Alhamisi, 11 Dhu al-Hijjah 1447 | 2026/05/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Pongezi kutoka kwa Amiri wa Hizb ut Tahrir, Mwanachuoni Mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, kwa Waislamu kwa Jumla na Mashababu (Wanachama wa Hizb) Hasa kwa Mnasaba wa Sikukuu ya Idd al-Adha 1447 H Sawia na 2026 M

Wapendwa ndugu na dada: Idd hii inakuja huku uvamizi wa Mayahudi, unaoungwa mkono na Amerika na silaha zake, ukiendelea dhidi ya Gaza (Hashim) na Palestina yote. Watawala katika nchi za Kiislamu wanaangalia kinachoendelea, wakiwahesabu mashahidi (shuhadaa) na kuwaita wafu! Na bora zaidi kati yao ni wale wanaopatanisha kana kwamba hawaegemei upande wowote, lakini wako karibu zaidi na Mayahudi!

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Mazungumzo ya Usaliti Kati ya Lebanon na Umbile la Kiyahudi

Jijini Washington, mazungumzo yalifanyika kati ya mabalozi wa Lebanon na umbile la Kiyahudi. Hii ilionekana kama mazungumzo ya kiwango cha juu cha amani, pamoja na makubaliano ya kusitisha mapigano ya siku kumi ambayo baadaye yaliongezwa hadi miezi mitatu mnamo Aprili 24, 2026. Hata hivyo, umbile la Kiyahudi linaendelea kuzidisha uchokozi wake, “jeshi la uvamizi lilitangaza kwamba lilifanya mfululizo wa mashambulizi usiku kucha likilenga zaidi ya maeneo hamsini kusini mwa Lebanon...” (Al-Jumhur, Mei 2, 2026). Je, nia, kama Trump alivyosema, ni amani kupitia nguvu? Basi watawala wa Lebanon wanawezaje kukubali mazungumzo haya ya usaliti ambayo waziwazi, na si kwa siri, yanamaanisha kupanda treni ya uhalalishaji mahusiano?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Ushirika Mkuu wa Ushirikiano wa Ulinzi (MDCP) kati ya Marekani na Indonesia

Mnamo 13 Aprili 2026, Waziri wa Ulinzi wa Marekani na Waziri wa Ulinzi wa Indonesia walitangaza kuanzishwa kwa Ushirika Mkuu wa Ushirikiano wa Ulinzi (MDCP) kati ya Marekani na Indonesia. Kabla ya hili, hati ya siri kutoka Idara ya Ulinzi ya Marekani ilivuja kuhusu idhini ya safari za anga za juu za ndege za Marekani kupitia anga ya Indonesia. Je, maudhui ya makubaliano haya ni yapi na athari zake ni zipi? Athari zake ni zipi kwa uhusiano wa Indonesia na Amerika? Na athari zake ni zipi kwa uhusiano wa Indonesia na China?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Vita dhidi ya Iran

Je, ni nini maana ya kauli za Trump zenye kusitasita—kutoa Iran masaa 48, kisha siku 5, kisha siku 10—na pendekezo lake la mpango wenye nukta 15? Namna gani ujanja wa kauli, nyingi kutoka kwa Trump na chache kutoka kwa Iran, na tangazo la televisheni ya Iran kukataa pendekezo la Trump? Matokeo ya hayo yote ni nini?

Soma zaidi...

Nusra (Msaada) Inatafutwa Kutoka Kwa Nani?!

Kutafuta Nusra (kuomba msaada) kunapaswa kufanywa kwa yule anayekubali Uislamu na kuuingia, na ambaye ni miongoni mwa watu wa nguvu na ulinzi, ili aweze kuinusuru dini na kusimamisha utawala kwa yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu. Masharti haya mawili lazima yatimie kwa mnayeitafuta Nusra kwake. Ikiwa hatakubali Uislamu na kuuingia, au si katika watu wa nguvu na ulinzi wenye uwezo wa kuleta mabadiliko, peke yake au pamoja na wengine, basi hatakuwa miongoni mwa watu wa Nusra

Soma zaidi...

Pongezi kutoka kwa Amiri wa Hizb ut Tahrir, Mwanachuoni Mkubwa, Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, kwa Wanaozuru Kurasa zake kwa Mnasaba wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan wa Mwaka 1447 H sawia na 2026 M

Enyi Waislamu, nawakumbusha haya yote katika siku hizi ambapo uvamizi wa kikatili wa Mayahudi dhidi ya Ukingo wa Magharibi pamoja na Gaza unaendelea, kisha uvamizi wa Mayahudi ukaenea hadi Lebanon na Syria… ambapo waliranda wakiwa huru katika nchi za Kiislamu bila kukutana na upinzani wowote wa kweli. Badala ya watawala kuhamasisha majeshi ya Waislamu kupigana na umbile la Kiyahudi, kuwafukuza wale walio nyuma yake na kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa... badala yake, tunawaona watawala hawa wakisaini makubaliano baada ya makubaliano nalo, na hata mtawala dhalimu Trump anawakusanya pamoja ili kuwadhalilisha, bila aibu yoyote mbele ya Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, au waumini!

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Habari za Zama za Mwisho na Kushuka kwa Masihi (AS)

Ni lazima ieleweke kwamba taarifa zilizomo katika maandiko ya Kiislamu, iwe kuhusu matukio ya zamani au yajayo, lazima zithibitishwe ili zikubaliwe; yaani, hazipaswi kuwa dhaifu au za kubuniwa. Nitataja baadhi ya dalili sahihi zinazohusiana na swali lako, lakini sitataja zote; Unaweza kupata zaidi katika vitabu vinavyohusika vya fiqh ya Kiislamu.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Matukio nchini Syria na Kurudi Nyuma kwa Vikosi vya Kidemokrasia vya Syria

Matukio yanatokea kwa kasi kubwa kaskazini mashariki mwa Syria, na Vikosi vya Kidemokrasia vya Syria (SDF) vinapoteza udhibiti wa maeneo hayo kwa kasi kubwa, huku serikali ya Syria ikiyachukua. Yote haya yalitokeaje? Hili linapaswa kuelewekaje ikizingatiwa kwamba serikali na SDF ni vibaraka wa Amerika? Na licha ya idhini ya Marekani kwa serikali ya Syria kuwa wazi kama mwanga wa mchana katika kuteka maeneo hayo, utawala wa Trump unapanga nini nchini Syria au viunga vyake?

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu