Jumatatu, 27 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/23
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Wakenya Amkeni

Kenya, shamba la kikoloni, kwa mara nyingine imo katika mchafuko na mtikisiko kwa kuwa mchezo wa bahati nasibu wa kidemokrasia umezunguka nyuzi 360! Walioko madarakani na walioko barabarani wakiandamana wanalaumiana, huku madai yakielekezwa kwa Mswada wa  Kifedha wa 2024 ulioandaliwa kwa maelekezo ya Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) (Business Daily, 28 Juni 2024)! Mswada huo unapendekeza mikakati ya kuzidisha ukusanyaji wa ushuru ambao unatajwa kuwa ni wenye kukandamiza na kuwadidimiza  raia katika umasikini zaidi!

Soma zaidi...

Kwa Mujibu wa Uislamu, Hairuhusiwi Kugombea, au Kupiga Kura kwenye Chaguzi za Kidemokrasia

Ushiriki wa Muislamu katika Demokrasia ni jambo lenye kuwashughulisha watawala, wanasiasa, wasomi na watungaji sera. Hii ni ima Waislamu wakiwa katika Ulimwengu wa Kiislamu, au wakiishi ughaibuni katika nchi za Magharibi. Hivyo kuna mjadala kuhusu ushiriki wa Muislamu katika Demokrasia nchini Australia, Uingereza na Amerika, kama ulivyo mjadala kuhusu ushiriki wa Waislamu katika uchaguzi nchini Uturuki, Pakistan na Misri.

Soma zaidi...

Hatuwezi Kuishi bila Mfumo wa Sasa wa Ulimwengu

Imani kwamba hatuwezi kuishi bila mfumo wa sasa wa ulimwengu labda ndio kikwazo kikubwa kwa usalama wa watu wa Palestina. Iwe kwa kujua, au kutojua, imani hii inaonekana kushikiliwa na watu kote ulimwenguni huku wakiendelea kujaribu kutumia njia za kidemokrasia kuwasaidia watu wa Palestina, licha ya ukweli kwamba wamewafelisha watu kote ulimwenguni.

Soma zaidi...

Marufuku ya Hijab ya Ubelgiji: Kutopendelea upande wowote kama Haki mpya ya Kimungu (Droit Divin)

Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu (ECHR) imeidhinisha marufuku ya Ubelgiji ya kuvaa hijab shuleni, uamuzi ambao umezusha mijadala kuhusu uhuru wa kidini na usekula barani Ulaya. Mahakama ilipata kwamba marufuku hiyo, iliyokusudiwa kuhakikisha ‘kutopendelea upande wowote’ katika elimu ya umma, haikiuki Mkataba wa Ulaya wa Haki za Kibinadamu. Kesi hiyo ilianzishwa na mwanafunzi mmoja Muislamu ambaye alidai kuwa sera hiyo inakiuka haki zake za uhuru wa dini na elimu. Hata hivyo, ECHR iliamua kwamba marufuku hiyo ilihalalishwa na haja ya kudumisha ‘kutopendelea upande wowote,’ kama ilivyotarajiwa.

Soma zaidi...

Ash-Sham ndio Nyumba ya Khilafah

Tunaweza kusema kwamba kuwasili kwa Khilafah katika Bait ul Maqdis kuna dalili zaidi ya moja. Ya kwanza ni kwamba Bait ul Maqdis ni eneo la kihistoria, kisiasa na kijografia la ulimwengu wa kale. Ni kitovu cha dini zote na kitovu cha umakini wao. Yeyote anayeidhibiti atatawala ulimwengu wa zamani. Hii ina maana kwamba pale Khilafah itakaposimamishwa, basi Waislamu watatawala ulimwengu mzima licha ya Mayahudi na Wakristo kuwa dhidi yao. Pili ni malipo kwa watu wa Ash-Sham kwa yale yaliyowapata na maumivu, kuvunjika, subira na uvumilivu waliyopitia kwa miongo mingi.

Soma zaidi...

Barakoa Zimepomoka: Miaka 76 ya Ukaliaji Kimabavu wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina

Palestina haitakombolewa kwa kujifunza kuhusu historia yake. Kususia, kutengwa na vikwazo havitaikomboa Palestina. Palestina haitakombolewa kwa msaada wa chakula. Palestina itakombolewa wakati wana shupavu wa Umma katika majeshi ya Waislamu watakapowaasi watawala wasaliti, wakavunja minyororo yao na kuandamana kuelekea Al Quds.

Soma zaidi...

Zama za Mitandao ya Kijamii: Ufichuaji wa Uongo

Kuibuka kwa mitandao ya kijamii, watu wamejikuta wakiweza kuunganika na walioko maeneo mengine ya dunia. Hili liliyapa faida makampuni na serikali hadi ilipotumika dhidi yao. Wakati mauwaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina yalipoanza, watu wa Gaza waliweza kuunganika kwenye majukwaa kama ya TikTok na kuchapisha picha na video juu ya hali ya sasa.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu