Jumanne, 18 Dhu al-Qi'dah 1447 | 2026/05/05
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Je, Ugaidi ni Quran na Vitabu, Enyi Mliofilisika

Tovuti ya Russia Today ilichapisha ripoti ya habari mnamo tarehe 5/2/2025 ikisema kwamba "Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilisambaratisha seli ya magaidi yenye mafungamano na Hizb ut Tahrir katika Rasi ya Crimea na kuwakamata watu watano waliokuwa wakisajili wafuasi wa Hizb, ambayo imepigwa marufuku nchini Urusi." Ripoti hiyo ilijumuisha video inayoonyesha operesheni ya ukamataji na uvamizi wa nyumba, ambapo ilionekana wazi kwamba kile ambacho idara ya usalama ya Urusi ilichukua kutoka kwa nyumba za Mashababu ni nakala za Al-Quran Al-Kareem, vitabu, na vijitabu vya kisiasa na kifikra vya Kiislamu - machapisho maarufu ya Hizb ut Tahrir kwa jina pamoja na maalumati yaliyomo.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Kuongezeka kwa Uhasama nchini Sudan

Al Arabiya Net ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 4/2/2025: "Jeshi na vikosi vyake vya usaidizi viliingia katika maeneo ya kusini-mashariki ya Jimbo la Khartoum wakati wa saa zilizopita, wakitokea Jimbo la Al-Jazeera.." na tovuti ya Youm7 ilichapishwa mnamo tarehe 2/2/2025: "Mwandishi wa Kituo cha Habari cha Cairo aliripoti katika habari mpya zinazochipuka kwamba jeshi la Sudan linachukua idadi kadhaa ya vijiji mashariki mwa mto Nile katika Jimbo la Khartoum." Kabla ya hapo, mnamo tarehe 11/ 1/2025, Vikosi vya Msaada wa Haraka vilishindwa na jeshi la Sudan katika mhimili wa Jimbo la Al-Jazeera na mji mkuu wake, Wad Madani, “na kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka, Hemeti, alikiri katika kanda ya sauti iliyohusishwa naye kwamba vikosi vyake vilishindwa katika Jimbo la Al-Jazeera...” (Al-Jazeera 1/13/2025).

Soma zaidi...

Uhamisho au Ukombozi, enyi Umma wa Kiislamu?

Dhalimu wa Marekani, Trump, alisema katika mkutano na waandishi wa habari pamoja na mhalifu Netanyahu jioni ya Jumanne, 4 Februari 2025: "Marekani itachukua Ukanda wa Gaza, na tutafanya kazi nayo pia" Aliongeza, "Tutageuza Ukanda wa Gaza ulioharibiwa kuwa Riviera ya Mashariki ya Kati." Alizungumzia juu ya umiliki wake wa muda mrefu wa Gaza na alisisitiza taarifa yake ya awali kuhusu kuwahamisha watu wa Gaza, ambapo alisisitiza kutiishwa kwa watawala wa Misri na Jordan na wasaidizi wao, akisema: "Misri na Jordan zilisema hazitapokea wakaazi kutoka Gaza, na mimi nasema lazima watapokea." Hapo ndio watawala watiifu, wasaliti.

Soma zaidi...

Kutangaza Jamhuri nchini Syria ni Usaliti wa Mapinduzi ya Kiislamu!

Ahmed al-Shara, ambaye alifanya ziara yake ya kwanza ya kigeni nchini Saudi Arabia baada ya kuchukua kiti cha Urais nchini Syria, alitoa taarifa muhimu kuhusu mustakabali wa Syria sambamba na ramani ya utendakazi ya kisiasa ambayo amedumisha katika mahojiano na televisheni ya Syria. Akiahidi kukuuza uchumi wa soko huru na vifaa vya uwekezaji, Shara alisema, "Syria ni nchi ambayo itahifadhi hali yake ya asili, muundo wa serikali utakuwa wa jamhuri, kutakuwa na bunge, tawi la utendaji na mamlaka zinazofanya kazi kwa ushirikiano kati yao." alitumia maneno yake. (Mawakala)

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Uhamishaji wa Watu wa Gaza

Al Jazeera ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 26/1/2025: “Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba anaishinikiza Jordan, Misri na nchi nyingine za Kiarabu kupokea wakimbizi zaidi wa Kipalestina kutoka Gaza, baada ya vita vya Israel dhidi ya Ukanda huo kusababisha mgogoro wa kibinadamu. Alipoulizwa ikiwa hili lilikuwa pendekezo la muda au la muda mrefu, Trump alisema, “Inaweza kuwa hili au lile.”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Indonesia: Katika Kumbukumbu ya Kuvunjwa kwa Khilafah “Palestina itakombolewa kupitia Khilafah na Jihad”

Kwa mnasaba wa kumbukumbu (miaka 104 H) ya kuvunjwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab Tukufu 1342 H sawia na 03/03/1924 M mikononi mwa wahalifu wa Kiarabu na Kituruki, na kwa kuzingatia mauaji ya kikatili (mauaji ya halaiki) yaliyofanywa na umbile nyakuzi la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina), Hizb ut Tahrir / Indonesia iliandaa matembezi makubwa katika mji mkuu wa Jakarta yenye kichwa “Palestina itakombolewa kupitia Khilafah na Jihad”.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu