Jumatatu, 19 Muharram 1447 | 2025/07/14
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Njama Endelevu, Iliyoimarishwa ya Kimataifa ya Kuzuia Mapinduzi ya ash-Sham yasifikie Malengo na Misingi yake

Mwenyezi Mungu (swt) alipowapa watu wa ash-Sham baraka za kumwangusha dhalimu mhalifu wa Syria, asubuhi ya tarehe 8 Disemba 2024, licha ya mipango na njama kubwa zilizopangwa na ulimwengu wote wa Magharibi, ukiongozwa na Marekani, ili kuyabatilisha mapinduzi na kuyazuia yasifikie lengo lake, ulikuwa ni utashi, azma, na Iman ya watu ash-Sham, kwa zana zao hafifu na za kawaida, ambapo hatimaye walishinda dhidi ya jumuiya ya kimataifa.

Soma zaidi...

Je! Uongozi wa Pakistan Ulipotezaje Hadhi Yake Mbele ya India na Trump?!

Uongozi wa kisiasa na kijeshi wa Pakistan ulipoteza ushindi uliopatikana na mwewe wa Jeshi lake la Anga, na simba wa jeshi lake la nchi kavu, juu ya India mnamo Mei, ikitoa funzo ambalo India haitalisahau kamwe, kwa kukubali kusitishwa kwa mapigano kati ya nchi hizo mbili. Hii ni licha ya msisitizo wa India kusitisha Mkataba wa Maji wa Indus, na kuinyima Pakistan karibu 80% ya maji ambayo hutiririka kutoka kwa Mto Indus, ambao unatoka China, unapitia India, na kisha kuingia Pakistan. Hii pia ni licha ya kwamba India bado inaendelea kuikalia kimabavu Kashmir... Kisha, baada ya upatanishi wa Rais wa Marekani, Donald Trump kuweka usitishaji vita kati ya pande hizo mbili, na kuiokoa India kutokana na mtego iliyokuwa imejiwekea, kutokana na hesabu potofu ya mienendo ya madaraka, serikali ya Pakistan ilitangaza, mnamo tarehe 21 Juni 2025, uteuzi wake wa Rais wa Marekani Donald Trump kwa ajili ya Tuzo ya Amani ya 2026, ikidai ni kutokana na “kuhusika kwake pamoja na Islamabad na New Delhi ambako kulipunguza hali iliyokuwa ikizorota kwa kasi” kati ya Pakistan na India mwezi Mei.

Soma zaidi...

Maumbile ya Mahusiano kati ya Uingereza na Urusi

Maumbile ya mahusiano kati ya Uingereza na Urusi yamekuwa makali na yenye taharuki tangu karne ya 18, na uadui wa wazi na dhahiri kati yao. Kwa mfano, Dmitry Medvedev, Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Urusi, alisema mnamo Aprili 21, 2023, "Uingereza daima imekuwa, na sasa, na itakuwa adui yetu wa milele. Angalau hadi wakati ambapo kisiwa chao chenye majivuno kitazama ndani ya shimo la bahari kutokana na wimbi lililochochewa na mfumo wa kivita wa Urusi."

Soma zaidi...

Kutoka Pakistan hadi ash-Sham: Je, Kweli Tulimshinda Bashar au Tulimbadilisha tu kwa Nakala zake?!

Wakati miji yote ilipokombolewa kutoka mikononi mwa dhalimu wa ash-Sham, Bashar, tulifikiri ushindi ulikuwa umefika. Tuliamini kuwa wakati umefika wa kusimamishwa Khilafah kwa njia ya Utume—hali ile ile iliyobashiriwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw)—ambayo itatawala kwa Qur’an na Sunnah na ilionekana iko tu kwenye kona. Walakini, kuvunjwa moyo kulilingana na ukubwa wa mihanga, na usaliti ulifuata takriban miezi sita baada ya wanamapinduzi kuingia Damascus kwa takbira na shangwe za ushindi. Usaliti ulikuja kutoka kwa wale tuliotarajia wangejenga upya juu ya magofu—sio kujisalimisha kwao!

Soma zaidi...

Mstari Mwekundu wa Unafiki: Jinsi Mauaji ya Halaiki mjini Gaza, Yanavyofichua Nyuso

Mnamo Jumamosi, tarehe 17 Mei 2025, kitovu cha kisiasa cha Uholanzi kiligeuka kuwa chekundu. Maelfu ya watu walijiunga na maandamano jijini The Hague, ambapo mstari mwekundu wa ishara ulichorwa - mstari unaoashiria mpaka wa maadili wa kile ambacho bado kingali kinaweza kutetewa. Kichocheo hakikuwa tu ushiriki wa ‘Israel’ katika Shindano la Nyimbo la Eurovision, bali zaidi ya yote ni kuongezeka kwa hasira juu ya baa la njaa mjini Gaza na kutochukua hatua kwa aibu kwa serikali za Magharibi.

Soma zaidi...

Harakati ya Taliban na Fursa ya Kusimamisha Khilafah

Maisha haya ya dunia ni kama dimbwi la hasara, ambalo ni wale tu wanaojua kukamata fursa ndio wataokolewa. Kwa sababu hii, Siku ya Kiyama inaitwa “Siku ya Majuto,” kwa sababu watu wengi wamezama katika hasara ya kidunia, na wameshindwa kutumia fursa za thamani walizopewa katika maisha yao. Walipoteza kwa urahisi nyakati za dhahabu alizozitoa Mwenyezi Mungu (swt) kwa ajili ya mwamko na izza ya Umma.

Soma zaidi...

Mafanikio ya Kweli Mpaka Siku ya Mwisho ni kwa Umma wa Kiislamu Pekee

Hata leo, katikati ya misiba isiyohesabika na isiyoweza kuvumilika, Ummah huu umethibitika kuwa thabiti katika kitambulisho chake na hivyo hauwezi kuangamizwa. Imethibitika kuwa unastahiki vyeo ulivyotunukiwa na Mola wa walimwengu, Mwenyezi Mungu Azza wa Jall! Angalia Kashmir, India, Afghanistan... Angalia Waislamu wa Syria, Turkestan Mashariki, Myanmar, katika nchi za Afrika, duniani kote, na mwisho kabisa Waislamu wa Palestina na hasa Gaza! Magaidi hao wa Kizayuni wameshindwa katika kila lengo lao kuhusu Gaza. Ummah huu umethibitisha mara kwa mara, kwamba uwepo wake hauzimiki! Hata adui zake wawe wakatili kiasi gani!

Soma zaidi...

Je, Mafanikio kwa Waislamu yanaweza Kupatikana kupitia Siasa za Kidemokrasia?

Kutokana na mauaji makubwa ya halaiki yanayotokea Gaza na dori ya Marekani katika kusaidia na kuunga mkono yaendelee, kumekuwa na mijadala mingi miongoni mwa Waislamu kuhusu jinsi ya kujihusisha zaidi kisiasa na jinsi jamii ya Kiislamu inavyoweza kuwa mstari wa mbele katika kuunda siasa za Marekani ili kubadilisha dunia kuwa bora. Ndani ya mijadala hii, mengi yanasemwa kuhusu kujishughulisha na uraia, kujiunga na kuunga mkono wagombea mahususi wa kisiasa, kunyima kura zao kama aina ya adhabu, na hatimaye kupata Waislamu zaidi, au "washirika" kwenye nyadhifa katika ngazi za dola na majimbo. Kuna gumzo hata miongoni mwa kina dada wakidai kwa furaha kwamba wanajaribu kumlea kijana au binti yao kuwa Rais wa kwanza wa Marekani Muislamu. Haya yanawekwa kama mafanikio sio tu kwa Waislamu wa Amerika, lakini Waislamu kote ulimwenguni. Huu unawekwa kama mpango wa mafanikio licha ya ukweli kwamba vyama vyote vya kisiasa, iwe vya rangi ya samawati, nyekundu, au kijani vinaunga mkono umbile la Kizayuni, au dola zengine zenye kufanya mauaji ya halaiki mithili ya China na India.

Soma zaidi...

Wanawake Waliofaulu katika Uislamu wana Sifa hizi

Katika Uislamu, hakuna fahamu ya kuingia Jannat kulingana na nani unamjua na hadhi yako ya kidunia ni ipi. Wote walisifiwa na Mwenyezi Mungu (swt) kwa sababu ya sifa zao za pamoja za kuwa karibu katika utendaji wao wa kuwa kama mfano wa Mtume (saw). Ikiwa tunataka hadhi sawa ya kuingia Jannat lazima basi tufuate mfano wao wa kufanikiwa. Sifa zifuatazo basi zinahitajika.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu