Jumamosi, 12 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Enyi Watu wa Sudan, Komesheni Mambo Matatu ya Marekani ambayo Yanahusisha Uhalifu Mkali: Vita, Kuitenga Darfur, na Uhalalishaji Mahusiano na Umbile la Kiyahudi

Kila mtu anashangaa juu ya siri iliyoko nyuma ya kuongezeka kwa kasi hii katika operesheni za kijeshi za jeshi hivi karibuni, kama vile vita vilivyokuwa hapo awali, na kwa zaidi ya mwaka mmoja, vimekuwa vikifanyika ndani ya duara lililofungwa, huku kukiwa na kusonga mbele na kurudi nyuma, bila ya kuwepo na uamuzi wa kijeshi kutoka upande wowote.

Soma zaidi...

Kwa Washiriki wa Kongamano lenye Kichwa: "Kashmir na Palestina inayokaliwa kwa mabavu - Suluhisho ni Nini?"

Imeharamishwa waziwazi kurudi kwa Umoja wa Mataifa (UN) kuhusiana na kadhia ya Kashmir, kwa sababu Umoja wa Mataifa ni Taghut, mamlaka yaliyojengwa juu ya msingi juu wa hukmu nyengine isiyokuwa ile aliyoiteremsha Mwenyezi Mungu (swt), kwa mujibu wa Sharia. Kuregelea kwa Umoja wa Mataifa ni kukaribisha Ghadhabu za Mwenyezi Mungu (swt).

Soma zaidi...

Maamuzi ya Mikutano ya Mawaziri wa Kiarabu ni Matupu na Hayatapita zaidi ya Maandishi kwenye Karatasi

Mkutano wa Mawaziri wa Pande Sita wa Kiarabu jijini Cairo mnamo Jumamosi, 1 Februari 2025, kuhusu Gaza na Kadhia ya Palestina ambayo ni pamoja na Jordan, Imarati, Saudi Arabia, Qatar, na Misri, pamoja na Katibu wa Kamati ya Utendaji ya Jumuiya ya Ukombozi wa Palestina na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu - walithibitisha katika taarifa yao kile walichokiita "uungaji mkono wao kamili wa watu wa Palestina juu ya ardhi yao na kuzingatia haki zao halali kwa mujibu wa sheria ya kimataifa."

Soma zaidi...

Wauyghur Pia Ni Sehemu ya Umma Bora, Musiwasahau

Tunapokaribia kumbukumbu ya mwaka wa 104 wa kuvunjwa kwa Khilafah, Umma wa Kiislamu unaendelea kupokea habari za ukandamizaji kutoka kwa maadui wake kila mahali, kuanzia Palestina hadi Syria, Sudan, Misri na China, ambako Waislamu wa Uyghur wanavumilia mateso na vikwazo vikali katika kila nyanja ya maisha yao.

Soma zaidi...

Hatari ya Uhamisho Inayotafutwa na Trump na Umbile la Kiyahudi Inalazimu Hatua Kali katika Kuamiliana nao kama Maadui

Utawala wa Jordan na kundi la watu wake wakati wote wa vita vya Kiyahudi dhidi ya Gaza walikuwa na bado wangali wanatetea kutowanusuru watu wa Gaza kijeshi, na angalau sio kufutilia mbali makubaliano ya udhalilishaji na aibu na umbile la Kiyahudi, lakini kwa busara na hekima na ujanja wa kisiasa hii ni hatua na udhoofishaji wa amani, usalama na chemchemi ya utulivu ambayo Jordan inaishi ndani yake. Mfalme alifikiri kwamba Uingereza ilimuamuru kurukuu na kujibu ajenda ya Amerika ambayo imelitawala eneo hilo tangu aingie madarakani, kufuatia mbinu ya baba yake, na kile ilichomuagiza kuhitimisha makubaliano ya pamoja ya ulinzi nayo mwaka 2021 ambayo yanahujumu kila maana ya ubwana wa nchi yoyote, na kuifungua nchi kwa ujumla kwa kambi za Amerika pekee na viwanda na vikosi vyake.

Soma zaidi...

Katika Kumbukumbu ya Kila Mwaka ya Kuvunjwa Khilafah na ukingoni mwa kuregea kwake, Tunaulingania Umma wa Kiislamu Uharakishe Kuisimamisha

Tangu Khilafah ilipovunjwa mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H, sawia na 3 Machi 1924 M, Ummah umekuwa ukipitia majanga na kushindwa mfululizo; kuanzia mgawanyiko wa ardhi yake, mpaka kunyang'anywa mali yake, na kuwaua wanawe, na kudhihakiwa matukufu yake na mashambulizi dhidi ya Sharia yake. Hata hivyo, leo Khilafah iko karibu zaidi kuliko wakati mwingine wowote kurudi, Rayah (bendera) yake iko tayari kupeperushwa kwa mara nyengine tena juu ya ardhi za Waislamu. Kwa hakika, tunaishi katika wakati unaokumbusha usiku ule watu wa Madina walipokuwa wakishauriana, wakikubaliana kwamba wakati umefika wa kumpa Bay'ah bwana wetu Muhammad (saw) kama kiongozi wao wa kisiasa na mkuu wa dola.

Soma zaidi...

Nani Anasherehekea Maadhimisho ya Isra na Mi’raj?

Tawala za ulimwengu wa Kiislamu zinatoa wito wa kuadhimisha kumbukumbu ya mwaka huu, licha ya kuwa wametambua uwepo wa umbile linaloinajisi ardhi iliyobarikiwa ya Isra na Mi’raj. Wamesimama kando, wakishuhudia mito ya damu ya Wapalestina ikitiririka, mabomu yaliyosababisha nyumba kuwa vifusi, na uharibifu ulioharibu vitongoji, mazao, na vizazi. Wametazama huku hofu ikiwashika wazee na vijana, huku njaa isiyo kifani ikiwasibu, na huku baridi ikigandisha miguu na nyoyo za watu.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Kenya Iliandaa Msururu wa Amali katika Kumbukumbu ya Miaka 104 ya Kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah

Kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 104 ya kuondolewa kwa Khilafah, Hizb ut Tahrir/Kenya ilifanya kampeni nchi nzima katika mwezi mtukufu wa Rajab 1446 H. Kampeni hii iliyoanza mwanzoni mwa mwezi mtukufu wa Rajab ilihusisha shughuli mbali mbali; Darsa, Semina na Visimamo. Hii ilikuwa ni kuukumbusha Ummah kuhusu hali yake ya kusikitisha ambayo umekuwa ukikabiliana nayo tangu kuondolewa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H sawia na tarehe 3 Machi 1924 M.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu