Ijumaa, 24 Rabi' al-awwal 1446 | 2024/09/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Je, Tunapaswa Kuzingatia Maneno Yako Mazuri au Matendo Yako Mabaya!

Katika hotuba yake katika Programu ya Ufunguzi wa Wiki ya Mawlid al-Nabi Rais Erdoğan alisema, “Mtu pekee katika ulimwengu huu ambaye tunamuiga, tunafuata nyayo zake na ambaye tunajitolea maisha yetu kwake ni Mtume wetu wa Mwenyezi Mungu. Yeye ndiye kiongozi wetu na kipenzi chetu ambaye tutakufa kwa ajili yake. Mola wetu atujaalie tutembee katika nyayo za Mtume wa Mwenyezi Mungu, tujenge shakhsiya yetu kwa maisha yake, na tuwe na maadili mema ya kupigiwa mfano.”

Soma zaidi...

Mabadiliko Ndio Fikra Inayopiganiwa Zaidi katika Historia

Barabara za Kenya zilisalia kuwa uwanja wa vita huku maandamano, yaliyochochewa na ongezeko la ushuru lenye utata, yakibadilika na kuwa kilio kikubwa dhidi ya tofauti za kiuchumi zilizokita mizizi na kukosekana kwa uwajibikaji wa serikali. Mstari wa mbele wa vuguvugu hili ni kizazi cha vijana wa Kenya, wanaokataa kunyamazishwa licha ya kukabiliwa na msako mkali wa polisi.

Soma zaidi...

Uzbekistan: Faini za Mamilioni ya Soum kwa Kuwafunza Watoto Uislamu

Mnamo Juni 25, wawakilishi wa Oliy Majlis ya Jamhuri ya Uzbekistan walipitisha katika usomaji wa kwanza mswada unaokataza wazazi kupeleka watoto wao kusoma katika mashirika ya kidini ambayo hayajasajiliwa au kwa watu binafsi bila kibali kinachofaa. Mswada huo ulianzishwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Jamhuri ya Uzbekistan.

Soma zaidi...

Mwito wa Mabadiliko: Uislamu Mfumo pekee Usiocheza Shere na Kuhujumu Maisha ya Watu

Kenya, imekumbwa na maandamano makubwa katika masiku ya hivi majuzi baada ya bunge kupitisha mswada wa kuongeza ushuru – ikiwa ni pamoja na mahitaji ya kila siku kama vile mafuta ya kupikia, nepi, na mkate – kwa idadi ya watu ambao tayari wanakabiliwa na mfumko wa bei na viwango vya juu vya ukosefu wa ajira. Rais Ruto alikataa kutia saini mswada huo baada ya maandamano makubwa ambayo kufikia sasa watu 39 wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa.

Soma zaidi...

Onyesho la Mshikamano nchini Malaysia huku Hali mjini Gaza Ikizidi kuwa Mbaya

Hali mjini Gaza inazidi kuwa mbaya. Umbile haramu la Kiyahudi linaendelea na mashambulizi yake, na kusababisha idadi ya vifo ambayo sasa imefikia 37,000, na zaidi ya 82,000 kujeruhiwa. Inajulikana sana kuwa hakuna maeneo salama kabisa yaliyosalia kwa wakaazi wa Gaza kutafuta kimbilio kutokana na mashambulizi ya umbile hilo haramu la Kiyahudi. Takriban Waislamu wote wa Gaza sasa wanalazimika kuyahama makaazi yao, wakitafuta hifadhi hadi kusini mwa Rafah, karibu na mpaka wa Misri.

Soma zaidi...

Vifo vya Hajj ni Kosa la Utawala wa Saudi kutokana na Ukosefu wao wa Ustawi kwa Wageni wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu

Zaidi ya mahujaji Waislamu 1,300 waliripotiwa kufariki wakati wa Hija ya kila mwaka, au hija ya Makka, mwezi huu nchini Saudi Arabia, ambapo halijoto imepanda zaidi ya nyuzi joto 50 (nyuzi 122 za Fahrenheit). Mfiduo usiodhibitiwa wa joto kali unaweza kusababisha aina mbalimbali za madhara ya kiafya yanayojulikana ikiwemo kufeli kwa viungo vya mwili na hata kifo.

Soma zaidi...

Mashirika ya Leo ya Vyombo vya Habari si Chochote isipokuwa ni Chombo cha Dola Ovu za Kilimwengu

Ingawa vyombo vya habari vinaitwa “nguzo ya nne ya demokrasia,” vikionyesha kutoegemea upande wowote na fikra yake, kama mamlaka ya mahakama kwa mfano, uhalifu uliofanywa na serikali ya Kiyahudi huko Gaza, na katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, ulitosha kufichua madai haya. Uhalifu huo ulifichua ukweli kuhusu vyombo vya habari na wanahabari. Jinai hizo zilionyesha wazi kwamba hakuna mamlaka ya kimaadili au uhalali, bali kwa ajili ya nguvu ya unyama, inayowakilishwa na dola za kimataifa na silaha zao duniani, ikiwemo Ulimwengu wa Kiislamu, ikiwa ni pamoja na watawala, serikali, na taasisi za vyombo vya habari.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu