Jarida la Al-Waie: Vichwa Vikuu vya Habari vya Toleo 443
- Imepeperushwa katika Jarida la Al-Waie
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Asubuhi ya Jumamosi, Julai 22, 2023 M, Hizb ut Tahrir/Wilayah Tunisia itafanya kongamano kwa mnasaba wa kumbukumbu ya Hijra ya Mtume.
Tangu kukaliwa kimabavu kwa Iraq mwaka 2003, mvamizi Marekani imekuwa ikicheza karata ya kimadhehebu na hata kuanzisha mfumo wa kimadhehebu na kikabila ili kuisambaratisha nchi hiyo. Waliamua kugawanya sehemu za Masunni na Waarabu kutoka kwa Wakurdi na kutangaza kwamba sehemu ya Mashiya inawakilisha idadi ya walio wengi.
Nchini India, wanawake wa Kiislamu kwa mara nyingine tena wanakuwa walengwa wa ajenda ya kisiasa ya chama tawala cha Bharatiya Janata Party (BJP) chini ya uongozi wa Waziri Mkuu Narendra Modi. Pendekezo la Kanuni Sawa ya Kiraia (UCC) si chochote zaidi ya jaribio jipya la kudhibiti zaidi maisha ya wanawake wa Kiislamu na kuzuia desturi zao za Kiislamu.
Nina maswali mawili muhimu, na natumai kuwa jibu litakuwa la kina kadiri inavyowezekana, nikijua kuwa majibu yanayochapishwa ni ya kina kila wakati, lakini ningependa dalili nyingi za Shariah zenye maelezo ya kina ili ufahamu wa maswala haya uwe wa kina.
Mnamo Julai 17, wizara ya mambo ya nje ya Urusi ilitangaza kuwa nchi hiyo itaondoka kwenye makubaliano ya Mkataba wa Nafaka wa Bahari Nyeusi ambao umesaidia kuleta nafaka za Ukraine katika masoko ya dunia katika mwaka uliopita.
Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan imeandaa kampeni kwa kichwa, “Umma Mmoja… Khilafah Moja” katika mitandao ya kijamii.
Kwa Mabadiliko ya Kweli... Kataeni demokrasia... Simamisheni Khilafah.
Baada ya miezi mitatu ya mauaji, uharibifu, ufurushaji, uporaji wa mali ya umma na ya kibinafsi, na uharibifu wa miundombinu, Marekani imerejea kuzungumza kuhusu majadiliano kati ya pande zinazozozana nchini Sudan.
Katika ripoti ya kushangaza ya vyombo vya habari juu ya ukamataji na maandamano ambayo yamefanyika katika maeneo yaliyokombolewa kwa zaidi ya miezi miwili, waangalizi wa France 24 walitushangaza kwa mkusanyiko wa uwongo wa makusudi ambao chaneli kama France 24 haifai kufanya isipokuwa ikiwa wahariri wake bado wangali chini ya athari ya mshtuko wa maandamano yaliyozuka katika nchi yao iliyokumbwa na mgogoro.