Alhamisi, 26 Shawwal 1446 | 2025/04/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Unyanyasaji wa Watoto Umefikia Kiwango cha Juu sana nchini Ufilipino, huku nchi za Magharibi zikiwa ndio Wahalifu Wanaoongoza

Ufilipino ndiyo nchi yenye uzalishaji mkubwa zaidi wa nyenzo za unyanyasaji wa watoto. Mashirika ya kutoa misaada yamekadiria kwamba mtoto 1 kati ya 5 hudhulumiwa, na kwa kawaida wazazi na watu wa ukoo hufaidika kutokana na unyanyasaji huo. Kufungwa kwa miji wakati wa Janga la maambukizi kuliwaacha watoto walio hatarini wakiwa wamenaswa na watu wazima walio na tamaa ya kifedha.

Soma zaidi...

Siasa za Kidemokrasia zina Faida Sana kwa Wanasiasa

Mwaka mmoja baada ya kashfa ya mbunge wa Uingereza Owen Paterson kupelekea ahadi za udhibiti mkali, wanasiasa wamevuna £5m kutokana na kazi ya pembeni, gazeti la ‘The Observer’ limeripoti.

Kwa ujumla, wabunge walipata zaidi ya £5.3m kutokana na kazi za nje kuanzia Oktoba 2021 na Septemba 2022, huku wengi, wakiwemo mawaziri wa zamani, wakichukua majukumu mapya kama washauri na wasio watendaji katika mwaka uliopita kwa makampuni ambayo katika kesi kadhaa yaliendeshwa na wafadhili wakuu wa vyama.

Soma zaidi...

Kizazi Kichanga - Mshawishi katika Kusimamisha Uislamu

Uteuzi wa Dato Seri Anwar Ibrahim kuwa Waziri Mkuu wa 10 wa Malaysia hatimaye umemaliza kipindi cha siku 5 cha ‘wadhifa wazi wa serikali’ baada ya Uchaguzi Mkuu wa 15 (GE15). Mfalme wa Malaysia, Yang di-Pertuan Agong Sultan Abdullah Ri’ayatuddin Al-Mustafa Billh Shah, ameridhia uteuzi huu na kuanzishwa kwa serikali ya umoja ya Malaysia.

Soma zaidi...

Hatua za Kwanza za Kupiga Marufuku Shule za Quran Uholanzi

Serikali ya Uholanzi inachukua hatua dhidi ya mashirika yasiyo rasmi ya elimu ya Kiislamu kama vile shule za Qur'an na shule nyingine za kibinafsi ambapo watoto wanaweza kujifunza Kiarabu na Quran. Hii inahusisha safu nzima ya hatua za vikwazo ili kuingilia kati, kufuatilia na kubadilisha mtaala wa elimu ya Kiislamu.

Soma zaidi...

Mamlaka za Kyrgyzstan Zaendelea Kuwatesa Wabebaji Dawah

Oktoba 31, 2022 Huduma ya habari ya Kamati ya Serikali ya Usalama wa Kitaifa ya Jamhuri ya Kyrgyz kwenye ukurasa wake wa tovuti iliripoti: “Shughuli za seli ya chinichini ya Shirika la Kidini lenye itikadi kali (REO) “Hizb ut-Tahrir al-Islami” zimekandamizwa. Mnamo Oktoba 27, 2022, ndani ya muundo wa kesi ya jinai iliyoanzishwa chini ya Kifungu cha 332 sehemu ya 2 (Uzalishaji, usambazaji wa nyenzo zenye msimamo mkali) ya Kanuni ya Jinai ya Jamhuri ya Kyrgyz, wanachama 11 wachangamfu wa REO “Hizb ut-Tahrir al-Islami”.

Soma zaidi...

Uongozi wa Kijeshi Sio Ngawira

“Waziri Mkuu Shehbaz Sharif alimteua Jenerali Asim Munir kama mkuu wa jeshi mpya wa Pakistan, chaguo ambalo linaweza kuimarisha upinzani wa Waziri Mkuu wa zamani Imran Khan kwa serikali na kuzua mapigano yake makubwa na jeshi. Khan, ambaye kama waziri mkuu alimuondoa Munir kutoka wadhifa wa mkuu wa upelelezi, atauona uteuzi huo kama kikwazo kinachowezekana kwa jaribio lake la kulazimisha uchaguzi wa mapema...

Soma zaidi...

Magharibi inawatakia nini Waislamu kupitia Thaqafa yake wa Kimagharibi?

KUN.UZ na tovuti zingine za habari ziliripoti kwamba mnamo Novemba 14-16, Tashkent iliandaa “Kongamano la Pili la Ulimwengu la Malezi na Elimu ya Mtoto Wadogo  (WCECCE).” Akizungumza katika kongamano hilo, Rais wa Uzbekistan, Shavkat Mirziyoyev, alipendekeza kupitisha azimio maalum la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu matokeo ya Kongamano hilo la Kiulimwengu, kuhusu umuhimu wa kuwasomesha watoto, kama jambo muhimu katika kufikia maendeleo ya wanadamu wote. Pia imependekezwa kuasisiwa kituo cha kikanda cha UNESCO huko Tashkent.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu