Ijumaa, 03 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/05/30
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Katikati ya Tabasamu za Idd na Machozi ya Gaza: Wito kwa Maafisa na Wanajeshi

Huku Waislamu wakijiandaa kukaribisha Idd al-Adha na kusherehekea pamoja na watoto wao na wenza wao katika siku hizi za sherehe, tunaelekeza ujumbe huu makhsusi kwa wanajeshi na maafisa wanyoofu wa jeshi la nyuklia la Pakistan, na majeshi mengine ya Ummah kwa jumla. Tunawakumbusha katika siku hizi kwamba wamewatelekeza watu wao wenyewe, wanawake, watoto, wazee, na wanaume katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina na Gaza, na hawakujitokeza kuwanusuru licha ya kuwa na uwezo wa kufanya hivyo.

Soma zaidi...

Serikali Yalazimisha Watu Kusherehekea Uhuru Unaodaiwa Sambamba na Mauaji ya Kikatili ya Halaiki!

Je, watu wa Jordan wanasherehekea uhuru unaodaiwa wakati jana, daktari Muislamu mwenye msimamo thabiti huko Gaza alipoteza watoto wake tisa wote kwa wakati mmoja, kutokana na kombora lililorushwa na ndege ya jeshi la mauaji ya halaiki nyumbani kwao, katika mandhari ya kinyama isiyo na kifani katika historia ya mwanadamu?

Soma zaidi...

Enyi Madhalimu! Fungueni Macho yenu!

Mnamo 19 Mei 2025, kesi ya wanachama 33 wa Hizb ut Tahrir, iliyodumu kwa karibu miezi minane, ilifikia kikomo. Kwa mujibu wa uamuzi wa mahakama, Musayev Shukrullah alihukumiwa kifungo cha miaka 17 katika jela maalum ya utawala; Selimov Dilshod alihukumiwa miaka 16 katika gereza maalum la utawala; Watu 20 walihukumiwa kifungo cha miaka 12 katika gereza maalum la utawala; Watu 8 walihukumiwa kifungo cha kati ya miaka 8 na 10, 4 kati yao katika hali maalum na wengine 4 katika hali kali; na watatu waliosalia walihukumiwa kati ya miaka 4 na 5 chini ya kifungo cha nyumbani.

Soma zaidi...

Serikali ya Muda Inatengwa na Wananchi kwa sababu ya Utiifu wao kwa Amerika; kwa upande mwingine, Msimamo wa Jeshi letu katika Kupendelea Ubwana wa Nchi kwenye Masuala ya 'Mkondo' na 'Bandari' ni Dhihirisho la Matarajio ya Watu

Huku serikali ya mpito, ikiwapuuza Waislamu wa Rohingya na ubwana wa nchi hiyo, inatamani sana kupeana 'mkondo' kwa maslahi ya kisiasa ya kijiografia ya Amerika na kukabidhi shughuli za 'New Mooring Container Terminal' kwa kampuni yenye ushawishi wa Marekani "DP World", msimamo mkali wa jeshi letu kuunga mkono ubwana wa nchi umesifiwa na watu wengi.

Soma zaidi...

Wananchi Wanataka Kupinduliwa kwa Serikali na Kusimamishwa kwa Utawala wa Kiislamu

Aden, mji mkuu wa muda wa serikali ya Yemen, umeshuhudia maandamano matatu ya wanawake na wanaume katika wiki mbili zilizopita. Kutokana na mateso yanayoendelea kwa wananchi, maandamano ya hasira yamefanyika mjini Aden, wakidai huduma za msingi na kukemea hali ngumu ya maisha na huduma duni. Maandamano haya yalijumuisha kauli mbiu dhidi ya muungano wa Waarabu, serikali ya Yemeni, na Baraza la Mpito, ambalo linadhibiti mji mkuu wa muda, Aden. Maandamano haya pia yalishuhudia milio ya risasi na kukamatwa kwa baadhi ya waandamanaji. Maandamano haya yalifanywa na wanawake na wanaume kwa siku tofauti. Kilichotia fora ni kuregea kauli mbiu isemayo “Wananchi wanataka kupinduliwa kwa serikali,” ambayo inatukumbusha Mapinduzi ya Kiarabu dhidi ya ukandamizaji na udhalimu.

Soma zaidi...

Maandamano ya Kulaani yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir, Wilayah Bangladesh: “Palestina, Kashmir, Arakan – Khilafah pekee ndiyo Suluhisho”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, leo (23/05/2025) baada ya swala ya Ijumua, iliandaa maandamano ya kulaani katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong dhidi ya wimbi jipya la mashambulizi ya umbile lililolaaniwa la Kiyahudi kuchukua udhibiti wa Ukanda wote wa Gaza.

Soma zaidi...

Nia na Malengo ya Ziara ya Afisa wa Uingereza nchini Uzbekistan

Mnamo Mei 13, 2025, Lord Cocker, Waziri wa Ulinzi wa Uingereza, alifanya ziara rasmi nchini Uzbekistan. Ziara hii ni muhimu kwani ni ziara ya kwanza rasmi nchini Uzbekistan kwa mwakilishi wa serikali mpya ya Uingereza. Wakati wa ziara yake, alikutana na uongozi wa jeshi la Uzbekistan, akiwemo Naibu Waziri wa Ulinzi Kanali Jenerali Hamdam Qarshiyev na Kamanda wa Walinzi wa Kitaifa Luteni Jenerali Rustam Juraev. Mikutano hii ilithibitisha kujitolea kwa Uingereza katika kuimarisha ushirikiano wa ulinzi wa nchi mbili na Uzbekistan. Lord Cocker pia alitoa hotuba katika Chuo cha Jeshi la Uzbekistan, mara ya kwanza kwa Waziri wa Ulinzi wa Uingereza kuzungumza katika chuo hicho.

Soma zaidi...

Bunge la Ulaya na Maazimio ya Ukoloni Mambo Leo

Wiki iliyopita Bunge la Jumuiya ya Ulaya (EU) lilitoa mwito kwa Tanzania kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kutatua kesi waliyosema ina msukumo wa kisiasa ya kiongozi wa chama cha upinzani, kutoa uhuru zaidi wa kisiasa kupitia majadiliano, kufanya mabadiliko ya sheria za uchaguzi,kuheshimu haki ya vyama kushiriki katika uchaguzi huru nk.

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina ilimuua Rami Zahran, Kisha Mzee Mmoja, Ikikamilisha Uhalifu wake Dhidi ya Watu wa Palestina

Mnamo siku ya Jumanne,13/5/2025, vikosi vya usalama vya Mamlaka ya Palestina vilimuua kijana Rami Zahran kutoka kambi ya wakimbizi ya Al-Far'a huko Tubas. Kisha wakafuatilisha hili kwa kumuua mzee mmoja (Abu Khalil al-Saba'neh) kutoka mji wa Jenin. Huu ni mwendelezo wa jinai zake dhidi ya watu wa Palestina, zikiwemo za mauaji, uchomaji moto, ukamataji, uvamizi wa misikiti, na unyang'anyaji mali ya Wapalestina kinyume cha sheria, kula mali zao kwa njia ya dhambi na fujo.

Soma zaidi...

Mwisho wa Enzi ya Awami League, Chama Kinara cha Siasa za Kisekula - ni Onyo la Kihistoria kwa Vyama Vilivyopo vya Kisiasa na Nyuso Mpya za Kisiasa

Kwa kuanguka kwa dhalimu Hasina na tangazo rasmi la kupigwa marufuku kwa shughuli zote za chama kiovu cha Awami League, enzi ya giza ya siasa za chama kikuu cha kisekula -Awami League imekamilika. Kuangamia huku kwa Awami League, mrithi wa 'All India Muslim League' iliyoanzishwa mwaka wa 1906, hakutokani na mlingano wa kisiasa wa mamlaka ya kundi lolote la kisiasa, bali ni ukweli wa kihistoria na usioepukika. Hamu ya Waislamu wa India ni kuishi chini ya utawala wa Kiislamu-Khilafah.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu