Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 532
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 104 Hijria ya kuvunjwa dola ya Kiislamu (Khilafah) mnamo tarehe 28 Rajab Tukufu mwaka 1342 H sawa na 03/03/1924 M mikononi mwa wahalifu wa Kiarabu na Kituruki, na kwa kuzingatia mabadiliko na mishtuko mikali inayotokea ndani na karibu na ardhi ya Ash-Sham, Hizb ut Tahrir/Wilayah Lebanon inaandaa kongamano lenye kichwa: “Mabadiliko katika Ardhi ya Ash-Sham... Wasiwasi na Bishara!”
Mnamo tarehe 5 Januari, iliripotiwa kwamba umbile la mauaji la Kizayuni lililishambulia kwa mabomu Ukanda wa Gaza zaidi ya mara 100 katika muda wa siku 3 tu, na kuua zaidi ya watu 200 - wengi wanawake na watoto. Shabaha hizo zilijumuisha majengo ya makaazi, vikundi vya watu waliokusanyika barabarani na sokoni, na wale walio ndani ya makaazi yao. Pia iliripotiwa kuwa mtoto wa 8 aliganda hadi kufa katika Ukanda huo kutokana na baridi kali inayovumiliwa na wale wanaoishi katika mahema ya muda ambayo hayatoi ulinzi dhidi ya hali ya hewa ya baridi kali, na pia kutokana na kikwazo katili cha Wazayuni ambacho kinazuia mahitaji muhimu kama vile chakula, mafuta na nguo za majira ya baridi na blanketi kutokana na kuingia Gaza.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jordan Ayman Safadi, wakati wa kushiriki kwake katika Kongamano la Kiuchumi la Dunia huko Davos mnamo Jumatano, 22/01/2025, alisema kuwa mbinu yoyote ya baadaye ya Gaza lazima iegemee juu ya umoja wa Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi na lengo la kufikia amani tu kwa msingi wa suluhisho la dola mbili. Alisema: “Katika muktadha wa suluhisho la kisiasa, serikali ya Palestina ndiyo pekee inayoshikilia uamuzi wa amani na vita, na hakupaswi kuwe na makundi ya kisilaha nje yake.”
Katika mahojiano na gazeti la ‘Financial Times’, waziri wa mambo ya nje wa Syria alifichua ruwaza ya serikali mpya ya Syria baada ya Assad, akisisitiza kwamba nchi hiyo “haitaki kuishi kwa msaada,” na kwamba suluhisho liko katika kupunguza vikwazo vya Amerika na Ulaya. Aliongeza kuwa serikali haina mpango wa kusafirisha mapinduzi hayo ng’ambo au kuingilia masuala ya nchi nyingine. Hivyo, ikionyesha mabadiliko makubwa katika sera ya kigeni. Pia alionyesha katika mahojiano yayo hayo nia ya kubinafsisha bandari na viwanda vinavyomilikiwa na serikali na kuvutia uwekezaji wa kigeni, licha ya changamoto kubwa zinazoikabili Syria, ikiwemo madeni ya dolari bilioni 30 kwa washirika wa zamani wa Assad; Iran na Urusi.
Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina inatoa pongezi na baraka zake kwa wafungwa walioachiliwa huru na familia zao baada ya kuachiliwa kutoka katika magereza ya madhalimu.
Tangu Khilafah ilipovunjwa mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H, sawia na 3 Machi 1924 M, Ummah umekuwa ukipitia majanga na kushindwa mfululizo; kuanzia mgawanyiko wa ardhi yake, mpaka kunyang'anywa mali yake, na kuwaua wanawe, na kudhihakiwa matukufu yake na mashambulizi dhidi ya Sharia yake. Hata hivyo, leo Khilafah iko karibu zaidi kuliko wakati mwingine wowote kurudi, Rayah (bendera) yake iko tayari kupeperushwa kwa mara nyengine tena juu ya ardhi za Waislamu. Kwa hakika, tunaishi katika wakati unaokumbusha usiku ule watu wa Madina walipokuwa wakishauriana, wakikubaliana kwamba wakati umefika wa kumpa Bay'ah bwana wetu Muhammad (saw) kama kiongozi wao wa kisiasa na mkuu wa dola.
Mnamo Jumanne na Jumatano, wizara za mambo ya nje za Jordan, Saudia, Imarati, Mamlaka ya Palestina na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu zililaani uchapishaji wa akaunti rasmi unaohusiana na umbile la Kiyahudi wa ramani za kanda hiyo ambazo ni pamoja na maeneo ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, Jordan, Lebanon na Syria, wakidai kwamba hayo ni ramani ya kihistoria ya umbile la Kiyahudi. Walionyesha wasiwasi wao kuhusu masuala mawili.
Mnamo tarehe 06/01/2025, rufaa ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Najib Tun Razak kuhusu kuwepo kwa amri ya nyongeza ya Mfalme, inayomruhusu kutumikia kifungo chake kilichosalia chini ya kifungo cha nyumbani, imekubaliwa na mahakama kwa wingi wa 2-1. Majaji wa Mahakama ya Rufaa kisha wakaamuru kesi hiyo irudishwe katika Mahakama Kuu ili ombi la Najib la uhakiki wa mahakama lisikizwe na jaji mpya. Amri hii ya nyongeza, ambayo ni sehemu ya mchakato wa msamaha wa kifalme, imekuwa jambo la kawaida, ambalo halijawahi kutokea katika asili yake. Sambamba na hilo, kulikuwa na jambo jengine - mkusanyiko mkubwa wa kuonyesha mshikamano uliokusanyika nje ya mahakama, ulioandaliwa na vyama ambavyo hapo awali vilikuwa wapinzani wa kisiasa wa Waziri Mkuu huyo wa zamani.
Kalima iliyotolewa na shab Muhammad Ali Al-Aouni kwenye Barabara ya Al-Thawra katika mji mkuu Tunis wakati wa kisimamo kilichoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Tunisia kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 14 ya mapinduzi nchini Tunisia.