Jumapili, 26 Rabi' al-awwal 1446 | 2024/09/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir: Kitengo cha Wanawake “Kongamano la Kimataifa la Wanawake: Ukombozi wa Palestina... Changamoto na Bishara Njema”

Mwaka mzima umepita tangu kuanza kwa Kimbunga cha Al-Aqsa na vita vikali vilivyofuata huko Gaza. Tangu tarehe 7 Oktoba mwaka jana, watu wa Gaza wamevumilia mitihani mikubwa, wakiishi katika machungu, mateso, na majanga yasiyohesabika.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Ukombozi: “Enyi Waislamu, Je, Mtawaacha Watu wa Palestina peke yao na Hali Umma una Majeshi yenye Nguvu?”

Baada ya Swala ya Ijumaa, katika mji mkuu, Tunis, yalifanyika matembezi ya hamsini yaliyoitishwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia, kwa watu wa Zaytouna, kwa ajili ya kuwanusuru watu wa Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) na Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa ulio mateka, na kichwa chake kilikuwa, “Enyi Waislamu, je, mtawaacha watu wa Palestina peke yao na hali Umma una majeshi yenye Nguvu?!”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Mkutano na Waandishi wa Habari: “Uchaguzi ni njia ya Kuendeleza Mfumo wa Kisekula ambao ni Wajib Ubadilishwe kwa Kusimamisha Khilafah”

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia ilifanya mkutano na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano huko Ariana katika mji mkuu, Tunis, saa 10:30 asubuhi kwa saa za eneo, wenye kichwa “Uchaguzi ni njia ya Kuendeleza Mfumo wa Kisekula ambao ni Wajib Ubadilishwe kwa Kusimamisha Khilafah”

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Kinachapisha Barua ya Wazi kwa Majeshi ya Waislamu ili Kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina

Takriban watu 40,000 wameuwawa mjini Gaza katika kipindi cha miezi 10 iliyopita, wengi wao wakiwa wanawake na watoto, huku serikali za ulimwengu, zikiwemo nchi za Waislamu zikitazama kama watazamaji pekee wa mauaji haya ya umwagaji damu, bila ya dhamira yoyote ya kisiasa ya kukomesha mauaji hayo. Hakika, tawala nyingi za ardhi za Kiislamu kwa miongo kadhaa zimeimarisha mkono wa uvamizi wa Kiyahudi kupitia mikataba yao ya amani, kuhalalisha mahusiano ya kidiplomasia, na ushirikiano wa kiuchumi na umbile hili la mauaji ya halaiki.

Soma zaidi...

Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir: Kitengo cha Wanawake “Wito kwa majeshi kutoka kwa kina Mama, Mabinti na Dada wa Umma wa Kiislamu kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina)!”

Wanawake wa Kiislamu kutoka sehemu mbalimbali za dunia wameelekeza wito kwa wana wa majeshi ya Kiislamu kutekeleza wajibu wao wa Kiislamu katika kuwalinda Waislamu wa Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) kutokana na uchafu wa umbile la kiyahudi linaokalia kwa mabavu, na kukomboa kila shubiri ya ardhi hii iliyobarikiwa kutoka kwa makucha ya uvamizi huu wa kikatili.

Soma zaidi...

Tunahitaji Sana Khilafah Kuilinda Bahari ya China Kusini

Mgogoro wa Bahari ya China Kusini umeibuka tena kufuatia kuvuja kwa waraka wa kidiplomasia kutoka Jamhuri ya Watu wa China (PRC) kwa Ubalozi wa Malaysia jijini Beijing, wa tarehe 18 Februari. Ujumbe huo ulifichua pingamizi ya China na kuitaka Malaysia kusitisha shughuli za utafiti wa mafuta na gesi huko Beting Raja Jarum na Beting Patinggi Ali, maeneo ya ndani ya Visiwa vya Spratly.

Soma zaidi...

Wakati Msambazaji Mkuu wa Silaha Anapozungumza juu ya Usitishaji Vita na Amani, Hakika ni Dhihirisho la Udanganyifu na Unafiki

Mwishoni mwa mwezi uliopita, Malaysiakini iliripoti mahojiano yake na Balozi wa Marekani nchini Malaysia, Edgard D. Kagan, ambapo alizungumzia, pamoja na mambo mengine, msimamo na sera za Marekani katika Asia Magharibi, haswa kuhusiana na Palestina. Alipoulizwa kuhusu mgongano unaoonekana wa wito wa kusitishwa kwa mapigano na upunguzaji kasi ya ghasia nchini Palestina huku wakati huo huo kukisafirishwa silaha kusaidia ‘Israel,’

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu