Jumatano, 29 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/25
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Na Mwenyezi Mungu si mwenye Kughafilika na Wanayoyafanya Madhalimu

Tunaona kwamba vyombo vya usalama vya dola nchini Kyrgyzstan vinawakamata wahalifu ambao wamefanya uhalifu mbalimbali, na baadhi yao walishtakiwa kuwa katika genge la wahalifu, huku wengine wakishtakiwa kwa hongo, mauaji, na mashtaka mfano wa hayo. Ikiwa kweli wanahusika katika uhalifu huo, basi wanachukuliwa pia kuwa wahalifu kwa mujibu wa Shariah ya Kiislamu. Lakini wakati huo huo, tunashuhudia kwamba kuna wafungwa ambao hawakufanya kitendo chochote cha jinai, bali walikamatwa kwa sababu tu ya kulingania dini ya Mwenyezi Mungu na kwa kusema: “Mola wetu ni Mwenyezi Mungu”! Na pia wanakamatwa kikatili mithili ya wahalifu wa kweli na kutupwa magerezani ambako hupigwa sana na mbinu nyingine za "kisasa" za mateso. Hawa ni wanachama wa Hizb ut Tahrir, na madhalimu ni maafisa wa serikali na vyombo vyao vya usalama.

Soma zaidi...

Tukio la Jalalabad: Kuilinda Dawah ni Wajibu kwa Kila Mmoja Wetu

Mnamo tarehe 26 Novemba, Mashababu wa Hizb ut Tahrir waliandaa amali dhidi ya rasimu ya sheria ya “Uhuru wa Dini na Mashirika ya Kidini” katika eneo la Jalalabad. Wiki tatu baadaye, kati ya Disemba 10 na 14, Kamati ya Serikali ya Usalama wa Kitaifa ilifanya msako katika nyumba 21 katika eneo hilo na kuwaweka kizuizini kinyume cha sheria wanachama wa Hizb ut Tahrir. Vikosi vya usalama havikuruhusu wanachama waliozuiliwa (Mashababu) kukutana na mawakili wao na badala yake walifanya uchunguzi mbele ya mawakili waliofunzwa mahususi kwa kesi hii. Kutokana na hali hiyo, Mashababu wetu walizuiliwa kwa muda kwa kipindi cha mwezi mmoja kwa kisingizio cha kusambaza vipeperushi misikitini vinavyopinga sheria hiyo. Kesi ya jinai ilifunguliwa dhidi yao chini ya shtaka la “kuandaa na kuendesha shughuli za itikadi kali.”

Soma zaidi...

Serikali Kuchimba Migodi katika Eneo linaloishi Viumbe Hai (Biosphere) ni Dhulma kwa Umma!

Rais Sadyr Japarov alifanyia marekebisho sheria kuhusu “maliasili zilizo chini ya ardhi” na “maeneo yanayoishi viumbe hai (biosphere)” ambapo utafiti wa kijiolojia na utafiti katika maeneo ya yanayoishi viumbe hai (biosphere), uchunguzi wa kijiolojia wa rasilimali za dunia, uchimbaji wa akiba muhimu na kazi ya uchunguzi wa kijiolojia kwa rasilimali za chini ya ardhi zitafanywa kwa msingi wa uamuzi wa serikali.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu