Mgogoro wa Dolari ya Kimarekani Tanzania na Pengine ni Kielelezo cha Ubwana wa Mabavu ya Marekani Kiuchumi
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Tanzania kama nchi nyingine nyingi inakabiliwa na mgogoro wa uhaba wa fedha ya dolari ya kimarekani. Ripoti zinasema akiba ya fedha za kigeni mwishoni mwa mwezi wa Aprili 2023 ni dolari bilioni 4.9, na ndani ya mwezi wa Julai 2023 ni bilioni 5.55. Kwa mujibu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), hifadhi hiyo inaweza kukidhi mahitaji ya uagizaji wa bidhaa kwa takriban miezi mitano.