Jumamosi, 25 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kuna Uungwana kutoka Ng'ambo ya Bahari... Uko wapi Uungwana wa Jeshi la Misri?!

Katika wakati ambapo mauaji dhidi ya watu wa Gaza yamezidi, na ardhi kuungua chini ya miguu ya wanyonge, vyombo vya habari vya Marekani vimeandika kichwa cha kikuu habari kuhusu kijana Muislamu kutoka Misri aitwaye Mohammed Sabry Soliman, ambaye alituhumiwa kwa kurusha vinywaji vya Molotov kwenye maandamano ya kuunga mkono umbile la Kiyahudi nchini Amerika, akiimba "Uhuru kwa Palestina." Wakati vyombo vya habari vinajadili tukio hili, kiini cha tukio hili hakiwezi kupuuzwa: kijana Muislamu, aliyehama kutoka ng'ambo ya bahari, akisukumwa na maumivu ya moyo wake na maumivu ya Ummah wake, kueleza kukataa kwake kimya cha kimataifa na kufeli kwa Waarabu kushughulikia hali inayoendelea mjini Gaza.

Soma zaidi...

Pongeza kutoka kwa Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq kwa Sikukuu ya Idd al-Adha 1446 H

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq inatoa pongezi na baraka zake nyingi kwa Umma wa Kiislamu kwa mnasaba wa Idd al-Adha iliyobarikiwa. Hasa tunatoa salamu hizi kwa wabebaji da’wah, na kwa mwanachuoni mkubwa, Amiri wa Hizb utTahrir, Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah Mwenyezi Mungu amlinde na amhifadhi na ampe ushindi na tamkini kupitia mikono yake.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir Ndio Inayofanya Kazi Ipasavyo Kusimamisha Khilafah Basi Acheni Kuvuruga Ulinganizi Wake na Kuwakamata Wanachama Wake

Tangu kuanzishwa kwake kama chama cha kisiasa chenye msingi wa Uislamu mwaka 1953, Hizb ut Tahrir imefanya kazi ya kurudisha mfumo kamili wa Kiislamu wa maisha ya Kiislamu kupitia kusimamisha dola ya Kiislamu, ambayo dola yake ya kwanza ilianzishwa na Mtume Muhammad (saw) mjini Madina. Ingawa inafuata njia ya Mtume (saw) ya kusimamisha dola hii, haijishughulishi na kitendo chochote cha kinguvu au kile kinachoitwa vurugu katika kufanya hivyo.

Soma zaidi...

Kutafakari juu ya Gaza, Mfano wa Ibrahim (as) na Wito wa Haraka wa Nusrah Leo

Umma unapoingia katika siku tukufu za Tashriq, katikati ya ibada za Hijja, tunakumbushwa kwamba nguzo hii adhimu ya Uislamu ni safari ya kiroho, faradhi wa kiwahyi inayoonyesha kujitolea kipekee kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (swt). Ibada za Hijja zinajumuisha mila ya Nabii mtukufu Ibrahim (as), mke wake mtukufu Hajar (as), na mwanawe Ismail (as), familia ambayo mitihani yao iliufundisha Ummah asili ya tawakkul, imani isiyoyumba kwa Mwenyezi Mungu (swt), na kujisalimisha kikamilifu kwa amri Yake tukufu, hata pale amri hiyo inapopingana na mantiki ya kidunia.

Soma zaidi...

Historia Inawalingania Wanajeshi wa Pakistan – Wakati Umewadia wa Uongozi wa Kweli wa Kiislamu

Shambulizi la Pahalgam mnamo Aprili 2025, ambapo washambuliaji wenye silaha waliua raia 26 na kujeruhi wengine kadhaa, kwa mara nyingine tena limeitupa Kashmir katikati ya hali ngumu ya kisiasa na kiitikadi. Ingawa mamlaka mara moja zilielekeza kidole cha lawama kwa makundi ya wapiganaji yanayoungwa mkono na Pakistan kuwa yanahusika, tukio hilo liliingizwa siasa haraka na kuingizwa katika masimulizi mapana ambayo yameunda utawala wa Narendra Modi kwa zaidi ya muongo mmoja: mapambano kati ya dola ya kitaifa ya Kibaniani na wanaodaiwa kuwa maadui zake—wa ndani pamoja na nje.

Soma zaidi...

Ukamataji wa Waislamu nchini Urusi

Vikosi vya usalama vilipandikiza kazi za SIM wakati wa upekuzi katika nyumba za Waislamu, kesi za kushiriki katika shirika la kigaidi zilitungwa, jamaa zao walisema katika malalamiko kwa wanaharakati wa haki za binadamu. Kwa jumla, watu 48 walizuiliwa wakati wa operesheni ya vikosi vya usalama huko Nalchik na Nartan, Kavkazsky Uzel (tovuti ya habari) iliripoti mnamo Juni 3, ikinukuu wanaharakati wa haki za binadamu.

Soma zaidi...

Sheria ya Kimataifa ni Sheria ya Pori - Hairuhusiwi Kuiendea

Chini ya ufadhili wa Daniel Capoli, Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu katika misheni ya Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) nchini Yemen, ICRC huko Sana'a ilipanga, mnamo Jumanne na Jumatano, 20-21/05/2025, kwa ushirikiano na Wizara ya Habari na Wizara ya Mambo ya Nje, kozi ya mafunzo katika Wizara ya Mambo ya Nje kwa wafanyikazi wa vyombo vya habari na taasisi ya waandishi wa habari. Kozi hiyo ilishughulikia sheria za kimataifa, misingi na malengo yake, na istilahi zinazohusiana na sheria za kimataifa za kibinadamu, haswa katika suala la haki za binadamu katika ulinzi na maisha yenye staha, kuzuia ghasia, na kukidhi mahitaji ya vikundi vilivyo hatarini zaidi vinavyofinikwa na ulinzi wake, na vile vile kulinda raia dhidi ya athari za uhasama na kuharamisha mateso yasiyo na haja au madhara kupita kiasi.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen Inawapongeza Watu wa Imani na Hekima na Umma wa Kiislamu kwa Sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen inatoa pongezi zake za dhati na baraka zenye thamani kubwa zaidi kwa watu wa imani na hekima, na kwa Amiri wa Hizb, mwanachuoni mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, na kwa wanachama wote wa Hizb, na kwa Ummah mzima wa Kiislamu kwa sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa mwaka huu wa 1446 H. Mwenyezi Mungu airudishe kwao, juu yetu, na juu ya ulimwengu wote kwa kheri, baraka, na furaha.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu