Alhamisi, 06 Safar 1447 | 2025/07/31
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kuzingirwa kwa Gaza ni Ushahidi wa Khiyana ya Serikali ya Misri

Gaza imeingia katika awamu ya tano njaa (awamu ya janga la njaa), kulingana na ripoti ya Umoja wa Mataifa. Huku Waislamu kila mahali wakijaribu kuwanusuru ndugu zao kwa michango na kuanzisha misafara ya kuvunja mzingiro dhidi yao, nchi jirani zinatazama bila harakati yoyote—mbele yao zaidi ni Misri, ambayo ina mpaka na Gaza, lakini inadai kuwa haina usemi katika suala hilo na imeridhia kuchukua dori ya mpatanishi. Hivyo, je, kweli Misri haina uwezo wa kuwanusuru watu wa Gaza?!

Soma zaidi...

Enyi Wanazuoni wa Al-Azhar: Ikiwa hamtasema neno la haki leo... lini basi?!

Katika wakati ambapo sura za mauaji yanayofanywa na Mayahudi mjini Gaza zikiongezeka, na chakula, dawa, na maji vikizuiliwa kwa watoto, wanawake na wanaume, Al-Azhar ilitoa tamko la kulaani "jinai ya kuweka njaa" inayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi. Taarifa hiyo ilifutwa baadaye! Basi je, inajuzu kilio dhidi ya dhalimu kifutwe?! Na je, sauti ya wanazuoni inaweza kukaa kimya dhidi ya mauaji?! Taarifa hiyo ilikuja ikiwa imejaa misamiati ya kibinadamu, yenye kuwavutia watu wenye dhamiri hai, jumuiya ya kimataifa, na dola zenye ushawishi, na kutoa wito wa kufunguliwa kwa vivuko na utoaji wa misaada. Umbile la Kiyahudi lilielezewa kuwa linafanya uhalifu wa njaa, likituhumiwa kwa mauaji ya halaiki na kuzuia misaada, na ilitoa wito kwa mashirika ya kibinadamu, Umoja wa Mataifa na mashirika ya kimataifa kusonga mbele kufungua vivuko, pamoja na kuwaombea dua watu wa Gaza kwamba Mwenyezi Mungu awanusuru na alipize kisasi kwa ajili yao.

Soma zaidi...

Hasira ya Watu wa Gaza kutoka Ng'ambo za Bahari Inataka Mzingiro Uvunjwe... Watu wa Misri na Jeshi lake Watakasirika Lini? Lini Hasira yao Itakuwa Moto wenye Kuteketeza Umbile la Kiyahudi na Tawala za Mamluki Zinazolilinda?

Wakati Gaza ikiwa inakufa kwa njaa, ikizingirwa kwa kimya cha aibu cha Waarabu na njama ya wazi ya kimataifa, kijana mmoja wa Kimisri kutoka ng'ambo, Anas Habib, alifunga milango ya ubalozi wa Misri nchini Uholanzi na kumwaga unga kwenye kizingiti chake. Alipiga kelele kwa jina la watu waliozingirwa wa Gaza na kuliita jeshi lake nchini Misri kuvunja mzingiro, kufungua kivuko, na kumaliza njaa ya kupangwa... Kilio kutoka nchi ya mbali kilisikika ndani ya nyoyo huru. Je, kuna yeyote kati ya watu wa Misri atakayejibu? Je, kuna ulinzi wowote katika nyoyo za watu wa jeshi la Kinana? Au kufuli zilizowekwa kwenye ubalozi wa Misri jijini The Hague ni za kikatili kidogo kuliko kufuli zilizowekwa kwenye utashi na silaha zao?!

Soma zaidi...

Kuitelekeza Gaza ni Doa katika vipaji vya Nyuso Zenu Enyi Wanajeshi wa Kinana na muhimu zaidi, ni Swali kutoka kwa Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama

Kila siku, mtoto mjini Gaza hufa kwa njaa, au mzee hupumua pumzi yake ya mwisho bila dawa, au mwanamke hufunga macho yake kwa mara ya mwisho kwa maumivu yasiyoweza kuvumilika kutokana na kiu au njaa. Kila saa mbingu hutokwa na machozi, mawe yanapiga kelele, na ardhi inawalaani wale waliowaacha peke yao. Hii ndiyo Gaza... Gaza, ambayo imezingirwa si tu kwa mipaka na vifaru, bali na uzio wa usaliti uliosukwa na viongozi wa majeshi, watawala wa khiyana, na kimya cha Umma wao.

Soma zaidi...

Kuhamishwa kwa Watu wa Arish ni Uhalifu wa Kisiasa Uliojificha kama Maendeleo

Wakati serikali ya Misri ikizungumzia "kuimarisha bandari ya Arish," kuigeuza kuwa bandari ya kimataifa na kuiunganisha na mradi mpya wa ukanda wa kiuchumi, uhalifu wa halisi unafanywa dhidi ya wakaazi wa kitongoji cha Al-Raisa huko Arish. Watu wanalazimishwa kuondoka majumbani mwao chini ya athari ya matingatinga, na nyumba zao zinabomolewa kinyume na matakwa yao kwa kisingizio cha manufaa ya umma. Wanakabiliwa na shinikizo la kisaikolojia na mazungumzo ambayo hayaendani na hadhi ya kibinadamu na yanakiuka kanuni za Kiislamu.

Soma zaidi...

Bwawa la An-Nahdha: Silaha Mpya ya Marekani ya Kuvunja Utashi wa Misri na Kuzuia Ukombozi Wake kutokana na Utiifu

Tangu Ethiopia ilipotangaza ujenzi wa Bwawa la Kuu la Ethiopia la An-Nahda Dam kwenye  Nile ya Samawati mwaka 2011, uhalifu mkubwa wa kisiasa na wa kimkakati umekuwa ukijitokeza. Wale wenye ufahamu wanaona sio tu kama jengo la maji au mradi wa maendeleo, lakini kama chombo kipya cha kikoloni kinachotumiwa na Amerika kutawala eneo hili - hasa Misri, kitovu cha ardhi za Kiislamu, ambayo inakusudiwa kubaki kudhalilishwa chini ya shinikizo la kiuchumi, kisiasa, na hata la maji, kama sehemu ya mtindo mpya wa vita visivyo vya moja kwa moja.

Soma zaidi...

Ajali za Barabarani nchini Misri: Ushahidi Tosha wa Kukosekana kwa Ustawi wa Jamii na Ufisadi wa Mfumo wa Kirasilimali

Katika tukio ambalo limekuwa la kusikitisha, watu waliamka siku chache zilizopita na kushuhudia maafa mengine ambayo yalisababisha vifo vya watu tisa wasio na hatia katika ajali iliyotokea kwenye Barabara ya Kanda katika Jimbo la Monufia, chini ya wiki moja baada ya maafa ya kuhuzunisha ambapo wasichana wachanga kumi na nane waliangamia katika ajali sawia, ikitofautiana na ile ya awali tu na kwa idadi ya wahasiriwa. Barabara ya Kanda - ambayo serikali imekuwa ikiitangaza kwa muda mrefu kama "mafanikio ya kitaifa" - imekuwa shahidi wa kudumu wa upuuzi wa yale yanayodaiwa kuwa mafanikio yanayosifiwa na watawala huku wakijificha nyuma ya mabango ya vyombo vya habari vya uwongo na kupuuza haki msingi ya watu: kuishi kwa usalama kwenye barabara ambazo hazinyakui maisha yao.

Soma zaidi...

Utelekezaji wa Serikali ya Misri wa Gaza: Kuanzia Kuzuia Nusra, Hata wa Maneno, hadi Kushiriki kwa Kizuizi!

Katika mandhari inayojirudia rudia, kwa kila maafa yanayowakumba watu waliozingirwa wa Gaza, tawala za Kiarabu - zinazoongozwa na utawala wa Misri - zinathibitisha kwamba sio tu hazipo katika wajibu wao wa kunusuru, lakini pia ziko katika nafasi ya ulaji njama na usaliti, na hata kushiriki kikamilifu katika mzingiro, kulinda vivuko na kuzuia mradi wowote wakilishi au maarufu kwa lengo la kukandamiza Waislamu.

Soma zaidi...

Kuna Uungwana kutoka Ng'ambo ya Bahari... Uko wapi Uungwana wa Jeshi la Misri?!

Katika wakati ambapo mauaji dhidi ya watu wa Gaza yamezidi, na ardhi kuungua chini ya miguu ya wanyonge, vyombo vya habari vya Marekani vimeandika kichwa cha kikuu habari kuhusu kijana Muislamu kutoka Misri aitwaye Mohammed Sabry Soliman, ambaye alituhumiwa kwa kurusha vinywaji vya Molotov kwenye maandamano ya kuunga mkono umbile la Kiyahudi nchini Amerika, akiimba "Uhuru kwa Palestina." Wakati vyombo vya habari vinajadili tukio hili, kiini cha tukio hili hakiwezi kupuuzwa: kijana Muislamu, aliyehama kutoka ng'ambo ya bahari, akisukumwa na maumivu ya moyo wake na maumivu ya Ummah wake, kueleza kukataa kwake kimya cha kimataifa na kufeli kwa Waarabu kushughulikia hali inayoendelea mjini Gaza.

Soma zaidi...

Mkondo wa Bahari wa Suez: Mtazamo kwa Kauli za Trump na Msimamo wa Utawala wa Misri

Katika onyesho jengine la kiburi, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kwenye jukwaa la "Ukweli wa Kijamii" kwamba meli za Kimarekani zinapaswa kupita kwenye Mikondo ya Suez na Panama bila malipo, akidai kwamba Marekani "iliunda mikondo yote miwili." Alimteua Waziri wake wa Mambo ya Nje kufuatilia makubaliano ambayo yataasisisha matakwa haya ya kikoloni.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu