Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
H. 19 Muharram 1447 | Na: HTS 1447 / 03 |
M. Jumatatu, 14 Julai 2025 |
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Mashambulizi ya "Warefu Tisa" yatamalizwa tu kwa Utekelezaji wa Adhabu za Sharia chini ya Dola ya Khilafah
(Imetafsiriwa)
Habiba Al-Amin, mwandishi wa habari wa tovuti ya Kush News, alishambuliwa vikali na wanachama wa genge la "Warefu Tisa" katika eneo la kivuko kwenda Port Sudan alipokuwa akiregea kutoka kwenye uangaziaji wa habari akiwa na wenzake kadhaa. Hili ni moja tu ya matukio mengi ya uporaji, ujambazi na mauaji katika miji inayodaiwa kuwa salama, kama vile Omdurman, Khartoum, na sasa mji mkuu wa utawala, Port Sudan. Hii ni miji iliyo chini ya udhibiti wa serikali na vyombo vyake vya usalama.
Hata hivyo, wahalifu hushambulia kwa ujasiri wote, kana kwamba wanajiamini kuwa mkono wa serikali hautawafikia, na ukiwafikia, wanatulizwa na udhaifu wa adhabu ya hafifu, licha ya ukubwa wa uhalifu unaofanywa.
Hakuna shaka kwamba kuenea kwa uhalifu kunaweza tu kuzuiwa na utekelezaji wa adhabu zilizowekwa kisheria. Kanuni ya kisheria ni kwamba "adhabu zilizoadhibiwa ni vizuizi na tiba." Zinazuia kutendwa kwa uhalifu na kutoa msamaha kwa wale walioadhibiwa, na kuwapunguzia mateso kesho Akhera.
Kutoka kwa Abdullah bin Omar amesema: «قطعَ النَّبيُّ ﷺ في مِجَنٍّ قيمتُهُ ثلاثةُ دراهمَ» “Mtume (saw) alikata (mkono wa mwizi) kwa ngao yenye thamani ya Dirham tatu.” Imepokewa na Ibn Majah kwa maneno haya.” (Imepokewa na Al-Bukhari na Muslim). Katika riwaya nyingine: «أنَّ النبيَّ ﷺ قطعَ يدَ رجلٍ سرقَ تُرساً من صُفَّةِ النساءِ ثمنُهُ ثلَاثة دراهم « “Mtume alikata mkono wa mtu aliyeiba katika sehemu iliyotengewa wanawake ngao ambayo thamani yake ilikuwa dirham tatu.” (Sahih Abi Dawood, Al-Nasa’i na wengineo).
Ama wale wanaotishia usalama, na kutekeleza mauaji, ubakaji, uporaji na ufujaji, kwa nguvu ya silaha, kama ilivyokuwa kwa genge la "Warefu Tisa", aya tukufu zilikuja kuwaonya na kuwazuia. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
[إِنَّمَا جَزَاءُ الَّذِينَ يُحَارِبُونَ اللهَ وَرَسُولَهُ وَيَسْعَوْنَ فِي الْأَرْضِ فَسَاداً أَن يُقَتَّلُوا أَوْ يُصَلَّبُوا أَوْ تُقَطَّعَ أَيْدِيهِمْ وَأَرْجُلُهُم مِّنْ خِلَافٍ أَوْ يُنفَوْا مِنَ الْأَرْضِ ذَٰلِكَ لَهُمْ خِزْيٌ فِي الدُّنْيَا وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٌ]
“Basi malipo ya wale wanao mpiga vita Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakawania kufanya uchafuzi katika nchi, ni kuuwawa, au kusalibiwa, au kukatwa mikono yao na miguu yao kwa mabadilisho, au kutolewa nchi. Hii ndiyo hizaya yao katika dunia; na katika Akhera watapata adhabu kubwa.” [Al-Ma'idah 5:33]. Ikiwa serikali ingetekeleza adhabu moja tu, wahalifu wote wangezuiliwa. Hata hivyo, inaonekana kwamba hii ni heshima ambayo haistahili. Kwa hiyo, tunaiona ikizunguka raundi, ikiamini kwamba kumteua Waziri wa Mambo ya Ndani, kupeleka polisi katikati mwa jiji la Cairo, au kuandaa kampeni za kuzuia kutaleta mabadiliko. Badala yake, hali inazidi kuwa mbaya zaidi. Hukmu za Sharia hutabikishwa tu chini ya dola ya Kiislamu – Khilafah Rashida, kwa msingi wa mafundisho ya Mtume. Hii pekee ndio inaweza kuzuia na kuwaadhibu wahalifu. Mifumo ya kidemokrasia, hata hivyo, huzaa wahalifu, kukuza uhalifu, na kukuza ufisadi kutokana na adhabu zao dhaifu. Wanaamini kuwa wao ni wenye huruma zaidi kwa watu kuliko Muumba wao, na hakuna dhambi kubwa zaidi kuliko ukafiri.
Je, watu wenye uwezo na nguvu katika nchi yetu wataitikia wito wa Mwingi wa Rehema, na kutoa nusrah (msaada) kwa Hizb ut Tahrir, kuweka kiapo cha utiifu (Shari’ bayah) kwa Khalifa muongofu ambaye atasimamisha uadilifu, kueneza usalama, na kuwazuia wahalifu, wakubwa kwa wadogo, katika kutimiza kauli ya Mtume: «وإنَّما الإمَامُ جُنَّةٌ يُقَاتَلُ مِن ورَائِهِ ويُتَّقَى به» “Hakika Imamu (kiongozi wa Waislamu) ni ngao yao. Watu hupigana nyuma yake na kujihami kwaye (kutokana na madhalimu na wavamizi)”?!
[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ]
“Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele.” [Al-Anfal 8:24]
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan
Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari Wilayah Sudan |
Address & Website Tel: 0912240143- 0912377707 http://www.hizb-sudan.org/ |
E-Mail: Spokman_sd@dbzmail.com |