Jinsi Siasa Inavyo Fanana na Zamani … Matukio Yanaendelea Kama Wanavyo Endelea Watazamaji!
- Imepeperushwa katika Kitengo cha Wanawake Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Wanajeshi madhalimu wa umbile la Kiyahudi walimuua msichana kutoka Palestina kwa kummiminia risasi katika kituo cha upekuzi cha al-Za’im, mashariki mwa ardhi iliyo kaliwa Al-Quds (Jerusalem). Shahidi huyo ni mwanafunzi wa shule ya upili aliyekuwa amebeba mkoba wake wa shule wakati wa kuuwawa kwake; aliuwawa kutokana na madai ya kujaribu kutekeleza oparesheni ya kudunga kisu. Majeshi hayo vamizi yalizuia wahudumu wa ambulensi kutomfikia ili kumpa tiba. Aliachwa kuvuja damu hadi kufa.