Jumamosi, 30 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Jeshi la Bangladesh Lazima Likatae Kuwa Rafiki wa Wakoloni kwa Jina la kile kinachoitwa Ulinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa na Kurudisha Hatima Yake kama Walinzi wa Ummah

Jeshi la Bangladesh linathibitisha shambulizi baya la droni kwenye kambi ya Umoja wa Mataifa katika eneo la Abyei nchini Sudan mnamo 13 Disemba 2025. Shambulizi hili liliwaua walinda amani sita wa Bangladesh na kuwajeruhi wengine wanane. Wakati huu wa kuhuzunisha moyo hauhitaji maombolezo tu, bali pia tathmini mpya muhimu ya misheni ambayo kwayo walitoa maisha yao.

Soma zaidi...

Mauaji ya Pilkhana Yalikuwa Njama ya India ya Kudhoofisha Jeshi la Nchi hii - Ripoti Hii ya Tume Huru ya Uchunguzi ya Kitaifa Imethibitisha Ukweli ambao Hizb ut Tahrir Iliuwasilisha kwa Taifa kwa Ujasiri Miaka Kumi na Sita Iliyopita. Tunatoa Wito Ten

Tume Huru ya Kitaifa ya Uchunguzi iliyoundwa na serikali ya mpito kuhusu mauaji ya Pilkhana, na kusababisha vifo vya maafisa 57 wenye sifa nzuri, yaliyotokea katika Makao Makuu ya BDR mnamo Februari 25 na 26, 2009, imetoa ripoti yake ya uchunguzi. Uchunguzi umethibitisha kuhusika kwa Hasina na washirika wake Tapas na wengineo katika kutekeleza njama ya India ya kudhoofisha jeshi la nchi hii. Tunataka sana adhabu ya haraka kwa wahalifu hawa waliohusika katika tukio hilo na kutangazwa kwa India kama dola adui. Lazima mukumbuke kwamba chama cha kisiasa chenye busara na ikhlasi, Hizb ut Tahrir, kilikuwa cha kwanza kuleta ukweli huu kwa ujasiri kwa taifa

Soma zaidi...

Hukumu ya Kifo kwa Hasina: Udhalimu wa Kisekula Uliomuunda Hasina Ungalipo

Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imetoa hukumu ya kifo ya kihistoria dhidi ya mtawala wa Bangladesh aliyeondolewa madarakani Sheikh Hasina. Kwa watu waliokandamizwa wa Bangladesh, uamuzi huu unatoa uthibitisho wa kiishara uliochelewa kwa muda mrefu na unasimama kama shtaka lenye nguvu kwa utawala uliokanyaga ubinadamu wa kimsingi. Lakini uamuzi huu unahitaji tafakari ya kina, sio sherehe tu. Haki ya kweli inahitaji mabadiliko ya kimfumo, sio adhabu ya mtawala dhalimu tu. Chanzo kikuu ni mfumo wa kimataifa unaoongozwa na Marekani, ambao unahubiri demokrasia huku ukitekeleza ‘mantiki ya siasa za kijiografia’.

Soma zaidi...

‘Mkataba wa Mageuzi ya Julai: Udanganyifu Mkubwa’: Hizb ut Tahrir Yalaani Mkataba huo, na Kuhimiza Badali Msingi ya Kisiasa kwa Demokrasia Iliyofeli

Katika kujibu hotuba ya hivi karibuni ya Mshauri Mkuu Profesa Yunus kuhusu utekelezaji wa Mkataba wa Kitaifa wa Julai na kura ya maoni kuhusu mapendekezo ya mageuzi ya katiba katika Mkataba huo, Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh inatoa onyo kali kwamba mapendekezo ya mageuzi na mchakato wake wa utekelezaji si kitu zaidi ya hatua ya juu juu ambayo inashindwa kushughulikia sababu za msingi za mgogoro wa kisiasa wa Bangladesh. Inatoa udanganyifu wa mabadiliko ili kuhifadhi dhati ya mfumo wa kidemokrasia uliofeli.

Soma zaidi...

Watu Wapendao Uislamu wa Nchi Wameukataa Mkataba wa Julai, ambao umejengwa juu ya Msingi wa Usekula na Demokrasia Batili ya Magharibi, Na Wanataka Mkataba wa Madina uliojengwa juu ya Msingi wa Imani yao Safi ya Kiislamu

Mnamo 17 Oktoba 2025, kipote cha wanasiasa wenye uchu wa madaraka nchini humu walitia saini ‘Mkataba wa Julai - suluhisho la kisiasa lililoandikwa kwa kuzingatia imani potofu za kidemokrasia ya kisekula na mfumo wa Wakoloni makafiri wa Magharibi hasa Marekani-Uingereza, na kuweka mfano mwengine wa kuchukiza wa usaliti kwa Uislamu na Waislamu, na utiifu kwa nchi za Magharibi. Mfumo huu wa kisekula wa kibepari uliotungwa na wanadamu umefeli katika nchi zote duniani. Jambo hili ni la kweli mithili ya mwangaza wa mchana kwamba, mfumo huu wa ukandamizaji unalinda maslahi ya tabaka tawala, mabepari wachache na wakoloni wa Magharibi, na kuwanyonya watu wengi zaidi. Mnashuhudia kwamba kizazi cha vijana (Gen-Z) katika nchi nyingi wanaasi tabaka tawala la kibepari moja baada ya jengine na kuwaangusha watawala.

Soma zaidi...

Suluhisho la Dola Mbili ni Kejeli ya Karne isiyo na Aibu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh inashutumu vikali kile Prof. Yunus alisema kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa, “Ni kwa msingi wa mipaka ya kabla ya 1967 tu, na Israel na Palestina wakiishi bega kwa bega kwa amani, haki inaweza kutendeka”. Wakati watu wa Palestina wanaangamizwa mbele ya macho yetu na Mayahudi kunyakua 78% ya Palestina kinyume cha sheria, ni vipi haki inaweza kutendeka kwa kuruhusu ‘Israel’ kuishi bega kwa bega na Palestina! Kwa nini tunaita makundi machache ndani ya umbile haramu la Kiyahudi kuwa ni dola (Palestina), lakini haina hata jeshi lake?

Soma zaidi...

Sehemu za dhati za nchi Lazima Ziungane dhidi ya Sera ya Serikali ya Mpito ya Utiifu kwa Marekani Mkoloni Kafiri

Serikali ya mpito inaisaliti nchi kwa kuonyesha kusitasita kulinda Mipaka yetu kutoka kwa ‘Jeshi la Arakan’ linaloungwa mkono na Marekani, huku ikitamani kuwatumia wanajeshi wetu kwa Misheni ya Amerika nchini Ukraine. Kuanzia Disemba 2024 hadi Septemba 10, kundi la waasi lenye makao yake nchini Myanmar liliwateka nyara wavuvi 325 kutoka maeneo mengi kando ya Mto Naf na Ghuba ya Bengal. (bdnews24.com, Septemba 12, 2025). Kinaya ni kwamba, serikali ya Yunus ilipuuza Jeshi la Arakan (wakala wa Marekani) linalofanya kazi ndani ya ardhi yetu na kutishia watu wetu na ubwana wetu. Wakati huo huo, ilikuwa haraka kuisaidia Ukraine ili kumfurahisha bwana wake wa ubeberu mamboleo, Marekani.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh Yawaalika Watu Wote Watambuzi, wakiwemo Wanasiasa, Wasomi, Waandishi wa Habari na Kizazi cha Vijana cha Nchi Kutazama Kongamano lake la Kisiasa Mtandaoni lenye Kichwa “Bangladesh 2.0: Utegemezi au Ukombozi?”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, imeandaa kongamano la kisiasa la mtandaoni lenye kichwa “Bangladesh 2.0: Utegemezi au Ukombozi?” kutoa mwongozo kwa wananchi ili kufikia lengo kuu la Mapinduzi ya Julai 24. Munaalikwa kutazama kongamano hili ili kupata mwamko wa kisiasa na kuamua nini cha kufanya katika hatua hii ya kisiasa nchini.

Soma zaidi...

Marekani ya Kibeberu Inatumia Wakala Wake Shirika la Excelerate Energy kutia Udhibiti juu ya Bandari na Bahari zetu za Kimkakati ili Kuendeleza Udhibiti wake wa Kisiasa

Balozi wa zamani wa Marekani nchini Bangladesh Peter D Haas alifanya mkutano wa karibu saa moja na Waziri wa Mambo ya Nje Asad Alam Siam mnamo Alhamisi (4 Septemba). Ingawa hakuna upande uliofichua maelezo ya majadiliano hayo, vyanzo vya habari viliripoti kuwa mazungumzo hayo yalihusu uwezekano wa kuagiza LNG kutoka Marekani, pamoja na ushirikiano wa sasa na miradi ya mustakabali. Kwa sasa Haas anatumika kama Mshauri wa Kimkakati wa Excelerate Energy - shirika la kimataifa la Texas ambalo linaendesha kituo cha LNG kinachoelea huko Maheshkhali, Cox’s bazar.

Soma zaidi...

Ufuatiliaji Mkubwa wa Mkoloni Amerika juu ya kile kinachoitwa “Mageuzi” sio Chengine ila ni Jaribio la kupanua Udhibiti wake nchini Bangladesh

Balozi Mdogo wa Marekani jijini Dhaka, Tracy Ann Jacobson, alifanya mkutano na Profesa Ali Riaz, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Kitaifa ya Maridhiano wiki iliyopita ili kuuliza kuhusu mipango ya mageuzi inayoendelea na maendeleo yake. Jacobson na manaibu wake wamekuwa wakifanya mfululizo wa mikutano na wawakilishi wa vyama vikuu vya kisiasa. Kama sehemu ya ushirikiano wa Marekani ‘kukuza demokrasia’ nchini Bangladesh, tunaona mikutano na taarifa za mara kwa mara kutoka kwa Ubalozi wa Marekani nchini Bangladesh na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani zinazohimiza marekebisho katika utawala. Kusiwe na shaka kwamba msukumo wa Marekani wa kuleta mageuzi na kile kinachoitwa ‘uwajibikaji wa kidemokrasia’ haukusudiwi kheri ya watu wetu. Katika historia, mbeberu mamboleo Marekani imekuwa ikiunga mkono madikteta kwa maslahi yake huku ikitetea ‘demokrasia’ na ‘haki za binadamu’.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu