Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 549
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Siku za hivi karibuni zimeshuhudia maendeleo ya ajabu katika vita. Droni zilishambulia Port Sudan, mji mkuu wa utawala, kwa siku sita mfululizo, na kushambulia uwanja wa ndege wa kiraia, kambi ya anga, na maghala ya mafuta, na kusababisha mgogoro wa mafuta kote nchini. Droni pia zilishambulia mji wa Kassala kwenye mpaka wa Eritrea upande wa mashariki, pamoja na miji mingine. Haya yote yalisababisha vikosi vya jeshi kuondoka kuelekea upande wa El Fasher na kuzingatia kulinda Sudan mashariki, kama BBC ilivyoripoti mnamo tarehe 10/5/2025. Je, hii ina maana kwamba shambulizi la mashariki mwa Sudan linalenga kuliondoa jeshi kutoka Darfur, na kuiacha ikiwa chini ya udhibiti wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) pekee? Je, matukio haya ni utangulizi wa Jukwaa la Jeddah (kongamano la mazungumzo)? Au kuna malengo mengine?
Trump alianza ziara yake nchini Saudi Arabia mnamo Mei 13, 2025, ikifuatiwa na Qatar mnamo Mei 14, 2025, akihitimisha safari yake nchini Imarati mnamo Mei 15, 2025, na kuhitimisha ziara yake mnamo Mei 16, 2025. Kisha aliandamanisha ziara hii kwa udanganyifu wake kwamba hatazuru umbile la Kiyahudi, kuwakejeli wajinga wanaodai kuwa uungaji mkono wa Trump kwa umbile la Kiyahudi umetikiswa! Hii ni licha ya ukweli kwamba umbile la Kiyahudi lilipanua mashambulizi yake kwenye Ukanda wa Gaza baada ya Trump kuondoka katika nchi hizo tatu.
Trump alitangaza kwa mshangao jana, Jumamosi, katika chapisho kwenye jukwaa lake la Ukweli wa Kijamii (Truth Social platform), kwamba "Baada ya usiku mrefu wa mazungumzo yaliyopatanishwa na Marekani, ninafurahi kutangaza kwamba India na Pakistan zimekubali kusitishwa kwa mapigano kamili na mara moja, "na kuzisifu nchi zote mbili kwa kutumia busara na akili kubwa." (Al Jazeera, 11/5/2025) ... ni upi ukweli katika uhasama na mzozo huu? Je, Mkataba wa Maji wa Indus ni nini haswa ambao India imeusitisha kwa muda? Je, Marekani inahusika katika kuanzisha shambulizi hilo na pia kulisitisha?
Kisimamo cha Nusra Mbele ya Bunge la Lebanon kwa ajili ya Waislamu waliowekwa Kizuizini kilicho andaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon.
Vyanzo vya kimatibabu vimeandika kuuawa shahidi kwa Wapalestina wasiopungua 42 kutokana na ulipuaji mabomu wa umbile la Kiyahudi katika Ukanda wa Gaza tangu alfajiri ya Jumatatu, 12 Mei 2025. Uvamizi huo ulianza tena jioni baada ya kusimama kwa saa kadhaa, ambapo mwanajeshi mmoja aliyekamatwa wa umbile la Kiyahudi aliachiliwa huru.
Mabadilishano ya makombora kati ya Pakistan na India yanaendelea katika njia nyingi za kusitisha mapigano huko Kashmir baada ya India kushambulia kwa mabomu maeneo tisa ndani ya Pakistan usiku wa Mei 6, ambayo ilisema ni "miundombinu ya kigaidi iliyohusika na shambulizi la silaha huko Kashmir" mwezi uliopita. Suluhisho la kivitendo la kusonga mbele haliwezi kuwa mzozo mdogo, lakini lazima liwe ukombozi wa kina wa maeneo yanayokaliwa kimabavu.