Ijumaa, 08 Jumada al-thani 1447 | 2025/11/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Risasi Zimechukua Maisha ya Watu … Na Serikali Zinacheza Densi Juu ya Majeraha!

Kwa mujibu wa mashirika ya habari; mtoto wa miezi 8 Laila Al-Ghandour alifariki mnamo Jumanne asubuhi eneo la Mashariki mwa Gaza baada ya kuvuta gesi. Tukio hili linaongeza idadi ya mashuhadaa wa “Msafara wa Mkubwa wa Maregeo” na kufikia idadi ya 61, wakiwemo watoto 7 na majeruhi 2,800, wengi wao wakiwa ni kutokana na risasi na wengine wakiwa ni kutokana na vipande vya mabomu na gesi ya sumu wakati wa uzimaji msafara na majeshi ya umbile la Kiyahudi iliyoanza maeneo tofauti Mashariki mwa ukanda wa Gaza katika kumbukumbu ya miaka 70 ya Nakba, na ambayo ilipinga na kukataa kuhamishwa kwa ubalozi wa Amerika jijini Al-Quds (Jerusalem).

Soma zaidi...

Watoto wa Ardhi Tukufu (Palestina) Wanaendelea Kutolewa Kafara Kutokana na Uhaini na Utiifu wa Biladi (za Waislamu kwa makafiri)!

Katika ripoti iliyo chapishwa na kituo cha habari cha Al-Jazeera idhaa ya Kiingereza, maafisa wa Umoja wa Mataifa (UM) walishutumu kuendelea kukamatwa kiholela kwa watoto katika Ardhi Tukufu (Palestina) na umbile la Kiyahudi, ikisema kuwa “Unyimaji uhuru huu kwa watoto hawa ni wa kitaasisi, kinidhamu, na ulio enea pakubwa”. Msururu wa ripoti za UM zilizo wasilishwa katika lile linaloitwa Baraza la Haki za Kibinadamu zimeonyesha jinsi hali za maisha za watu wa ardhi tukufu ya Palestina na Ukingo wa Magharibi na Gaza zilivyo zidi kudorora kwa zaidi ya mwaka mmoja uliopita, na jinsi watoto wanavyo himili ukatili wa uvamizi wa umbile la Kiyahudi, kwa mujibu wa Kate Gilmore, Naibu Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa UM.

Soma zaidi...

Watoto wa Ghouta, Takwimu za Kimataifa Zazidi Kuongezeka

Tangu Februari 18, majeshi katili ya serikali ya Syria yakisaidiwa na jeshi la anga la Urusi yameendelea na mashambulizi yao makali dhidi ya eneo la Mashariki mwa Ghouta, baada ya kuligawanya kuwa sehemu tatu za kivita. Natija yake, yaliweza kudhibiti zaidi ya asilimia 80 ya eneo hili lililo karibu na mji mkuu wa Damascus, ambalo tangu mwaka wa 2012 limekuwa ngome kubwa zaidi na muhimu zaidi kwa makundi ya upinzani. 

Soma zaidi...

Ni Kipi Kilicho Nyuma ya Oparesheni ya Uturuki "Olive Branch" Kaskazini Mwa Syria?

Imegunduliwa kwamba harakati za Erdogan nchini Syria zimetulia kwa kiasi fulani baada ya oparesheni ya kuhami Furaat na kutelekeza kwa Erdogan mji wa Aleppo, na kuiruhusu serikali kuchukua udhibiti juu ya Aleppo, lakini akaregelea tena oparesheni hiyo kwa jina la ‘Olive Branch’ ikielekea eneo la Afrin tangu Jumamosi, 20/01/2018, kupitia mashambulizi ya anga ya silaha na makombora.

Soma zaidi...

Kwa Kukosekana Khilafah Wanawake Waheshimiwa wa Ash-Sham Wanakabiliwa na Kudhulumiwa Hata na Wale Wanaodai Kuwa Walinzi Wao!!!

Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa linalo shughulikia ufadhili wa watu (UNFPA) limesema kuwa wanawake katika kambi za wakimbizi nchini Syria wamekuwa wakidhulumiwa kimapenzi na wanaume wanaotoa misaada kwa niaba ya UM na mashirika ya kimisaada ya kimataifa. Ripoti hiyo, “Sauti kutoka Syria 2018”, ili eleza kwa kina namna wanawake wakimbizi wa Syria wanavyo lazimishwa kutoa ngono kama badali kwa chakula kutoka UM, na kwamba dhulma hii imeenea maeneo yote kusini mwa Syria.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu