Jumapili, 13 Muharram 1448 | 2026/06/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Moto Mijini: Jinsi Ubepari Unavyowasha Moto katika Miji ya Waislamu yenye Wakaazi Wengi

Mnamo Jumatatu, tarehe 1 Juni 2026, vyombo vya habari viliripoti kuhusu moto mkubwa ulioharibu eneo la makaazi lenye watu wengi huko Kebon Kosong, Kemayoran, Jakarta ya Kati, Indonesia. Takwimu rasmi kutoka kwa Wakala wa Kupunguza Maafa wa DKI Jakarta (BPBD) na uthibitishaji wa uwanjani zinaonyesha takriban familia 354—takriban watu 620—waliachwa bila makao. Takriban watoto 160 wenye umri wa kwenda shule waliathiriwa moja kwa moja.

Soma zaidi...

Ardhi Zetu Zitabaki Kukiukwa na Damu Yetu Itaendelea Kumwagika Hadi Tutakaposimamisha Khilafah Rashida Yetu

Mnamo Jumapili, tarehe 14 Juni 2026, jeshi la Kiyahudi lilifanya shambulizi la anga likilenga vitongoji vya kusini mwa Beirut, saa chache tu baada ya kuwaonya wakaazi wa takriban miji 30 kusini mwa Lebanon na kuwaamuru waondoke. Tovuti ya habari ya Axios iliripoti kwamba “jeshi la ‘Israel’ liliiarifu CENTCOM muda mfupi kabla ya shambulizi jijini Beirut kutokea.” Trump aliandika kwenye jukwaa lake la ‘Truth Social’ mnamo Jumapili: “Shambulizi la asubuhi ya leo dhidi ya Beirut halikupaswa kutokea, haswa katika siku maalum ambapo tuko karibu sana na Mkataba wa Amani na Iran.”

Soma zaidi...

Mtoto Aliyeuawa Shahidi, Kuhesabiwa kwa Waathiriwa Kutaisha Lini? Watu wa Damu hiyo Watainuka Lini Kuwalipiza Kisasi?

Wizara ya Afya ya Palestina ilisema kwamba vikosi vya uvamizi vilifyatua risasi kwenye gari moja lililokuwa limebeba raia wa Palestina katika mji wa Hebron katika Ukingo wa Magharibi wa kusini unaokaliwa kimabavu, na kusababisha kifo cha kishahidi cha mtoto mchanga wa miezi saba Sam Abu Hikal huku akiwa mikononi mwa mamake. Mamake na babake pia walijeruhiwa.

Soma zaidi...

Enyi Ummah wa Kiislamu na Majeshi Yake: Ikiwa Hamkasirishwi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na Mambo Yake Matakatifu, Basi Mtakasirishwa na Kuchukua Hatua kwa ajili ya Nini?!

Mnamo Jumatano, 27/5/2026, vyombo vya habari na mitandao ya kijamii vilirusha picha zinazoonyesha vikosi vya umbile la Kiyahudi vikimshambulia kikatili mwanamke mchanga wa Kipalestina huko Bab Hutta, moja ya malango ya Msikiti mtukufu wa Al-Aqsa, vikimnyang'anya kitambaa chake cha kichwani kwa nguvu kabla ya kumkamata. Tukio hili linajiri huku kukiwa na ongezeko la ukiukwaji wa sheria na hatua za usalama ulioongezeka kutoka kwa vikosi vya uvamizi katika milango ya kuingia katika Jiji la Kale la Al-Quds na malango ya Msikiti wa Al-Aqsa, sanjari na Idd al-Adha. Waliweka vituo vya ukaguzi na kuchunguza vitambulisho vya wapita njia, wakizuia idadi kubwa ya watu kuingia msikitini.

Soma zaidi...

Jibu kwa Mwandishi wa Makala (Usekula na Ugumu wa Historia ya Uislamu Iliyoghushiwa)

Uislamu ni itikadi ya kiroho na kisiasa ambayo ilikuja kushughulikia matatizo ya wanadamu, kwa kutambua kwamba wanadamu wana silika (ghariza) na mahitaji ya kimwili ambayo yanahitaji kushibishwa. Uislamu umebainisha jinsi mahitaji haya yanavyopaswa kukidhiwa bila ya ziada au upungufu, kupitia hukmu kutoka kwa Mwenye hekima, Mjuzi wa yote. Yeye aliyewaumba wanadamu anajua kipi kuna manufaa na kipi kina madhara kwao! Ukosefu wa elimu wa mwandishi juu ya hukmu hizi haumwondolei jukumu; badala yake, unasisitiza kutoujua kwake Uislamu.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Kadhia za Umma

Tunafuraha, kama Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio na hamu na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika Kikao cha kila mwezi cha Kadhia za Umma, ambacho mwezi huu kitafanyika katika afisi ya Hizb jijini Khartoum baada ya kukatizwa kwa muda mrefu kwa zaidi ya miaka mitatu kutokana na vita.

Soma zaidi...

Vikosi vya Msaada wa Haraka Vinafanya Mauaji Dhidi ya Watu Wasio na Silaha, na Serikali Haiwezi Kuwalinda!

Mnamo Alhamisi na Ijumaa, Mei 28 na 29, 2026, Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilizindua mashambulizi kwenye vijiji vilivyo magharibi mwa mji wa Bara katika Jimbo la Kordofan Kaskazini, na kusababisha vifo vya raia kadhaa wasio na silaha. Mtandao wa Madaktari wa Sudan ulithibitisha katika taarifa mnamo Ijumaa, Mei 29, 2026, kwamba RSF ilifanya mauaji makubwa katika mji wa Al-Marra na vijiji vinavyozunguka, na kuwaua raia 27. Katika ripoti yake ya hivi karibuni mnamo Jumamosi, Mei 30, 2026, Al-Arabiya TV ilisema: “Idadi ya vifo kutokana na mauaji ya Vikosi vya Msaada wa Haraka katika eneo la Al-Marra huko Kordofan Kaskazini imeongezeka hadi 58.” Wakati Vikosi vya Msaada wa Haraka vinafanya mauaji haya katika vijiji vya Kordofan, serikali inalaani tu na kuhesabu waliokufa, bila kuchukua hatua zozote kali kuzuia mauaji haya kutokea.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu