Uundaji wa Wanamgambo na Vikundi vyenye Silaha: Hatari Kubwa na Chombo cha Amerika cha Kugawanya Sudan
- Imepeperushwa katika Sudan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo Jumamosi, Novemba 16, 2024, kundi lenye silaha linalojiita Harakati ya Ukombozi ya Al-Jazirah lilitangaza nia yake ya “kulikomboa Jimbo la Al-Jazirah.” Pia lilionyesha uungaji mkono wake kwa vikosi vya jeshi. Katika video iliyosambazwa na vyombo vya habari na baadhi ya wanahabari wanaounga mkono jeshi, kundi hilo liliwataka watu wa Al-Jazirah kukusanyika karibu nalo na kukumbatia malengo yake.



