Jumapili, 09 Safar 1447 | 2025/08/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mustakabali wa Vita vya Kisasa na Dori Iliyokosekana ya Khilafah

Vita vinavyoendelea katika sehemu mbalimbali za dunia—hasa vita kati ya Urusi na Ukraine na mzozo kati ya Iran na umbile la Kiyahudi—vinaonyesha wazi kwamba ulimwengu umeingia katika awamu mpya na tofauti ya vita vya kijeshi na kijasusi. Mtazamo wa kale wa vita, uliopitwa na wakati, unaojengwa juu ya vikosi vikubwa vya askari wachanga, vifaru, na mizinga, unabadilika kwa kasi na kuporomoka. Leo, dola kama vile Marekani, China na Urusi zinatenga bajeti kubwa kwa viwanda vya juu vya kijeshi na zinafafanua upya mbinu mpya za kivita. Vita kwenye mstari wa mbele wa kisasa havikomei tena kwa risasi na bunduki – ni vita vya operesheni za kimahesabu (algorithms), akili ya bandia, droni, mtandao na mawimbi ya satelaiti.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Matukio Mjini Al-Suwayda

Axios iliripoti kwamba mkutano wa ngazi ya juu ulifanyika jijini Paris kati ya Waziri wa Mambo ya Kimikakati wa ‘Israel’ Ron Dermer na Waziri wa Mambo ya Nje Asaad Al-Shibani, uliopatanishwa na mjumbe maalum wa Marekani nchini Syria, Thomas Barak, mnamo 25/7/2025. Siku chache zilizopita tangu tarehe 12/7/2025 zimeshuhudia kuongezeka kwa machafuko katika Jimbo la Al-Suwayda [Sweida] kusini mwa Syria, ambalo wengi wa wakaazi wake ni Druze. Umbile la Kiyahudi limetangaza kuingilia kati masuala yao sambamba na kuendeleza uvamizi na mashambulizi yake nchini Syria. Lilishambulia pambizoni mwa kasri la rais, na kuishambulia Wizara ya Ulinzi na Majeshi jijini Damascus.

Soma zaidi...

Heshima yote ni kwa Mwenyezi Mungu

Bunge la Seneti mnamo Alhamisi lilipitisha azimio kwa kauli moja, kulaani tukio la mauaji ya wenza mchana kweupe kwa maagizo ya Jirga kwa jina la kile kinachoitwa “mauaji ya heshima” huko Balochistan. Lilisema mauaji haya ya kinyama hayawezi na hayapaswi kufunikwa na hoja yoyote ya kitamaduni, kikabila, au kimila kwa kisingizio cha kile kinachojulikana kama ghairat au “heshima.” Kwa kweli ni uhalifu ambao umelivunjia heshima taifa. Jaribio lolote la kuhalalisha uhalifu kama huo kwa msingi wa “desturi au heshima” halikubaliki kabisa, kama ilivyo kwa mchakato mzima wa kulaumiwa kwa mwathiriwa.

Soma zaidi...

Mkasa wa Milestone: Watoto Wasio na Hatia na Rubani wetu Jasiri Tauqir, walikuwa Waathiriwa wa Ukatili wa Kukosekana kwa Dola yenye kujali inayowachunga Watu

Jumatatu iliyopita (21 Julai, 2025) alasiri, ndege ya kivita ya Jeshi la Anga la Bangladesh F-7 BGI iligonga jengo katika sehemu ya chini ya Shule ya Milestone na Chuo katika eneo la Uttara katika Mji Mkuu kutokana na hitilafu ya kiufundi. Hii ilisababisha hali ya kusikitisha na ya kuhuzunisha kwa matukio ya kutisha ya watoto walioungua na kukatwa viungo na vijana waliouawa na kujeruhiwa. Sisi katika Hizb ut Tahrir, tunamuomba Mwenyezi Mungu (swt) msamaha kwa marehemu hao, na tunawaombea nafuu ya haraka waliojeruhiwa. Na tunamuomba Mwenyezi Mungu (swt) awajaalie wahasiriwa hadhi ya mashahidi Peponi kwa mujibu wa bishara njema ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw).

Soma zaidi...

Serikali ya “Matumaini” Yageuka Jinamizi kwa Wananchi kwa Kuporomoka kwa Pauni ya Sudan!

Katika hotuba yake baada ya kula kiapo cha kuwa Waziri Mkuu, Kamil Idris alisema: “Kauli mbiu yetu ni matumaini, na dhamira yetu ni kufikia usalama, ustawi, na maisha ya utulivu kwa kila raia wa Sudan!” Katika taarifa yake ya kwanza kwa vyombo vya habari, alitangaza kuwa atatoa muda na juhudi zake kuhakikisha maisha ya heshima kwa kila Msudan.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan inafuraha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio na hamu na masuala ya Umma kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha kisiasa, ambacho kitamwalika Ustadh Muhammad Jami' (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan.

Soma zaidi...

Kuzingirwa kwa Gaza ni Ushahidi wa Khiyana ya Serikali ya Misri

Gaza imeingia katika awamu ya tano njaa (awamu ya janga la njaa), kulingana na ripoti ya Umoja wa Mataifa. Huku Waislamu kila mahali wakijaribu kuwanusuru ndugu zao kwa michango na kuanzisha misafara ya kuvunja mzingiro dhidi yao, nchi jirani zinatazama bila harakati yoyote—mbele yao zaidi ni Misri, ambayo ina mpaka na Gaza, lakini inadai kuwa haina usemi katika suala hilo na imeridhia kuchukua dori ya mpatanishi. Hivyo, je, kweli Misri haina uwezo wa kuwanusuru watu wa Gaza?!

Soma zaidi...

Enyi Wanazuoni wa Al-Azhar: Ikiwa hamtasema neno la haki leo... lini basi?!

Katika wakati ambapo sura za mauaji yanayofanywa na Mayahudi mjini Gaza zikiongezeka, na chakula, dawa, na maji vikizuiliwa kwa watoto, wanawake na wanaume, Al-Azhar ilitoa tamko la kulaani "jinai ya kuweka njaa" inayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi. Taarifa hiyo ilifutwa baadaye! Basi je, inajuzu kilio dhidi ya dhalimu kifutwe?! Na je, sauti ya wanazuoni inaweza kukaa kimya dhidi ya mauaji?! Taarifa hiyo ilikuja ikiwa imejaa misamiati ya kibinadamu, yenye kuwavutia watu wenye dhamiri hai, jumuiya ya kimataifa, na dola zenye ushawishi, na kutoa wito wa kufunguliwa kwa vivuko na utoaji wa misaada. Umbile la Kiyahudi lilielezewa kuwa linafanya uhalifu wa njaa, likituhumiwa kwa mauaji ya halaiki na kuzuia misaada, na ilitoa wito kwa mashirika ya kibinadamu, Umoja wa Mataifa na mashirika ya kimataifa kusonga mbele kufungua vivuko, pamoja na kuwaombea dua watu wa Gaza kwamba Mwenyezi Mungu awanusuru na alipize kisasi kwa ajili yao.

Soma zaidi...

Kuitelekeza Gaza ni Doa katika vipaji vya Nyuso Zenu Enyi Wanajeshi wa Kinana na muhimu zaidi, ni Swali kutoka kwa Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama

Kila siku, mtoto mjini Gaza hufa kwa njaa, au mzee hupumua pumzi yake ya mwisho bila dawa, au mwanamke hufunga macho yake kwa mara ya mwisho kwa maumivu yasiyoweza kuvumilika kutokana na kiu au njaa. Kila saa mbingu hutokwa na machozi, mawe yanapiga kelele, na ardhi inawalaani wale waliowaacha peke yao. Hii ndiyo Gaza... Gaza, ambayo imezingirwa si tu kwa mipaka na vifaru, bali na uzio wa usaliti uliosukwa na viongozi wa majeshi, watawala wa khiyana, na kimya cha Umma wao.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu