Utawala wa Jordan Unalilinda Umbile Adui la Kiyahudi kwa Kuyapangua Makombora na Droni Zinazoelekezwa kwake
- Imepeperushwa katika Jordan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo siku ya Ijumaa, tarehe 13/6/2025, alfajiri, umbile la Kiyahudi lilianzisha mashambulizi dhidi ya Iran, yakilenga vituo vyake vya nyuklia, viwanda vyake vya makombora ya balestiki, na viongozi wa kijeshi, na kusababisha uharibifu mkubwa kwa maisha na mitambo ya kijeshi na ya kiraia, kwa msaada na ushirikiano wa Marekani. Iran, kama kawaida, iliapa kutoa jibu kali na baya kwa umbile la Kiyahudi kupitia mashambulizi ya droni na makombora. Ilitekeleza mawimbi ya mashambulizi haya asubuhi na jioni ya siku hiyo hiyo, yakivuka anga ya Iraq, Syria, na Jordan. Baadhi ya mashambulizi haya yalisababisha uharibifu kwa baadhi ya vifaa katika miji ya umbile hilo, kabla ya baadhi yake kupanguliwa katika anga ya jirani kabla na baada ya kufika kwenye umbile la Kiyahudi.