Jumatano, 16 Muharram 1448 | 2026/07/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwisho wa Uvamizi wa Kijeshi wa Marekani na NATO: Fursa ya Kukabiliana na Ukoloni Laini na Hatua ya Kuelekea Khilafah kwa Njia ya Utume!

Miaka minne iliyopita, mnamo 31 Agosti 2021, uvamizi wa kijeshi wa miongo miwili wa Afghanistan na vikosi vya Amerika na NATO ulimalizika, kwani mwanajeshi wa mwisho wa Amerika aliondoka nchi humu usiku wa manane. Hii ilikuwa hasa kwa sababu ya mhimili wa Wamarekani kuelekea Indo-pacifiki, kupunguza kasi ya maendeleo ya China. Nchi za Kiislamu, hususan Mujahidina wa Afghanistan walikuwa wamewaumiza kichwa Wamarekani na kukengeushwa na mkakati huu mpya. Tunatoa pongezi zetu kwa mafanikio haya ya kihistoria na siku kuu kwa Waislamu wote, hasa kwa watu wa Afghanistan, wabebaji Dawah, na Mujahidina.

Soma zaidi...

Miradi ya Wamarekani – Mayahudi ni Miradi ya Jinai na Uhaini, Iwe Inatekelezwa na PLO au Wengine

Chaneli 5 ya Kiebrania, kama ilivyoripotiwa na Al Jazeera, ilitangaza ripoti iliyosema kwamba Netanyahu anafanya mkutano kujadili kuchukua nafasi ya Mamlaka ya Palestina pamoja na viongozi wa kikabila huko Al-Khalil (Hebron). Taarifa ilitolewa baadaye na Gavana wa Al-Khalil (katika kujibu mashauri yanayoendelea ya serikali ya uvamizi kuhusu kuitenganisha Al-Khalil kutoka kwa jiografia ya kitaifa na kuikabidhi kwa utawala wa kikabila).

Soma zaidi...

Mpango wa Mipaka ya Damu na Uhalifu wa Kujitenga kwa Darfur

Baada ya kuanguka kwa kutia shaka kwa miji mikubwa ya Darfur, na kuondolewa kwa jeshi kutoka kwao, mbele ya utekaji nyara wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), pamoja na kuzingirwa kwa nguvu na vikosi hivi katika jimbo la mwisho lililosalia, Darfur Kaskazini na mji mkuu wake, Al-Fashir, wakati jeshi likishindwa kuwafukuza, ghafula yanakuja mazungumzo ya serikali sambamba yakiongozwa nao huko Nyala, mji mkuu wa Darfur Kusini, ambao wanaudhibiti, kwa ushiriki wa vibaraka wa Amerika kama vile Al-Hilu, na uungaji mkono wake kwa serikali hii, hata kuwa naibu ndani yake.

Soma zaidi...

Mauaji ya Halaiki ya Sudan: Dori ya Omar al-Bashir

Ingawa mengi yanajulikana kuhusu mauaji ya halaiki yanayowakumba ndugu na dada zetu nchini Palestina, machache sana yanajulikana—au yanasambazwa—kuhusu wale walio nchini Sudan, ambao kwa muda wa miezi 18 iliyopita wamevumilia mauaji ya halaiki ya kimya kimya. Ukatili huo umeua zaidi ya watu 15,000, zaidi ya milioni 10 wamekimbia makazi yao, na kuacha nusu ya watu—watu milioni 25—wakikabili uhaba wa chakula na njaa.

Soma zaidi...

Hakuna Suluhisho kwa Suala la Sudan Isipokuwa Kutawalisha Uislamu

Tangu uhuru wake mnamo tarehe 1/1/1956, Sudan imeshuhudia mfululizo wa mapinduzi ya kijeshi. Ya kwanza ilikuwa jaribio lililofeli lililoongozwa na Ismail Kabida, ambaye alijaribu kupindua serikali ya kwanza ya kitaifa iliyoongozwa na Ismail al-Azhari. Hii ilifuatiwa na mapinduzi ya kwanza yaliyofaulu yaliyoongozwa na Luteni Jenerali Ibrahim Abboud mnamo Novemba 1958 dhidi ya serikali iliyochaguliwa ya al-Azhari.

Soma zaidi...

Na anaye fedheheshwa na Mwenyezi Mungu hana wa kumhishimu. [Al-Hajj: 18]

Baada ya maafikiano yote yaliyofanywa na PLO, ambayo yalifikia uhaini mkubwa kwa kuitoa sehemu kubwa ya Palestina. Na baada ya kukubalika kwake kuwa chombo cha usalama (katika muundo wa mamlaka) kinachowapiga vita watu wa Palestina, kupokonya silaha kambi za ndani ya Palestina kwa kuua, kuzingira na kukamata, na nje ya Palestina kwa uratibu na serikali za Syria na Lebanon, ili kuzuia tishio lolote, kubwa au dogo, kwa usalama wa Mayahudi ndani au karibu na Palestina.

Soma zaidi...

Huku Amerika Ikiunga Mkono Mauaji ya Halaiki mjini Gaza, Inaingia Uzbekistan Kama Mshirika wa Usalama!

Mnamo tarehe 28/8/2025, Rais Shavkat Mirziyoyev alimpokea Mjumbe Maalum wa Rais wa Marekani wa Ushirikiano wa Kimataifa, Paolo Zampoli. Kulingana na taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Huduma ya Habari ya Rais, “Mkutano huo ulijadili ushirikiano wa kimkakati kati ya Uzbekistan na Marekani na upanuzi wa ushirikiano wa pande nyingi.”

Soma zaidi...

Watu wa Al-Fashir Baina ya Nyundo ya Vita na Kinoo cha Njaa, na Hawana Wokovu isipokuwa kwa Dola ya Khilafah

Mji wa Al-Fashir, mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini, unashuhudia janga halisi la kibinadamu, huku kukiwa na vita kati ya pande zinazopigana, ambapo makumi ya raia waliuawa katika siku chache zilizopita, huku wakaazi wakiteseka kutokana na kuzingirwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, na njaa ya makusudi, katika kivuli cha kimya cha kituliwa shaka cha kimataifa, huku Umoja wa Mataifa ukithibitisha mauaji ya angalau watu 89 katika mapigano ya siku zilizopita.

Soma zaidi...

Mvua ni Baraka na Rehema, lakini bila Uchungaji imekuwa ni Laana!

Ni huzuni na pia inasikitisha kwamba msimu wa mvua hauji kwa ghafla, bali ni kipindi cha taarifa ambacho hurudiwa kila mwaka. Kinachoshangaza zaidi ni kwamba vituo vingi vya uchunguzi wa hali ya hewa vilionya kuhusu mvua kubwa, lakini asasi za serikali hazikuchukua hatua yoyote kuzuia madhara yake, ambayo yalikuwa mabaya zaidi kwa vijiji vya Jimbo la Mto Nile, mashariki mwa Sudan na hata Kordofan, miongoni mwa kwengine.

Soma zaidi...

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Taqli Watoa Wito Mkali kwa Waislamu Kutibua Mpango wa Marekani wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/ Wilayah Sudan ya kukwamisha mpango wa kuisambaratisha Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kuzingatia umoja wa Ummah kama suala nyeti, suala la uhai na kifo, wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Sheikh Yahya kituo cha kuhifadhi Quran. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa matabaka yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, wanazuoni, maafisa na askari na wengineo, wakiwahimiza kutimiza wajibu wao wa kidini ili kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu