

Enyi watu wa Misri: Pazeni sauti zenu juu, kama alivyofanya Anas Habib, wala msiogope kulaumiwa na yeyote kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, hata kama mtazifungia taasisi zote za serikali hii kibaraka mpaka itakapong'olewa. Kumbatieni kila juhudi za dhati za maafisa na wanajeshi wanaotaka kufungua barabara ya Gaza na kuikomboa Palestina. Jueni kwamba mzozo wa leo ni baina ya Uislamu na ukafiri, baina ya haki na batili, na kwamba asiyekuwa pamoja na watu wa Gaza yuko upande wa maadui zao, watambue hilo au wasitambue.

Enyi Askari wa Kinana: Jueni kwamba nyinyi mnawajibika mbele ya Mwenyezi Mungu kwa umwagaji damu huu, njaa hii, na mzingiro huu. Hakuna medali, mishahara, au dhamana ya kirongo vitakavyokufaidi chini ya utawala wa msaliti.

Mwenyezi Mungu atakuulizeni: Kwa nini hamkuchukua hatua? Gaza itatoa hoja dhidi yenu Siku ya Kiyama ikiwa hamtainusuru. Historia haitakuwa na huruma kwa wale waliopuuza Safari ya Usiku ya Mtume (saw).

Wakati kijana wa Kimisri kutoka Uholanzi alipofunga ubalozi wa serikali yake kwa kufuli za hasira, alifungua lango ndani ya nyoyo za Ummah mzima, akiukumbusha kwamba jihad haiwezi kufungwa, kwamba ushindi hauwezi kuahirishwa, na kwamba Gaza sio kadhia ya kibinadamu, bali ni kadhia ya Umma, imani, na utu.

Enyi watu wa Misri, nyinyi ndio safu ya kwanza ya ulinzi wa Ummah, na mko kwenye moja ya mipaka ya Uislamu. Jihadharini usije Uislamu ukashambuliwa kutoka upande wenu. Sauti ya hasira kutoka ng'ambo ya bahari imetoa wito huo. Je, kuna yeyote katika jeshi la Misri ambaye atajibu?!

Hasira kutoka ng'ambo ya bahari haitatosheleza...Bali, ardhi yote ya Misri lazima iwe na hasira... Cairo lazima iwe inawaka moto kwa wito wa Khilafah... sio kufungua kivuko, bali kugeuza ukurasa mpya wa ushindi katika historia.

Ewe Mwenyezi Mungu, ilinde Gaza na watu wake, wanusuru wale wanaowanusuru, vunja kila mzingiro, na uupe Ummah mtu ambaye kwa mara nyengine tena atainua bendera ya ukombozi na ushindi. Ewe Mwenyezi Mungu, Simamisha Khilafah Rashida, fungua panga za jihad kupitia kwayo, ukomboe Msikiti wa Al-Aqsa kupitia kwayo, na uwanusuru wanaodhulumiwa mjini Gaza na nchi nyenginezo za Waislamu.

[وَمَا لَكُمْ لَا تُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللهِ وَالْمُسْتَضْعَفِينَ مِنَ الرِّجَالِ وَالنِّسَاءِ وَالْوِلْدَانِ الَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا أَخْرِجْنَا مِنْ هَٰذِهِ الْقَرْيَةِ الظَّالِمِ أَهْلُهَا وَاجْعَل لَّنَا مِن لَّدُنكَ وَلِيّاً وَاجْعَل لَّنَا مِن لَّدُنكَ نَصِيراً]

“Na mna nini msipigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu na ya wale wanao onewa, wanaume na wanawake na watoto, ambao husema: Mola Mlezi wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhaalimu, na tujaalie tuwe na mlinzi anaye toka kwako, na tujaalie tuwe na wa kutunusuru anaye toka kwako.” [An-Nisa 4:75]

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Misri

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Misri
Address & Website
Tel: 
http://hizb.net/
E-Mail:  info@hizb.net

Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.