Afisi ya Habari
Wilayah Misri
H. 14 Safar 1447 | Na: 1447/11 |
M. Ijumaa, 08 Agosti 2025 |
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Mkataba wa Gesi na Umbile la Kiyahudi
Ununuzi wa Utajiri wetu ulioibiwa na Msaada kwa Adui yetu Mnyakuzi
(Imetafsiriwa)
Katika kitendo kipya kinachojumuisha kiwango cha mporomoko na ubaraka ambao utawala wa Misri umefikia, ilitangaza kusainiwa kwa makubaliano makubwa na umbile la Kiyahudi ya kuagiza gesi asilia kutoka kwa uwanja wa Leviathan katika ardhi iliyonyakuliwa ya Palestina, kwa thamani inayokaribia dolari bilioni 35 hadi mwaka wa 2040. Chini yake, umbile la Kiyahudi linauza nje ya nchi karibu mita za ujazo 130 za gesi nchini Misiri, kutumika kukidhi mahitaji ya ndani na kusafirisha nje kupitia vituo vya kutengeneza gesi vya Misri. Makubaliano haya yamepigiwa debe kama "kuimarisha usalama wa nishati," huku kiuhalisia yakiwa ni usaliti kwa Ummah, kupuuza utajiri wake, muungano na adui yake, na msaada kwa uchumi wake unaodhoofika.
Kwa kuzingatia migogoro ya kiuchumi na kisiasa ambayo umbile la Kiyahudi linapitia, mpango huu unaunda njia ya kifedha na kimkakati kwa umbile la Kiyahudi, kwani unaliletea mabilioni ya dolari kila mwaka, unalipatia mshirika wa kutegemewa katika mauzo ya nje, na kuliwezesha kujiweka kama mhusika mkuu katika uchumi wa nishati wa kanda. Kwa upande mwengine, watu wa Misri wanaburutwa katika utegemezi zaidi, udhalilifu, na umaskini, kwani mpango huu hauleti chochote isipokuwa madeni, kodi, na kupanda kwa bei, katika wakati ambapo wanateseka kutokana na uhaba wa umeme na gesi na gharama kubwa ya maisha.
Mtazamaji wa mpango huu hahitaji kuchunguzwa sana ili kutambua mgongano huo hatari: Misri, nchi ya Kiislamu, inanunua gesi kutoka kwa umbile mnyakuzi wa Ardhi Iliyobarikiwa! Na baya zaidi kuliko hilo ni kwamba, uwanja wa Leviathan na viwanja vyengine kamwe Mayahudi hawana haki yoyote ndani yake, bali walipewa chini ya makubaliano batili ya kuweka mipaka ya baharini yaliyohitimishwa na utawala wa Misri mwaka 2018, ambapo iliinyima haki ya Ummah katika maji yake ya kiuchumi, na hivyo kuthibitisha ushirikiano wake kamili katika uhalifu huo.
Serikali ya Misri inapigia debe mkataba huu kama mafanikio ya kiuchumi, wakati kiuhalisia ni utiifu, kujisalimisha, na fungamano la kiuchumi na adui mnyakuzi. Kwani makubaliano haya ni zao la moja kwa moja la mikataba ya uwekaji mipaka ya bahari ambayo serikali ilitia saini na umbile la Kiyahudi, Cyprus, na Ugiriki, ambayo yalipelekea kuachia maeneo makubwa ya maji yake ya kiuchumi kwa Mayahudi. Makubaliano haya ni batili katika Sharia, kwa sababu yanawakilisha kuachiliwa kwa ardhi, maji, na mali kwa Mayahudi, na utambuzi wa wazi wa umbile lao.
Mkataba huu wa gesi ni jinai mpya iliyoongezwa kwenye rekodi ya serikali katika kupuuza Ardhi Iliyobarikiwa na watu wake na ushirikiano wake na umbile hilo nyakuzi.
Enyi Askari wa Al-Kinana: Simameni kabla historia haijaandika kwamba mlikuwa mashahidi wa uwongo wa usaliti mkubwa ambao Ummah umewahi kuujua katika zama zake za kisasa. Simameni, kwani Mwenyezi Mungu atakuulizeni, mmoja baada ya mwengine, kuhusu silaha ambayo haikunyanyuliwa, kuhusu sauti ambayo haikusikika, na kuhusu Ummah kuchinjwa mbele ya macho yenu, nanyi hamkuunusuru. Na jueni kwamba saa ya hesabu inakuja, na kwamba Mwenyezi Mungu (swt) hadanganyiki kwa kaulimbiu, wala hadanganyiki kwa nembo. Basi msiwe povu kama povu la mto, wala msiwe walinzi wa batili inayodunga Dini yenu kwa nyuma, kisha ikanyanyua juu yenu bendera za batili... Na twamuomba Mwenyezi Mungu akuongozeni kwenye haki na akuruzukuni kuifuata.
[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ لاَ تَتَّخِذُواْ الْيَهُودَ وَالنَّصَارَى أَوْلِيَاء بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاء بَعْضٍ وَمَن يَتَوَلَّهُم مِّنكُمْ فَإِنَّهُ مِنْهُمْ]
“Enyi mlio amini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa ni marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni katika wao.”[Surat Al-Ma’idah :51]
Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Misri
Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari Wilayah Misri |
Address & Website Tel: http://hizb.net/ |
E-Mail: info@hizb.net |