Jumamosi, 04 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/05/31
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ugonjwa wa Kipindupindu Waangamiza Sudan, na Serikali, kwa Uzembe wake, Inaomba Msaada kwa Mashirika ya Kimataifa!

Shirika la Afya Duniani (WHO) limefichua kuwa takriban wagonjwa 60,000 wa kipindupindu wamerekodiwa nchini Sudan, na kusababisha vifo vya zaidi ya 1640, likionya madhara ya kuporomoka kwa mfumo wa afya nchini humu. Ufichuzi huu unakuja wakati kipindupindu kikienea kwa kasi katika Jimbo la Khartoum, ambapo maambukizi mapya yanazidi 90% ya jumla ya nchi, haswa huko Karari, Omdurman, na Ombada. Mnamo Jumanne, 27/5/2025, Wizara ya Afya ya Sudan ilitangaza kurekodi kesi 2729, pamoja na vifo 172, katika wiki moja. Waziri wa Afya wa Sudan Dkt. Haitham Mohamed Ibrahim alisema kuwa kuenea kwa kipindupindu jijini Khartoum kunatokana na kuzorota kwa hali ya mazingira na matatizo ya vyanzo vya maji ya kunywa. Wakati huo huo, Waziri Mkuu mpya Kamil Idriss anatoa wito kwa WHO, huku ripoti za vyombo vya habari zikisema kuwa anawasiliana na Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom ili kujadili kusaidia juhudi za kudhibiti kipindupindu nchini humu.

Soma zaidi...

Ulimwenguni wa Kusini na Mfumo Mpya wa Ulimwengu – Tumaini au Sarabi?

Mnamo Aprili 2025, wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa BRICS nchini Brazil, Waziri wa Mambo ya Nje wa Malaysia Datuk Seri Mohamad Hasan alitoa ujumbe ulio wazi: ulimwengu hauwezi tena kutegemea utawala wa dola moja ili kuhakikisha utulivu wa kimataifa. Alihimiza mataifa ya Kusini mwa Ulimwengu – inayojumuisha nchi zinazoendelea kote Asia, Afrika, Amerika ya Kusini, na Oceania – kuinuka kwa pamoja na kuongoza uundaji wa mfumo mpya wa kilimwengu. Matamshi yake yanaangazia sauti za vibwagizo vinazokua zisizoridhika na utawala wa muda mrefu na kuanguka kwa uaminifu wa utawala wa kimataifa unaoongozwa na Marekani.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir/ Wilayah Pakistan: Gaza inahitaji kuingia kwa majeshi ya Waislamu, sio tu misaada ya kibinadamu!

Taarifa ya mwisho ya Mkutano wa Waarabu, ulioandaliwa na mji mkuu wa Iraq, Baghdad mnamo tarehe 17 Mei 2025, ilisisitiza haja ya kuleta misaada ya kibinadamu mjini Gaza. Watawala wa Waislamu, Waarabu na wasiokuwa Waarabu, wamezuia majeshi ya Waislamu kupigana na Mayahudi, kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu. Mtume ﷺ ametuambia kuwa kupigana na Mayahudi na kuwashinda kunaleta malipo makubwa.

Soma zaidi...

Kudumu kwa Mashirika ya Kifeministi na Mashoga hadi kufikia Hatua ya Kueneza Uchafu miongoni mwa Waumini ni Shambulizi la Dhahiri kwa Heshima ya Waislamu

Baada ya wasagaji wawili wanachama wa chama chenye uhusiano na Chuo Kikuu cha Marekani cha Beirut (AUBMC), chini ya kivuli na jina "Programu Oanishi ya Afya ya Jimai ya Wanawake (WISH) katika AUBMC," kutembelea shule ya upili ya wasichana jijini Tripoli, kwa uratibu wa Wizara ya Elimu; kisha kwa mbwembwe na bila aibu kuendekeza mambo machafu na kuonyesha picha na maudhui machafu kwa wanafunzi, wazazi wakasukumwa kuripoti tukio hilo kwa uongozi wa shule, ambao nao ulieleza kuwa wawili hao walikuja shuleni kwa amri ya Wizara ya Elimu na Elimu ya Juu!

Soma zaidi...

Serikali Yalazimisha Watu Kusherehekea Uhuru Unaodaiwa Sambamba na Mauaji ya Kikatili ya Halaiki!

Je, watu wa Jordan wanasherehekea uhuru unaodaiwa wakati jana, daktari Muislamu mwenye msimamo thabiti huko Gaza alipoteza watoto wake tisa wote kwa wakati mmoja, kutokana na kombora lililorushwa na ndege ya jeshi la mauaji ya halaiki nyumbani kwao, katika mandhari ya kinyama isiyo na kifani katika historia ya mwanadamu?

Soma zaidi...

Wananchi Wanataka Kupinduliwa kwa Serikali na Kusimamishwa kwa Utawala wa Kiislamu

Aden, mji mkuu wa muda wa serikali ya Yemen, umeshuhudia maandamano matatu ya wanawake na wanaume katika wiki mbili zilizopita. Kutokana na mateso yanayoendelea kwa wananchi, maandamano ya hasira yamefanyika mjini Aden, wakidai huduma za msingi na kukemea hali ngumu ya maisha na huduma duni. Maandamano haya yalijumuisha kauli mbiu dhidi ya muungano wa Waarabu, serikali ya Yemeni, na Baraza la Mpito, ambalo linadhibiti mji mkuu wa muda, Aden. Maandamano haya pia yalishuhudia milio ya risasi na kukamatwa kwa baadhi ya waandamanaji. Maandamano haya yalifanywa na wanawake na wanaume kwa siku tofauti. Kilichotia fora ni kuregea kauli mbiu isemayo “Wananchi wanataka kupinduliwa kwa serikali,” ambayo inatukumbusha Mapinduzi ya Kiarabu dhidi ya ukandamizaji na udhalimu.

Soma zaidi...

Serikali ya Muda Inatengwa na Wananchi kwa sababu ya Utiifu wao kwa Amerika; kwa upande mwingine, Msimamo wa Jeshi letu katika Kupendelea Ubwana wa Nchi kwenye Masuala ya 'Mkondo' na 'Bandari' ni Dhihirisho la Matarajio ya Watu

Huku serikali ya mpito, ikiwapuuza Waislamu wa Rohingya na ubwana wa nchi hiyo, inatamani sana kupeana 'mkondo' kwa maslahi ya kisiasa ya kijiografia ya Amerika na kukabidhi shughuli za 'New Mooring Container Terminal' kwa kampuni yenye ushawishi wa Marekani "DP World", msimamo mkali wa jeshi letu kuunga mkono ubwana wa nchi umesifiwa na watu wengi.

Soma zaidi...

Maandamano ya Kulaani yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir, Wilayah Bangladesh: “Palestina, Kashmir, Arakan – Khilafah pekee ndiyo Suluhisho”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, leo (23/05/2025) baada ya swala ya Ijumua, iliandaa maandamano ya kulaani katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong dhidi ya wimbi jipya la mashambulizi ya umbile lililolaaniwa la Kiyahudi kuchukua udhibiti wa Ukanda wote wa Gaza.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu