Jumatatu, 16 Rajab 1447 | 2026/01/05
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Unafiki wa Magharibi; Kati ya Kulaani Tukio la Sydney, na Kimya Juu ya Mauaji katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina

Bado hakuna kiongozi hata mmoja wa nchi au kiongozi wa Magharibi au wa Kiarabu ambaye hajashutumu tukio la Sydney, ambapo watu kumi na tano waliuawa kwa kupigwa risasi kufuatia shambulizi lililolenga tamasha la Mayahudi la Hanukkah jijini Sydney. Hata hivyo hatujaona azma mithili ya hiyo katika kulaani jinai za umbile la Kiyahudi katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina katika kipindi cha miaka miwili iliyopita. Kama kawaida, rai jumla ya umma imepotoshwa, na kupuuzwa kabisa nia ya tukio hilo, kwani kila mtu alijikita kukemea kitendo hicho, bila kujali sababu iliyowafanya washambuliaji hao wawili kuwafyatulia risasi washerehekaji.

Soma zaidi...

Watawala wa Waislamu Wameshikana Mkono kwa Mkono na Marekani na Mayahudi Kupitisha Mipango Yao, Na kwa Kauli na Shutma Tupu Pamoja na Waislamu

Umbile la Kiyahudi linaendelea kutekeleza jinai zake dhidi ya Gaza, Ukingo wa Magharibi, Lebanon na Syria; kumuua limtakaye, kupiga mabomu popote lipendapo, kubomoa nyumba na vituo, kujenga makaazi, na kuwaandama watu katika nyumba na ardhi zao, huku watawala wa Waislamu wakiendelea na misimamo yao ya fedheha ya kula njama na kurahisisha mambo kwa ajili yake, wakicheza dori ya mwangalizi na mwandishi wa habari anayeripoti habari na kutoa maoni yake kwa misemo isiyozuia wala kutibua njama.

Soma zaidi...

Unyanyasaji wa Kimpangilio wa Kijinsia Dhidi ya Wanawake wa Sudan Hautoi Jibu lolote kwa Kukosekana kwa Dola Inayojali Heshima ya Mwanamke Mwislamu

Mnamo Alhamisi tarehe 11 Disemba, shirika, ‘The Strategic Initiative for Women in the Horn of  Africa’, liliripoti kuwa limerekodi karibu matukio 1300 ya unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake katika majimbo 14 nchini Sudan tangu vita vianze nchini humo mnamo Aprili 2023, huku Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vikilaumiwa kwa 87% ya visa hivi. Lilielezea unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake ukitumika kama silaha ya kimfumo katika mzozo huo, likisema “umeenea, unarudiwa rudiwa, unakusudiwa na mara nyingi unalenga”. Ubakaji ulichangia robo tatu ya matukio yaliyorekodiwa, huku visa 225 vikihusisha watoto, baadhi wakiwa na umri wa miaka 4. Matukio yalitokea majumbani, maeneo ya umma na pia yalijumuisha kizuizini cha muda mrefu cha wanawake ambao waliteswa, kubakwa na genge na ndoa za kulazimishwa. Mnamo Jumapili tarehe 7 Disemba, vikundi vya matibabu vya Sudan viliripoti kwamba watoto na wanawake kadhaa walinyanyaswa kingono na kubakwa walipokuwa wakikimbia kukamatwa kwa El Fasher huko Darfur na RSF Oktoba hii.

Soma zaidi...

Vita vya Amerika dhidi ya Uislamu

Utawala wa Marekani na watoaji maamuzi ndani yake hawaachi kuonyesha uadui wao dhidi ya Uislamu na kufichua vita vyao vinavyoendelea na anuwai dhidi yake. Katika kila tukio na bila ya tukio, utamsikia afisa wa Marekani akipaza sauti yake kuushambulia Uislamu, akiuelezea kwa maelezo yanayofichua ukubwa wa chuki yao dhidi yake na kuashiria ukubwa wa utisho unaojaza nyoyo zao kutokana na Uislamu.

Soma zaidi...

Chuo Kikuu cha Al-Quds Kinafanya Kongamano kwa Ufadhili wa Magharibi na Programu Iliyoundwa na Magharibi Chini ya Kauli Mbiu “Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake”

Mnamo Jumanne, 2 Disemba 2025, Kitivo cha Sheria katika Chuo Kikuu cha Al-Quds – Abu Dis kilizindua kongamano la kimataifa lililopewa kichwa “Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake: Changamoto, Masuluhisho, na Mbinu Bora katika Eneo la Mediterania,” kwa ushirikiano na Wizara ya Masuala ya Wanawake ya Palestina, Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya Kupambana na Ukatili Dhidi ya Wanawake, Shirika la Idadi ya Watu la Umoja wa Mataifa (UNFPA), na Chuo Kikuu cha Perugia, Italia, kwa usaidizi wa ushirikiano wa Italia.

Soma zaidi...

Je, Watoto Wafungwa Katika Magereza ya Uvamizi ni Watoto au Wanaume?!

Taasisi za Palestina zinazohusika na masuala ya wafungwa, ikiwemo Klabu ya Wafungwa, zilisema kwamba zaidi ya watoto 1630 kutoka Ukingo wa Magharibi, ikiwa ni pamoja na al-Quds, na makumi kadhaa kutoka Ukanda wa Gaza wamekamatwa na uvamizi tangu mwanzo wa vita dhidi ya Gaza. Waliashiria kuuawa shahidi kwa mtoto mmoja ndani ya Gereza la Megiddo baada ya kukabiliwa na njaa, kunyimwa, na unyanyasaji. 350 kati yao bado wako katika magereza ya uvamizi, wakiwemo wasichana wawili, katika hali ngumu ambazo zinagongana kabisa na viwango vyote vya kimataifa vya ulinzi wa watoto. Wanakabiliwa na uhalifu wa mateso, njaa, na kupuuzwa kimatibabu, vilevile kudhulumiwa kijinsia, pamoja na kutengwa kwa pamoja na kunyimwa kutembelewa.

Soma zaidi...

Waislamu Maskini Wanastahili Zaidi Uwekezaji wa Watawala Wapumbavu Kuliko Amerika

Mfalme Mtarajiwa wa Saudi Arabia alifanya ziara nchini Marekani mnamo Jumanne, 18/11/2025, ambapo alionyesha kiwango cha upumbavu wake katika kufuja utajiri wa Ummah, kiwango cha utiifu wake kwa bwana wake Amerika, pamoja na kiwango cha usaliti wake kwa Ummah wa Kiislamu, njama yake dhidi yake, na vita vyake dhidi ya Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume Wake (saw) kwa kukubali kujiunga na Makubaliano ya Abraham, yaliyowekwa katika usaliti mwingine ambao unahakikisha njia iliyo wazi ya suluhisho la dola mbili.

Soma zaidi...

Ukosefu wa Masuluhisho ya Kudumu kwa Mgogoro wa Rohingya

Gazeti la ‘South China Morning Post’ liliripoti mnamo tarehe 10 Novemba kwamba Umoja wa Mataifa umeonya kwamba Kusini-mashariki mwa Asia kuna hatari ya “janga jengine la kibinadamu” ikiwa uvukaji wa bahari wa wakimbizi waliokata tamaa utaendelea bila kudhibitiwa. Vifo vya watu wasiopungua 21, wakiwemo watoto kadhaa, katika ajali ya boti karibu na pwani ya Malaysia vimeibua hofu ya kuongezeka tena kwa uvukaji hatari wa bahari wa wakimbizi wanaokimbia mzozo nchini Myanmar na hali mbaya katika nchi jirani ya Bangladesh. Kulikuwa na miili 12 iliyopatikana nchini Malaysia na tisa katika nchi jirani ya Thailand – kulingana na mkuu wa eneo wa shirika la bahari la Malaysia, Romli Mustafa.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Maisha Yenu Yanawezaje Kuwa Mazuri Wakati Wanawake Walio Huru Wako Katika Magereza ya Mayahudi, Wakiteswa na Heshima Zao Zikivunjwa?!

Kituo cha Haki za Kibinadamu cha Palestina kilifichua, kulingana na ushuhuda mpya uliokusanywa na mawakili na watafiti wa kituo hicho kutoka kwa wafungwa kadhaa walioachiliwa huru kutoka Ukanda wa Gaza kutoka magereza na vituo vya uzuizi vya umbile la Kiyahudi, utaratibu na mpangilio wa mateso ya kingono, ikiwemo ubakaji, kuvua nguo, kulazimishwa kurekodi filamu, na unyanyasaji wa kingono kwa kutumia zana na mbwa, pamoja na udhalilishaji wa kisaikolojia wa makusudi unaolenga kuponda utu wa binadamu na kufuta kabisa kitambulisho cha mtu binafsi.

Soma zaidi...

Rais wa Slovenia Hajui Historia, au Anaipuuza!

Hii ilikuwa katika mahojiano na Kituo cha Al Jazeera mnamo 9/11/2025, ambayo kituo kilitangaza kikamilifu asubuhi ya 10/11/2025. Kutoka ardhi ya Waislamu huko Qatar, Rais wa Slovenia, Nataša Pirc Musar, anasema: “Israel ina haki ya kuwa na dola.” Swali linaloelekezwa kwa rais ni: Ni nani aliyelipa umbile hili haramu la Kiyahudi haki hii? Na je, kuna mtu yeyote anayesoma historia na hajui jinsi umbile hili lemavu lilivyoanzishwa katika ardhi iliyobarikiwa ya Palestina? Je, mauaji ya Mayahudi dhidi ya Waislamu, watu wa Palestina, yanaondoka akilini mwa msomaji yeyote adilifu wa historia? Umbile hili lemavu lilisimamishwaje juu ya mafuvu na maiti za watu wengi wa Palestina?

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu