Jumamosi, 24 Shawwal 1447 | 2026/04/11
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Wanawake na Watoto wa Kiislamu Wanakumbwa na Njaa Hadi Kufa Nchini Somalia huku Watawala wa Waislamu Wakiunga Mkono Ukandamizaji Ulimwenguni

Mnamo tarehe 5 Oktoba 2022, BBC iliripoti kuwa Somalia inakabiliwa na baa la njaa inayotokana na ukame mbaya zaidi kuwahi kutokea katika kipindi cha miaka 40. Hadithi ya dada mmoja Muislamu inayofichuliwa na waandishi wa habari, ni ile ya Fatima Omar ambaye alimzika mtoto mmoja wa kiume kutokana na njaa na tayari alikuwa ameshamzika bintiye wa miaka 3 ambaye alifariki huku akitembea kwa siku 10 kutafuta msaada. Anawaambia waandishi wa habari kwamba hakuwa na nguvu za kumzika mtoto wake na alilazimika kuuacha mwili wake kando ya barabara huku akijua kuwa Fisi walikuwa wanakaribia kuingia ndani.

Soma zaidi...

Kipindupindu Kinawaua Watu wa Syria, Hivyo Iko Wapi Dola ya Kuwanusuru?!

Wizara ya Afya ya Utawala wa Syria ilitangaza mnamo Jumatatu kuwa mkurupuko wa kipindupindu katika maeneo kadhaa umewauwa watu 29, vifo na majeruhi vilikolea katika jimbo la kaskazini la Aleppo, ambapo watu 25 walithibitishwa kufariki, na maelfu kadhaa ya visa vinavyoshukiwa kuripotiwa kote nchini kuanzia Septemba 19, kulingana na data iliyopatikana na chama cha misaada kutoka Kitengo cha Afya cha Serikali ya Syria (GoS), Idara ya Kibinafsi ya Mamlaka ya Afya ya Mitaa, Kaskazini na Mashariki mwa Syria.

Soma zaidi...

Jinsi Vita Vilivyoshindwa vya Amerika Dhidi ya ‘‘Ugaidi’’ Vingali Vinawatoa Kafara Watu

Thomas West, Mwakilishi Maalum wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Amerika kwa Afghanistan, katika hotuba yake ya hivi majuzi katika Kituo cha Mafunzo ya Kimkakati na Kimataifa (CSIS) alisema: "Kwa kweli ninaogopa - na nadhani hii ni itifaki - kwamba tunachokiona sasa ni kusimama kidogo katika miaka 44 ya mzozo na kwamba tunaweza kuona kurudi kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe katika wakati wowote”.

Soma zaidi...

Waziri wa Mambo ya Ndani wa India Amit Shah Anaongoza katika "Ni Nani anacheza ngumu dhidi ya Waislamu!"

Mnamo tarehe 28 Septemba 2022, Serikali ya India ya BJP ilipiga marufuku shirika la India la Popular Front na mashirika mengine 8 yanayohusiana yaliyosajiliwa kwa miaka 5. Serikali ilidai kuwa imepiga marufuku PFI na makundi washirika wake kwa madai ya kufanya "shughuli zisizo halali" ambazo "zinaathiri uadilifu, uhuru na usalama wa nchi".

Soma zaidi...

Bangladesh Yazidi Kutumbukia ndani ya Mtego wa Indo-Pasifiki Uliotegwa na Marekani Mkoloni Mwenye Kiburi

Ripoti ya hivi punde ya Pentagon ilisema kwamba viongozi wa kijeshi wa Marekani wameanza kufanya maandalizi ya kulinda maslahi ya Marekani katika eneo la Indo-Pacifiki. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Marekani inafanya mazoezi ya kijeshi na kubadilishana mipango na nchi mbalimbali za eneo la Indo-Pacifiki kwa malengo maalum. Makamanda wa Komandi ya Indo-Pacifiki ya Marekani walisisitiza kuongezeka kwa ushirikiano katika eneo lote.

Soma zaidi...

Kuwa "Mzayuni Mkubwa" Kunamaanisha kuwa kama Putin na Kusaidia Uvamizi Kikatili na Haramu

Katikati ya uchumi unaofeli, mfumko wa bei wa tarakimu mbili, viwango vya rehani vinavyoongezeka, bili za juu za kawi, mabadiliko ya kodi, kupanda kwa deni, mgogoro wa pesa za mfuko wa pensheni, vita nchini Ukraine, sarafu inayoshuka thamani, ongezeko la uhamiaji na idadi inayodidimia ya wapiga kura, Waziri Mkuu mpya wa Uingereza (na labda nusu ya baraza lake la mawaziri) alipata wasaa wa kujitokeza kwenye hafla ya kando ya CFI kwenye dhifa ya kongamano lao la chama ambapo alijitangaza kwa fahari kuwa "Mzayuni mkubwa."

Soma zaidi...

Mkuu Mstahiki wa Jeshi ni Yule Anayekataa Kuitegemea Marekani, Anatoa Nusrah kwa ajili ya Kusimamisha Tena Khilafah na Kuhamasisha Kuikomboa Kashmir Iliyokaliwa

Jenerali Bajwa kwa sasa yuko jijini Washington, akifanya mikutano ya kuagana na mabwana zake. Ajenda yake ni kuhakikisha kwamba Pakistan inasalia ndani ya mtego wa utumwa wa Marekani baada yake, anapofanya mazungumzo thabiti pamoja na Pentagon na maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani.

Soma zaidi...

Karne ya Uturuki: Uasherati, Utegemezi, Kurudi Nyuma na Mengine Mengi

Akizungumza katika mwaka wa 6 wa utunzi wa sheria wa muhula wa 27 wa Bunge Kuu la Uturuki, Erdoğan alisema, "Tukiregelea maadhimisho ya miaka 100 ya kuanzishwa kwa Jamhuri yetu, ambayo tutasherehekea pamoja kwa shauku mwaka ujao, tunakuja katika uwepo ya taifa letu mwaka 2023 na neno jipya. Ahadi hii ni kujenga 'Karne ya Uturuki' juu ya kazi na huduma ambazo tumeleta katika nchi yetu hadi sasa.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu