Jarida la Al-Waie: Vichwa Vikuu vya Habari vya Toleo 455
- Imepeperushwa katika Jarida la Al-Waie
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Usekula wa Marekani unakumbwa na mgogoro mkubwa wa kitambulisho, ambao umeakisiwa hivi majuzi katika maoni yanayozidi kuwa tofauti kuhusu haki za LGBTQ+ na dori ya dini katika maisha ya umma.
Siasa za uchaguzi za Modi zinaegemea kueneza chuki za kidini dhidi ya Waislamu, katika maisha yake yote ya kisiasa. Wakati alipokuwa ni Waziri Kiongozi wa Gujrat mnamo 2002, Narendra Modi, alisimamia mauaji ya Waislamu zaidi ya elfu mbili. Mnamo tarehe 1 Machi 2002, katika kilele cha uchinjaji Modi alidai kwamba, “Kila kitendo kina majibu sawa na majibu ya kinyume yake (Har kriya ki pratigriya hoti hai).” Baadaye, akiwa waziri mkuu amesimamia uharibifu wa misikiti, ubomoaji wa nyumba za Waislamu na mashambulizi ya makundi ya watu dhidi ya jamii za Waislamu.
Mnamo siku ya Jumanne tarehe 25/6/2024, nilihukumiwa kifungo cha nje siku 60 katika Mahakama ya Jiji la Copenhagen kwa kutoa wito wa ukombozi wa Palestina. Jaji anayeendesha kesi aliamua wakati wa kutoa hukumu kwamba hotuba yangu ya 2021 katika suala hilo haikuelekezwa kwa Mayahudi kama kundi la kidini, lakini alitoa wito wa kuondolewa kwa umbile haramu la Kizayuni linaloitwa “Israel” kupitia uingiliaji wa kijeshi. Wito huu ulitangazwa na mahakama ya jiji kuwa sio halali!
Mnamo tarehe 24 Mei 2024, kitengo cha habari cha jeshi la Pakistan kilisema kuwa, “Mkuu wa Majeshi yuko katika ziara rasmi katika Jamhuri ya Shirikisho ya Ujerumani... Uongozi wa Ujerumani ulitambua dori ya Jeshi la Pakistan katika mapambano dhidi ya Ugaidi.”
Ingawa vyombo vya habari vinaitwa “nguzo ya nne ya demokrasia,” vikionyesha kutoegemea upande wowote na fikra yake, kama mamlaka ya mahakama kwa mfano, uhalifu uliofanywa na serikali ya Kiyahudi huko Gaza, na katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, ulitosha kufichua madai haya. Uhalifu huo ulifichua ukweli kuhusu vyombo vya habari na wanahabari. Jinai hizo zilionyesha wazi kwamba hakuna mamlaka ya kimaadili au uhalali, bali kwa ajili ya nguvu ya unyama, inayowakilishwa na dola za kimataifa na silaha zao duniani, ikiwemo Ulimwengu wa Kiislamu, ikiwa ni pamoja na watawala, serikali, na taasisi za vyombo vya habari.
Imani kwamba hatuwezi kuishi bila mfumo wa sasa wa ulimwengu labda ndio kikwazo kikubwa kwa usalama wa watu wa Palestina. Iwe kwa kujua, au kutojua, imani hii inaonekana kushikiliwa na watu kote ulimwenguni huku wakiendelea kujaribu kutumia njia za kidemokrasia kuwasaidia watu wa Palestina, licha ya ukweli kwamba wamewafelisha watu kote ulimwenguni.
Uongozi wa juu wa Pakistan umeidhinisha kuanzishwa kwa operesheni mpya ya kijeshi Inayoitwa Azm-e-Istehkam. Mpango huo mpya wa kijeshi unatarajiwa kuangazia vitisho vya usalama wa ndani na wapiganaji wenye silaha wanaovuka kutoka Afghanistan, huku kukiwa na taharuki inayoongezeka kati ya Islamabad na watawala wa Taliban jijini Kabul.
Gazeti la ‘The Daily Times’ liliripoti kuwa, “Sindh anasimamisha benki ya maziwa ya binadamu, inauregesha mpango huo kwa Baraza la Itikadi la Kiislamu... Benki ya kwanza ya maziwa ya binadamu nchini Pakistan iliundwa mapema mwezi huu na Taasisi ya Sindh ya Afya ya Mtoto na Matibabu ya Watoto (Neonatology)
Huku Mayahudi wa Kizayuni wakivuka mipaka yote katika ukatili wao, wito wa kampeni ya kisiasa ya Hizb #ArmiesToAqsa umefika kila barabara na kila kona, kwa Fadhila za Mwenyezi Mungu (swt). Wanafunzi wa vyuo vikuu mbalimbali, viongozi wa kisiasa, wanaharakati wa mitandao ya kijamii na umma kwa jumla sasa wote wanazidi kuimba, “Enyi Majeshi ya Waislamu, nendeni Palestina, nendeni Palestina.”