Mkondo wa Bahari wa Suez: Mtazamo kwa Kauli za Trump na Msimamo wa Utawala wa Misri
- Imepeperushwa katika Misri
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Katika onyesho jengine la kiburi, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kwenye jukwaa la "Ukweli wa Kijamii" kwamba meli za Kimarekani zinapaswa kupita kwenye Mikondo ya Suez na Panama bila malipo, akidai kwamba Marekani "iliunda mikondo yote miwili." Alimteua Waziri wake wa Mambo ya Nje kufuatilia makubaliano ambayo yataasisisha matakwa haya ya kikoloni.