Ijumaa, 24 Rabi' al-awwal 1446 | 2024/09/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Nchini Urusi, Wanawake wa Kiislamu Waliojistiri Wanakamatwa na Kufanyiwa Ukatili!

Mnamo Septemba 18, 2024, vyombo vya habari vya Urusi viliripoti uvamizi na ukamataji huko Tatarstan unaohusisha kina dada wanne Waislamu wanaotuhumiwa kuwa wa Hizb ut Tahrir. Wanakabiliwa na vifungo vya jela kwa zaidi ya miaka kumi chini ya Kifungu cha 205/5 cha sheria ya Shirikisho la Urusi. Kina dada hao, Leysan Sadykova (Лейсан Садыкова), Aliya Vaisova (Алия Ваисова), Alsina Khairullina (Альсина Хайруллина), na Albina Vali Akhmetova (Альбина Валиахметова).

Soma zaidi...

Kauli za Aibu za Waziri wa Mambo ya Nje wa Jordan

Kufuatia mkutano wa ile inayoitwa “Kamati ya Mawaziri wa Kiarabu na Kiislamu iliyopewa jukumu la kuchukua hatua za kimataifa kukomesha vita dhidi ya Gaza,” Waziri wa Mambo ya Nje wa Jordan Ayman Safadi alitoa kauli za aibu kwa waandishi wa habari ambazo haziendani na uzito wa tukio ambalo kwalo walikuwa wamekusanyika.

Soma zaidi...

Barua ya Wazi kwa Watu Wenye Nguvu katika Majeshi ya Waislamu Kutoka kwa kina Mama, Dada na Mabinti wa Ummah wa Kiislamu ili Kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina

Huu ni ujumbe kwa ndugu zetu, baba zetu na watoto wetu wanyoofu katika majeshi ya nchi za Kiislamu kutoka kwa wanawake wa Umma huu mtukufu wa Kiislamu. Tunakuhutubieni kama wale ambao wamepewa wajibu na Mola wa Walimwengu wote (swt) kuwalinda Waislamu na kulinda heshima yetu. Tunakuhutubieni kama watu wenye uwezo wa kukomesha mauaji ya Ummah wetu.

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Kinachapisha Barua ya Wazi kwa Majeshi ya Waislamu ili Kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina

Takriban watu 40,000 wameuwawa mjini Gaza katika kipindi cha miezi 10 iliyopita, wengi wao wakiwa wanawake na watoto, huku serikali za ulimwengu, zikiwemo nchi za Waislamu zikitazama kama watazamaji pekee wa mauaji haya ya umwagaji damu, bila ya dhamira yoyote ya kisiasa ya kukomesha mauaji hayo. Hakika, tawala nyingi za ardhi za Kiislamu kwa miongo kadhaa zimeimarisha mkono wa uvamizi wa Kiyahudi kupitia mikataba yao ya amani, kuhalalisha mahusiano ya kidiplomasia, na ushirikiano wa kiuchumi na umbile hili la mauaji ya halaiki.

Soma zaidi...

Udungaji Visu Mgongoni mwa Umma Unaendelea kutoka kwa Watawala Vibaraka Ruwaibidha wa Waislamu!

Ufalme wa Al Saud unaregesha udungaji visu wake mgongoni mwa Umma wa Kiislamu kwa kushirikiana na watawala wa Ruwaibidha (watepetevu na wazembe) katika nchi za Kiislamu kupitia mbio zao za kuhalalisha mahusiano na umbile nyakuzi, licha ya jinai zote za mauaji ya halaiki na uhangaishaji Waislamu katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi unaofanywa na umbile hilo katili.

Soma zaidi...

Watoto wa Palestina Watakuwa Mahasimu wa Ummah na Majeshi Yake Siku ya Kiyama iwapo Hawatasonga Kuwanusuru

Msichana mwenye umri wa miaka 13, Bana Amjad Bakr, aliuawa shahidi baada ya kupigwa risasi kifuani na wanajeshi wavamizi jioni ya Ijumaa, Septemba 6, 2024, wakati wa shambulizi la walowezi, wakisaidiwa na vikosi vya uvamizi, kwa kijiji cha Qaryut, kusini mwa Nablus katika Ukingo wa Magharibi.

Soma zaidi...

Chini ya Uongozi wa Watawala Ruwaibadha wa Waarabu na Waislamu, Majeshi na Uwezo wa Kijeshi wa Ummah Yamekuwa kwa ajili ya Maonyesho Tu!

Vyombo vya habari vya kidijitali na satelaiti vinasambaza habari kila mara za mazoezi ya kijeshi ya majeshi makubwa katika miji mikuu ya nchi za Kiislamu, ambapo ujuzi wao, silaha na visasisho vinaonyeshwa. Taarifa hizi za habari huanza kwa kuonyesha jinsi gani majeshi haya hayakosi uzoefu, teknolojia au vifaa vinavyohitajika kwa nchi yoyote kuwa kubwa, kuanzia kwa askari wenye uwezo ambao wamefunzwa kwa ukali.

Soma zaidi...

Ardhi Iliyobarikiwa - Palestina Sio Karata ya Uchaguzi kwa Ruwabidha Mzembe

Mnamo siku ya Jumatatu, tarehe 19/8/2024, Rais wa Algeria Abdelmadjid Tebboune alitoa wito kwa Misri kufungua mipaka na Ukanda wa Gaza kwa jeshi la Algeria, ili kuwanusuru wakaazi wa Ukanda wa Gaza, na kusema: “Naapa kwamba haraka iwezekanavyo tutapeleka vitengo huko na kujenga upya kile kilichoharibiwa,” na akasema: “Jeshi la Algeria liko tayari kwenda Gaza na sisi tuko tayari, tunasubiri tu Misri itufungulie mipaka yake.”

Soma zaidi...

Damu za Waislamu zinamwagika huku watawala wao wakishuhudia na hakuna suluhu!

Umbile la Kiyahudi linaendeleza uvamizi wake dhidi ya watu wa Palestina na linaendelea na jinai zake mbele ya masikio na macho ya walimwengu, bila kuzuiwa na azimio au hukumu yoyote ya Umoja wa Mataifa kutoka Mahakama ya Kimataifa. Idadi ya mashahidi waliohesabiwa imezidi 40,000, na pengine idadi sawia bado wamenaswa chini ya vifusi. Idadi ya waliojeruhiwa inakaribia 100,000, huku wale waliosalia wakiwa hai wanateseka sana kutokana na njaa.

Soma zaidi...

Serikali ya Jordan Kuanzisha Afisi ya NATO ni Uhalifu dhidi ya Palestina na Gaza na Usaliti kwa Umma wa Kiislamu

Huku Wamagharibi wakikata tamaa ya uwezo wa tawala vibaraka katika nchi za Kiislamu kuendelea kudhibiti na kutawala mambo, na uhakika wake kwamba Ummah unakaribia kuzifagilia mbali tawala hizi na kuziondoa, na hivyo kuondoa uwepo wao katika nchi zetu; kwa kuzingatia haya yote, hatua hii ilitoka kwa NATO, ili wao wenyewe waweze kusimamia utekelezaji wa mipango yao na kulinda maslahi yao katika ardhi zetu, na kulinda umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu