Jumanne, 06 Shawwal 1447 | 2026/03/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kwa Mujibu wa Uislamu, Hairuhusiwi Kugombea, au Kupiga Kura kwenye Chaguzi za Kidemokrasia

Ushiriki wa Muislamu katika Demokrasia ni jambo lenye kuwashughulisha watawala, wanasiasa, wasomi na watungaji sera. Hii ni ima Waislamu wakiwa katika Ulimwengu wa Kiislamu, au wakiishi ughaibuni katika nchi za Magharibi. Hivyo kuna mjadala kuhusu ushiriki wa Muislamu katika Demokrasia nchini Australia, Uingereza na Amerika, kama ulivyo mjadala kuhusu ushiriki wa Waislamu katika uchaguzi nchini Uturuki, Pakistan na Misri.

Soma zaidi...

Sintofahamu ya GISB: Nukta ya Mabadiliko ya Kushughulikia Upotofu na Kuregesha Khilafah

Katika wiki za hivi karibuni, Global Ikhwan Sdn Bhd (GISB) imekabiliwa na uchunguzi mkali kutoka kwa mamlaka kufuatia wasiwasi wa muda mrefu juu ya desturi zake potovu. Ingawa ripoti zilikuwa zimewasilishwa dhidi ya GISB mapema zaidi, hatua za hivi majuzi za polisi zinaashiria hatua ya kwanza muhimu ya kupunguza shughuli za kundi hili. GISB, ambayo mizizi yake inatoka kwenye vuguvugu la Al-Arqam ambalo sasa limezimika, imevutia umakini wa watu wengi kwa kulingania vitendo vya upotofu vya Aurad Muhammadiyah na madai ya utovu wa nidhamu, hasa katika uendeshaji wa nyumba za misaada.

Soma zaidi...

Bangladesh Haipaswi Kuyaangalia Mataifa ya Kibeberu ya Magharibi kwa Mafanikio na Ufanisi wake na Isiwe Mwathiriwa wa Siasa za Jografia za India na Marekani

Mshauri mkuu wa serikali ya mpito ya Bangladesh Dkt. Muhammad Yunus alitoa wito kwa viongozi wa kimataifa kuunga mkono ujenzi wa Bangladesh mpya wakati akizungumza kwenye mapokezi kando ya Mkutano Mkuu wa 79 wa Umoja wa Mataifa jijini New York mnamo Jumanne. Mara tu baada ya hotuba hiyo, rais wa Marekani Joe Biden pia alisema ikiwa wanafunzi wa Bangladesh wanaweza kujitolea sana kwa ajili ya nchi yao, Marekani pia inapaswa kufanya zaidi.

Soma zaidi...

Hawajaridhika na Uharibifu wa Gaza, Wazayuni Sasa Wanaendeleza Uhalifu Wao hadi Lebanon

Baada ya mwaka mmoja wa kampeni ya wazi ya mauaji ya halaiki dhidi ya watu wa Palestina, iliyofanywa mchana kweupe kwa ushirikiano wa dola za kimataifa na watawala wa Waislamu wanaowazunguka, Wazayuni hivi sasa wameendeleza jinai zao hadi Lebanon kwa kulipua mabomu kiholela katika makaazi yenye wakaazi wengi, na kuua maelfu ya watu tayari, kwa matumaini wanaweza kurekebisha sura yao iliyoshindwa baada ya kampeni yake angamivu mjini Gaza.

Soma zaidi...

Majeshi ya Waislamu Yanasukumwa na Marekani Popote Inapotaka, Lakini Hayasukumwi na Uungwana wa Al-Mu'tasim!

Kanuni msingi ya majeshi ya Waislamu ni kwamba wabebe Aqida ya Kiislamu (itikadi); ipasavyo, haijuzu kwao kuchukua hatua yoyote mpaka wajue hukmu ya Mwenyezi Mungu kuhusu hilo. Lakini kwa bahati mbaya wamejisalimisha kwa watawala wasaliti na vibaraka, wakitii amri zao na kutekeleza maamuzi yao hata wakiwa katika ghadhabu ya Mwenyezi Mungu.

Soma zaidi...

Viumbe Vioga zaidi vya Mwenyezi Mungu Vinaonyesha Ujasiri baada ya Mashujaa Kuzika Vichwa vyao kwenye Mchanga!

Operesheni Kimbunga cha Aqsa “Tufan Al-Aqsa” kwa hakika imezifichua na kuzidhihirisha tawala za khiyana katika ardhi za Waislamu na watawala wao wasaliti. Vile vile imewasilisha hoja ya wazi kwa watu wenye nguvu na ushawishi katika Ummah, hususan majeshi yake, na hatimaye, imefichua uwongo na udanganyifu wa kile kinachoitwa “Mhimili wa Upinzani.”

Soma zaidi...

Ukatili wa Kiyahudi unaweza tu Kukomeshwa kwa Kuivunja Mipaka ya Mgawanyiko ya Dola za Kitaifa na kuyaleta Majeshi ya Kiislamu chini ya Bendera ya Shahada ya Khilafah (Imetafsiriwa) Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, l

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, leo (27/09/2024) iliandaa maandamano na matembezi ya kulaani katika majengo ya misikiti tofauti ya Dhaka na Chittagong kupinga mashambulizi ya kuendelea dhidi ya Palestina na Lebanon yanayofanywa na umbile haramu la Kiyahudi.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu