Jumapili, 27 Muharram 1448 | 2026/07/12
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Je, Inaweza Kusemwa Kuwa Zama za Ustawi wa Maendeleo ya Kisayansi Katika Ulimwengu wa Kiislamu ni Zao la Falsafa za Kigeni?

Waislamu lazima waibuke kutoka katika mporomoko. Hili angalau linakubalika kwa wote, waliberali na wanaharakati wa Kiislamu. Hata hivyo, tafauti inakuja katika fikra zinazopelekea katika uoni huu. Msukumo kwa msimamo wa waliberali ni maendeleo ya ajabu ya kisayansi na ya vitu ya Wamagharibi, ambayo yanaweka kipimo kwa waliberali.

Soma zaidi...

Kongamano la Nchi Zinazozungumza Kifaransa Lililofanyika nchini Tunisia ni Kongamano la Kufeli na Usaliti

Kongamano la 18 la marais wa nchi na serikali zinazoshirikiana matumizi ya lugha ya Kifaransa, linaloitwa Kongamano la Nchi Zinazozungumza Kifaransa (Francophone), litafanyika katika kisiwa cha Djerba mnamo Novemba 19 na 20, 2022, baada ya vikwazo vya mara kwa mara tangu ilipotangazwa mnamo 2020 kwamba litafanyika katika nchi yetu.

Soma zaidi...

Mkutano wa 5 wa Kimataifa wa Wanawake na Haki Unatumikia CEDAW

Mnamo Novemba 4-5, 2022 jijini Istanbul, “Mkutano wa 5 wa Kimataifa wa Wanawake na Haki” ulifanyika, kwa hotuba ya ufunguzi ya Rais Recep Tayyip Erdogan. Uliandaliwa na kikundi cha utetezi wa wanawake, Chama cha Wanawake na Demokrasia (KADEM) pamoja na Wizara ya Huduma za Familia na Jamii. Tamko la mwisho la mkutano huo lilisisitiza umuhimu wa familia yenye nguvu kwa jamii yenye nguvu.

Soma zaidi...

 Ajali ya Ndege ya Precision Inadhihirisha Hali ya Kutojali kwa Ubepari

Ndege ya Precision aina ya ATR42-500 (twin turboprop) yenye usajili 5H-PWF, na kumbukumbu ya safari PW494 ikiwa na abiria 43 safarini kutoka Dar es Salaam kwenda Bukoba, mkoani Kagera ilianguka ndani ya Ziwa Victoria ndani ya Bukoba siku ya Jumapili 06 Novemba 2022 kiasi cha saa 2.53 asubuhi. Ajali hiyo ilipelekea kufariki dunia watu 19 kama ilivyothibitishwa na shirika la Precision lenyewe, na pia kuthibitishwa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania.

Soma zaidi...

Mkataba wa Maelewano (MoU) wa Umeme kwa Maji ni Mwezeshaji Waziwazi wa umbile la Kiyahudi Kwa Gharama ya Watu wa Jordan na Ummah na Dhidi ya Chaguo lake la Kuikomboa Palestina

Mnamo tarehe 8/11/2022, juu ya kadhia za ziada za Mkutano wa Kilele wa Tabianchi huko Sharm El-Sheikh, Jordan, Imarati na umbile la Kiyahudi zilitia saini mkataba wa maelewano (MoU) ili kuendeleza upembuzi yakinifu na "kushiriki katika kutengeneza ala muhimu katika zilizopangwa kwa wakati kwa ajili ya mkutano wa COP28” utakaofanyika Imarati mnamo Novemba 2023, kuanzisha miradi miwili tofauti, inayotegemeana na kuhusiana; kwa lengo la kuasisi kiwanda cha kusafisha maji katika Bahari ya Mediterania kwa badali ya kuanzishwa kwa kiwanda cha kuazalisha umeme safi nchini Jordan.

Soma zaidi...

Muamala kwa Shule za Qur'an: Kwa Mara Nyengine Tena ni Dhihirisho la Sera dhidi ya Uislamu

Serikali imekubali mpango ambao Waziri wa Elimu Dennis Wiersma anataka kuutekeleza kwa shule za Qur'an, shule za wikendi na maeneo mengine ambayo 'elimu isiyo rasmi' inatolewa. Ufafanuzi kutoka kwa Wizara wa mpango huu wa kibaguzi ambao kwao Waislamu wanatengwa ni kwamba ndani ya elimu isiyo rasmi kumekuwa na kesi zinazodaiwa za shughuli ambazo 'zinapinga na uoanishaji, zinapinga demokrasia dhidi ya utawala wa sheria.'

Soma zaidi...

Jaribio la ATU la Kuwabandika Majina Wanachama wa Hizb ut Tahrir waliokuwa Wazungumzaji wa Makongamano ya Kisiasa ya Mtandaoni kuwa ni Wanamgambo ni Kitendo cha Ugaidi na Ukandamizaji

Serikali ya Hasina ilifanya jaribio jengine lililofeli la kusitisha dawah ya Hizb ut Tahrir katika kurudisha Mfumo kamili wa Maisha wa Kiislamu kupitia kusimamisha tena Khilafah Rashida kwa kuwahangaisha na kuwakandamiza wanachama wake kupitia kikosi chake maarufu cha kigaidi kinachojulikana kama "Kitengo cha Kupambana na Ugaidi (ATU)”.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu