Ijumaa, 27 Shawwal 1446 | 2025/04/25
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Taifa Imara huzaliwa kutokana na Fikra Imara

Akijibu maswali ya waandishi wa habari kuhusu ajenda katika Jumba la Rais, Rais Erdoğan alisema, “Mataifa imara yanajumuisha familia imara. Kama sharti la hadhara yetu ya zamani, sisi ni taifa linaloundwa kutokana na familia imara. Sio mahali pa mtu yeyote kuharibu muundo wa familia ya taifa hili. Tutalinda muundo wa familia yetu dhidi ya kila aina ya upotovu.”

Soma zaidi...

Minyororo ya Taratibu za Biashara Huria katika Mipaka ya Ardhi za Kiislamu

Mapema Oktoba, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mtakatifu Burhanuddin alitembelea mkoa wa Visiwa vya Riau, ambao ni eneo la mpakani nchini Indonesia. Aliomba kwamba upande wa mashtaka kwa kesi za Ulanguzi wa Dawa za Kulevya na Binadamu katika Visiwa vya Riau utoe athari ya kuzuia wahalifu katika eneo la Visiwa vya Riau (Kepri). Alitaka vifungu viweze kuongezwa.

Soma zaidi...

Unyumbuaji Misuli wa Kijeuri wa IMF ili kunyakua Utawala wa Uchumi wa Bangladesh Unafichua Uhusiano Halisi wa Bwana na Mtumwa

Mfuko wa Fedha wa Kimataifa umeelezea hatua pana za mageuzi, ikiwemo kuleta nidhamu katika sekta ya fedha na kuongeza ukusanyaji wa mapato, kwa Bangladesh kupata mkopo wa dolari bilioni 4.5. Hatua hizo zilijadiliwa wakati wa msururu wa mikutano kati ya ujumbe uliozuru wa IMF na mashirika mbalimbali ya serikali na idara za Bangladesh.

Soma zaidi...

Rishi Sunak – Waziri Mkuu Mwanabenki

Kazi ya kwanza ya Rishi Sunak ilikuwa katika benki ya uwekezaji ya Marekani Goldman Sachs. Aliendelea kwa miaka 14 katika sekta hiyo kabla ya kuwa mbunge. Kwa njia nyingi, uteuzi wake ambao si wa kuchaguliwa unaashiria hatua kuu ya utawala mkubwa wa fedha wa mfumo wa kisiasa na kiuchumi wa Uingereza - upenyezaji wa kimya kimya wa Westminster na Whitehall umekuwa ukifanyika kwa miongo kadhaa na bila kutambuliwa.

Soma zaidi...

Sheria ya Kupambana na Upotoshaji wa Habari

Sheria ya Kupambana na Upotoshaji wa Habari, pia inaitwa Sheria ya Mitandao ya Kijamii, imepitishwa na Bunge Kuu la Uturuki na kuanza kutekelezwa. Kwa mujibu wa sheria hii, mtu yeyote anayesambaza hadharani taarifa zisizo za kweli kuhusu usalama wa ndani na nje, utangamano wa umma na afya kwa jumla ya nchi kwa njia inayozua wasiwasi, hofu au kuogopa miongoni mwa umma kwenye mitandao ya kijamii kwa njia inayoleta usumbufu kwa amani ya umma ataadhibiwa kwa kifungo kuanzia cha mwaka 1 hadi miaka 3.

Soma zaidi...

Pindi Waokozi wanapofanywa kuwa Wahanga

Kiongozi wa BSP Imran Masood alisema mnamo Jumamosi katika tweet iliyotumwa kwa Kihindi, "Dola inageuka kuwa isiyo salama kwa mabinti chini ya utawala wa CM Yogi Adityanath. Huko Meerut, mwanafunzi wa BDS Vania Shaikh alijiua kwa kuruka kutoka kwenye mtaro, mwanafunzi mwenzake alimnyanyasa kimapenzi hadharani na kumpiga kofi kwa kupinga hilo.”

Soma zaidi...

Afya ya Watoto wa Umma iko Hatarini bila ya Khilafah

Mnamo tarehe 20 Oktoba 2022, BBC iliripoti kwamba Indonesia imepiga marufuku uuzaji wa dawa zote za kikohozi za watoto baada ya watoto 99 kufariki kutokana na kufeli kwa figo. Iligunduliwa kuwa viwango vya juu vya sumu haramu vilikuwepo ndani ya dawa zilizochafuliwa. Maafisa wanahofia kwamba idadi kamili ya vifo haijajulikana kwani dawa hizo zilikuwa na mzunguko mkubwa.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu