Ziara ya Biden ya Dakika za Mwisho Afrika: Kuimarisha Ajenda ya Ukoloni na Unyonyaji wa Marekani
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Jumatano ya tarehe 04/12/2024 Rais wa Marekani Joe Biden alihitimisha ziara yake ya siku tatu nchini Angola. Katika siku ya mwisho ya ziara yake, Biden alitembelea mradi wa Ukanda wa Lobito, mradi wa reli inayojengwa kwa ufadhili wa Marekani yenye kilomita 1,300 inayoanzia Zambia kwenye utajirim kubwa wa madini ya shaba hadi bandari ya Lobito kusini magharibi mwa taifa la Angola. Pia, Biden alifanya mkutano na maraisi wa Angola, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Zambia na Makamu wa Rais wa Tanzania (VOA Africa 05/12/2024).