Jumamosi, 12 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir Wakutana na Mkuu wa Harakati ya Wokovu wa Kitaifa

Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia inakutana na Bw. Ahmed Najib Al-Shabi, mkuu wa Harakati ya Wokovu wa Kitaifa, jana, Jumanne 11/02/2025. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hizb kwenye makao makuu ya Sakra Ariana, na uliongozwa na Bwana Al-Arabi Karbaka, mwanachama wa Hizb ut Tahrir. Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Bw. Al-Habib Hajji, Tamim Noura, Dkt. Faisal Darghouth, na Mhandisi Yasser Al-Anwar, wanachama wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir/Wilayah Tunisia.

Soma zaidi...

Kuanguka kwa Khilafah Kunaashiria Wito wa Kuhuishwa Kwake

Mnamo tarehe 3 Machi 1924, sawia na 28 Rajab 1342 H, kikundi kidogo cha wasaliti wa Kituruki, wakiongozwa na Mustafa Kemal, walivunja urithi wa zaidi ya karne 13 za umoja wa Waislamu. Kuanzia wakati huo na kuendelea, Waislamu walipoteza paa lao juu ya vichwa vyao na wakawa mayatima. Leo, miaka 104 ya hijria imepita tangu tukio hili la kusikitisha. Baada ya kuanguka kwa Khilafah, makafiri waligawanya ulimwengu wa Kiislamu katika maeneo madogo yaliyojitenga. Waliweka vikwazo vya usafiri kati ya maeneo haya, yakihitaji pasipoti na visa, na kuharibu majeshi yetu, silaha, rasilimali, ardhi, uwezo wa binadamu, na teknolojia-kila kitu.

Soma zaidi...

Vitisho vya Kutojali vya Trump Vitasambaratishwa dhidi ya Mwamba wa Ustahamilivu wa Gaza

Mara tu Trump alipotwaa urais wa Marekani, alianza kutoa vitisho kushoto na kulia. La kukasirisha zaidi kati ya haya lilikuwa ni tangazo lake la nia yake ya kuwahamisha kwa nguvu watu wa Gaza. Alisisitiza tena uungaji mkono wake wa kufukuzwa kwa kudumu kwa Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza hadi nchi nyingine wakati wa mkutano wake na Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi mnamo Jumanne, 4 Februari 2025. Hata alitangaza nia yake ya kununua ardhi ya Gaza na kuigeuza kuwa mradi wa uwekezaji!

Soma zaidi...

Trump asingeweza Kututawala kama Tungekuwa na Khalifa, na Umbile la Kiyahudi Lisingekuwepo bila Usaliti wa Watawala wetu

Viongozi wa ukafiri nchini Amerika na Ulaya, pamoja na chombo chao, umbile la Kiyahudi, wanajua kwamba misimamo ya watawala wa Waislamu, duara zao za kisiasa, na wapambe wao—wanaowatukuza—hawawakilishi wengi wa Waislamu, wala hawaakisi matumaini yaliyo ndani ya nyoyo zao kwa ajili ya kuregeshwa kwa mamlaka yao. Ukitaka kuelewa msimamo wao wa kweli na jibu lao kwa maamrisho ya Mwenyezi Mungu mbele ya chuki kwenu na kuwaua duniani kote, na kusubutu kwenu kutishia kukalia ardhi zao zaidi na kupora mali zao, musiangalie zaidi ya kiburi cha kiongozi wenu Trump. Kwa kutokuwa na haya mbele ya ulimwengu, ameonyesha kiburi cha Amerika kafiri na msaada wake kwa wale walioshukiwa na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu.

Soma zaidi...

Urusi Yajaribu Kubandika Shtaka la Ugaidi kwa Chama Kinachoheshimika zaidi cha Kisiasa ili Kuhalalisha Ukandamizaji na Kufilisika kwake!

Chini ya kichwa cha habari: "Huduma ya Usalama ya Urusi yakamata seli ya kigaidi yenye uhusiano na Hizb ut Tahrir," Russia Today ilichapisha ripoti mnamo 5 Februari 2025, ikisema kwamba "Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilisambaratisha seli ya kigaidi yenye uhusiano na Hizb ut Tahrir huko Crimea na kuwakamata watu watano ambao walikuwa wakisajili wafuasi wa chama hicho, ambacho kimepigwa marufuku nchini Urusi." Video ilionyeshwa inayoonyesha operesheni ya ukamataji na uvamizi wa nyumba.

Soma zaidi...

Al-Burhan Anatafuta Kuiga Mfumo Ule Ule wa Kisekula Uliopita

Katika hotuba iliyotolewa leo na Jenerali Al-Burhan, Mwenyekiti wa Baraza la Utawala na Amiri Jeshi Mkuu, alisema: "Kipindi kijacho kitashuhudia kuundwa kwa serikali ili kukamilisha kazi za mpito. Inaweza kuitwa serikali ya muda. Baada ya kuidhinishwa kwa waraka wa katiba, serikali itaundwa, na waziri mkuu atachaguliwa kutekeleza majukumu yake katika kusimamia baraza la mawaziri la serikali bila kuingiliwa."

Soma zaidi...

Enyi Majeshi ya Waislamu: Nani Atawakomesha Wapumbavu Hawa Wawili?!

Jana usiku, chaneli za satelaiti zilitangaza sherehe za mapokezi ya Rais wa Marekani Donald Trump kwa Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi, pamoja na mkutano wa waandishi wa habari uliotangulia mazungumzo yao. Trump alionekana kama mcheshi akilenga kufurahisha watazamaji wanaomtazama, kwa kauli zake za kizembe kuhusu Ukanda wa Gaza, na nia yake ya kuwaondoa watu wake na kuweka udhibiti wa Amerika juu yake.

Soma zaidi...

Trump Aitishia Gaza kwa Uvamizi wa Moja kwa Moja na Kuwafukuza Watu Wake

Jioni ya Jumanne, 4 Februari 2025, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza katika mkutano wake na Waziri Mkuu wa Kiyahudi kwamba "Wapalestina hawana chaguo zaidi ya kuondoka Ukanda wa Gaza. Nataka kuona Jordan na Misri zikipokea Wapalestina kutoka Gaza. Hakuna badali kwa wakaazi wa Gaza isipokuwa kuondoka." Aliongeza, "Jordan na Misri tayari zimekataa kuwapokea wakaazi kutoka Gaza, lakini baadhi ya watu wanakataa mambo isipokuwa hatimaye kukubaliana nayo."

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu