Ramadhan, Fursa ya Kutafakari na Kubadilika
- Imepeperushwa katika Uchambuzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Ramadhani ni mwezi wa kheri na baraka, na fursa adhimu ya kujitahidi kupata mafanikio ya duniani na akhera. Ni msimu wa utiifu, na uwanja wa kushindana katika mambo ya kheri na kufikia uchamungu ili kupata radhi za Mwenyezi Mungu, ambayo ndio mafanikio ya kweli. Ni mwezi maalum wa fadhila, si kwa sababu tu ni mwezi wa saumu na ibada, bali pia kwa sababu ni fursa adhimu ya kutafakari uhusiano wetu na Mwenyezi Mungu na kutathmini upya mwenendo wa maisha yetu ili kubadilika na kuwa bora zaidi, na kuzingatia malengo yetu ya kweli na kufafanua fahamu ya mafanikio katika maisha yetu, si kwa mtazamo wa Kidunia, bali kwa mtazamo wa kidini, kiroho na kiakhlaqi.