Jumanne, 29 Muharram 1448 | 2026/07/14
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Msikose Fursa ya Kuunda Mfumo Mpya wa Kimataifa, Enyi Waislamu — Nyinyi Ndio Watu Wake na Mnaliweza hilo Kupitia Itikadi Yenu Tukufu

Hivi majuzi, Rais wa Urusi Vladimir Putin alitembelea China, na mwishoni mwa ziara hiyo taarifa ya pamoja ya zaidi ya nukta arubaini ilitolewa. Ndani yake, nchi hizo mbili zilitangaza mikataba na makubaliano kadhaa. Hata hivyo, kinachoonekana katika taarifa hiyo ni wito wa nchi zote mbili wa mpangilio mpya wa ulimwengu wa nchi nyingi. Pia inaeleweka kwamba ziara ya Putin nchini China ilikuja baada ya ziara ya Rais wa Marekani Donald Trump nchini China, na baada ya ziara ya Putin kukamilika ilitangazwa kwamba rais wa China anakusudia kutembelea Korea Kaskazini.

Soma zaidi...

Hali Imefikia Hatua Ambapo Watawala wa Waislamu Wanacheza Kamari na Hatari ya Nyuklia Katikati ya Ardhi za Waislamu!

Afisi ya Habari ya Abu Dhabi iliripoti kwamba timu maalum za kukabiliana na dharura mnamo Jumapili zilidhibiti moto uliozuka katika jenereta ya umeme iliyoko nje ya eneo la ndani la Kiwanda cha Nguvu za Nyuklia cha Barakah katika eneo la Al Dhafra, kufuatia shambulizi la droni kwenye eneo hilo, bila majeraha yoyote au uvujaji wowote wa mionzi uliorekodiwa. Wizara ya Ulinzi ya Imarati ilieleza kwamba uchunguzi bado unaendelea ili kubaini chanzo cha mashambulizi hayo, ikibainisha kuwa maendeleo yoyote yatatangazwa mara tu uchunguzi utakapokamilika.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Msiruhusu Ardhi Zenu Kuwa Jukwaa la Majeshi ya Wakoloni!

Serikali ya Uingereza imetangaza kupelekwa kwa silaha ya gharama nafuu ya kupambana na droni katika operesheni zake za kijeshi Mashariki ya Kati. Katika taarifa yake, ilisema, “Mfumo mpya sasa umepelekwa katika kumbi za operesheni katika eneo la Mashariki ya Kati.” Pia ilisema kwamba Uingereza “itachangia kwa droni, ndege za kivita, na manuari katika misheni ya kimataifa ili kulinda Mlango-Bahari wa Hormuz.”

Soma zaidi...

Tangazo la Matokeo ya Uchunguzi wa Mwezi Mwandamo wa Shawwal 1447 H na Hongera kwa Idd Al-Fitr Iliyobarikiwa

Baada ya kuchunguza mwezi mwandamo wa Shawwal katika usiku huu mtukufu, usiku wa Alhamisi, kuonekana kwa mwezi mwandamo kumethibitishwa kwa kuonekana halali kisharia katika baadhi ya nchi za Waislamu. Kwa hivyo, kesho Alhamisi itakuwa siku ya kwanza ya mwezi wa Shawwal na siku ya kwanza ya Idd al-Fitr iliyobarikiwa.

Soma zaidi...

Tangazo la Matokeo ya Kuutafuta Mwezi Mwandamo wa Ramadhan Iliyobarikiwa ya Mwaka 1447 H

Ramadhan inakuja mwaka huu huku Ummah ukisimama kwenye njia panda mpya; kwa upande mmoja unageuka kwenye makaa ya hali ya ukoloni na miiba ya usaliti wa watawala, na kwa upande mwingine hali mpya zinazoibuka za kimataifa, haswa migogoro ya kafiri Magharibi ya kikoloni imetoa fursa mpya ambazo, ikiwa zitakamatwa, zingesababisha Ummah wa Kiislamu kuinuka kwa muda mrefu.

Soma zaidi...

Hitimisho la Kampeni “Khilafah sio Ndoto… Bali, ni Kilio cha Ulimwengu Unaowaka Moto!”

Leo, kwa Msaada Wake, tunahitimisha kampeni ya kimataifa iliyozinduliwa na Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir, kwa maelekezo ya Amiri wa Hizb ut Tahrir, mwanachuoni mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, katika kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, ambayo iliamshwa na wanaume na wanawake wa Hizb ut Tahrir kote ulimwenguni.

Soma zaidi...

Katika Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah... Dunia Inajitayarisha Kurudi Kwake

Mtu anaweza kufikiri, huku akiangalia yanayojiri hivi karibuni katika ngazi ya kimataifa na katika ardhi za Kiislamu, kwamba uhalisia unazidi kuwa wa giza tororo kwa Umma wa Kiislamu, na kwamba matumaini ya kuamka kwake na kuregeshwa kwa heshima yake yanafifia au kupungua. Hata hivyo, kutafakari haya yanayojiri kunaonyesha kwamba yanafichua matumaini ambayo yanajajidishwa na kuzidi kuwa makubwa, na mbinu ya kuelekea mwamko siku baada ya siku.

Soma zaidi...

Kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105, Tunaufufua Wito kwa Majeshi Yote ya Ummah Kuhamasisha Nguvu Zao Ili Kusimamisha Khilafah Rashida

Mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H, sawia na tarehe 3 Machi, 1924 M, amri ovu ilitolewa na lile lililoitwa Bunge Kuu la Kitaifa, ikielezea kufutwa rasmi kwa Khilafah. Kwa kuvunjwa kwa Khilafah, hukmu za Sharia ziliondolewa, kiapo cha utiifu (Bay’ah) kilisitishwa, na ardhi za Waislamu zilichanwa vipande vipande kwa misingi ya kitaifa na kikabila kuwa vijidola tete, tegemezi, na dhaifu. Vibaraka wa kulipwa waliteuliwa kuzitawala. Fikra ya umoja ilipigwa pigo kubwa. Kwa kuangamia kwake, Bayt al-Maqdis na Ardhi Iliyobarikiwa zilianguka, na umbile lenye saratani la Kiyahudi lilipandwa katikati ya ardhi za Waislamu.

Soma zaidi...

Unafiki wa Magharibi; Kati ya Kulaani Tukio la Sydney, na Kimya Juu ya Mauaji katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina

Bado hakuna kiongozi hata mmoja wa nchi au kiongozi wa Magharibi au wa Kiarabu ambaye hajashutumu tukio la Sydney, ambapo watu kumi na tano waliuawa kwa kupigwa risasi kufuatia shambulizi lililolenga tamasha la Mayahudi la Hanukkah jijini Sydney. Hata hivyo hatujaona azma mithili ya hiyo katika kulaani jinai za umbile la Kiyahudi katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina katika kipindi cha miaka miwili iliyopita. Kama kawaida, rai jumla ya umma imepotoshwa, na kupuuzwa kabisa nia ya tukio hilo, kwani kila mtu alijikita kukemea kitendo hicho, bila kujali sababu iliyowafanya washambuliaji hao wawili kuwafyatulia risasi washerehekaji.

Soma zaidi...

Watawala wa Waislamu Wameshikana Mkono kwa Mkono na Marekani na Mayahudi Kupitisha Mipango Yao, Na kwa Kauli na Shutma Tupu Pamoja na Waislamu

Umbile la Kiyahudi linaendelea kutekeleza jinai zake dhidi ya Gaza, Ukingo wa Magharibi, Lebanon na Syria; kumuua limtakaye, kupiga mabomu popote lipendapo, kubomoa nyumba na vituo, kujenga makaazi, na kuwaandama watu katika nyumba na ardhi zao, huku watawala wa Waislamu wakiendelea na misimamo yao ya fedheha ya kula njama na kurahisisha mambo kwa ajili yake, wakicheza dori ya mwangalizi na mwandishi wa habari anayeripoti habari na kutoa maoni yake kwa misemo isiyozuia wala kutibua njama.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu