Mashahidi Watatu Jijini San Diego: Matunda ya Chuki dhidi ya Uislamu
- Imepeperushwa katika Amerika
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Nyoyo zetu zimejaa huzuni kufuatia mauaji ya kusikitisha ya Waislamu watatu katika msikiti mmoja jijini San Diego wakati wa siku takatifu za kwanza za Dhul Hijjah, miongoni mwa siku takatifu zaidi katika kalenda ya Kiislamu. Familia na jamii zinapojiandaa kwa Idd al-Adha, wakati wa ibada, kujitolea muhanga, na umoja, waumini wasio na hatia badala yake walikutana na vurugu na chuki ndani ya nyumba ya Mwenyezi Mungu (swt).



