Jumamosi, 03 Shawwal 1447 | 2026/03/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ujasiri Wenu Kwa Mwenyezi Mungu, Enyi Madhalimu, Unatangaza Kukaribia Mwisho Wenu

Wakati Mayahudi walipokuwa wakiizingira Hospitali ya Kamal Adwan mjini Gaza, kisha kuivamia, kisha kuichoma moto, na kuwapeleka wagonjwa, majeruhi, na wafanyikazi wa matibabu kwenye hatima isiyojulikana hadi wakati wa kuandika taarifa hii, badala ya mamlaka hiyo kulaani uhalifu wao, badala ya kuuchochea ulimwengu dhidi ya vitendo vyao viovu na vya kikatili, badala ya kuuhamasisha Umma wa Kiislamu kuwanusuru watu wa Gaza, badala ya kuona haya kwa heshima ya majeraha ya Gaza na Ukingo wa Magharibi, walikataa kufanya chochote isipokuwa kuwa Jenin, wakifanya matendo ya Mayahudi na kuwanyanyasa watu wa Palestina mithili Mayahudi wanavyowanyanyasa.

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina Yafuata Mbinu za Mashetani Kuhalalisha Uhalifu wake katika Kambi ya Jenin!

Mamlaka ya Palestina (PA) ilikusanya vyombo vyake vya habari na vipaza sauti vya wasemaji na nzi wa kielektroniki (wanyanyasaji wa mtandaoni wanaounga mkono serikali) ili kuchafulia jina kambi ya Jenin na watu wake na kuhalalisha umwagaji wa damu yao. Kisha, ilikusanya vyombo vyake na majambazi katika mji wa Khalil al-Rahman, na wachache wa wale walioitwa watu mashuhuri waliojiuza kwa PA kwa manufaa maovu, na wale ambao iliwatishia kutoka kwa wafanyikazi na walimu. Ilitumia wizara, shule zilizofungwa, na kukodi mabasi ili Jimbo la Khalil al-Rahman, mji na wilaya, ionekane kuwa pamoja nayo katika kumwaga damu ya watu wa kambi ya Jenin. Hii ijapokuwa inajua na wale walio nyuma ya kwamba Khalil al-Rahman, pamoja na watu wake na koo zake, hawawezi kukubali kwamba itoa nusu ya neno kumwaga tone la damu ya Waislamu. Kwa kitendo hiki kiovu, inataka kuleta mgawanyiko kati ya watu wa Palestina (kaskazini na kusini) chini ya pazia la uongo la uhalifu wake.

Soma zaidi...

Unyonyaji Mbaya wa Bima ya Afya na Takaful

Tangazo la hivi majuzi la Chama cha Bima ya Uhai ya Malaysia (LIAM), Shirika la Takaful la Malaysia (MTA), na Jumuiya ya Bima Jumla ya Malaysia (PIAM) la kuongeza bima ya afya na malipo ya takaful kwa kiwango kikubwa mno cha 40% hadi 70% ni jambo la kushangaza. Dhihirisho la ulafi wa kirasilimali. Ingawa mashirika haya yanahusisha kupanda kwa gharama za matibabu na kuongezeka kwa mahitaji ya huduma ya afya, nia halisi ni dhahiri: kuongeza faida kwa gharama ya umma.

Soma zaidi...

“Mayahudi Hawawi Radhi Nawe, Wala Wakristo, Mpaka Ufuate Mila Yao” [Al-Baqarah: 120]

Utawala mpya nchini Syria umetoa taarifa mtawalia kuhusu mfumo wa serikali ambayo wananuia kutekeleza baada ya dhalimu kutoroka. Ni wazi kuwa si mfumo aliouweka Mwenyezi Mungu (swt) bali ni mfumo wa kisekula unaotenganisha dini na maisha kwa kisingizio cha kuwapa watu uhuru wa kuchagua mfumo wa utawala. Wanawaruhusu waandamanaji wa kike wanaodai uhuru na kuvua hijab, huku wakiwateka nyara waandamanaji wasafi wanaodai kuachiliwa kwa jamaa zao wanaotaka kutabikishwa kwa Shariah ya Mwenyezi Mungu (swt)!

Soma zaidi...

Mabadiliko ya Kweli Yanaweza Tu Kuja Kutokana na Mradi Unaotokana na Aqidah ya Ummah. Ni nani Aliye Nao?

Umma wa Kiislamu umeishi kwa karne moja katika unyonge na udhalilishwaji, mfarakano na mgawanyiko, na utegemezi kwa nchi kubwa. Hii inatokana na matendo ya watawala Ruwabidha (wajinga watepetevu) ambao hawaheshimu udugu au ahadi yoyote, wanachojali tu ni kubakia kwenye viti vyao vibovu (vya utawala), kutekeleza mipango ya nchi za Kikafiri katika ardhi zetu ili kukazanisha udhibiti wao juu yetu na kupora mali zetu. Wamesimama dhidi ya kila mtu anayewapinga au kutokubaliana nao, au kujaribu kuwabadilisha, na kuwaweka chini ya kifungo, mateso, mauaji, na ukiukaji wa matukufu. Bashar al-Assad na utawala wake wa kihalifu sio wa mwisho wao, ambaye uhalifu dhidi ya watu wake ulifichuliwa na matukio ya hivi majuzi nchini Syria, uhalifu ambao ni wa aibu na kuwafukuza wale wenye maumbile yaliyo sawa.

Soma zaidi...

Amerika ya Trump Itashindwa Kufanya Kile ambacho Kikongwe Biden Hakuweza Kukifanya

“Rais mteule wa Marekani Donald Trump ametoa kauli kadhaa zenye utata ambazo zinaakisi waziwazi ukubwa wa tofauti katika sera za ndani na nje za Marekani na za Rais anayeondoka wa chama cha Democrat Joe Biden. Kwa upande wa sera ya mambo ya nje, Trump alisema atakomesha kile alichokitaja kuwa machafuko katika Mashariki ya Kati, kusitisha vita nchini Ukraine, na kuzuia kuzuka kwa Vita vya Tatu vya Dunia, bila kueleza jinsi atakavyofanya haya yote...

Soma zaidi...

Kizungumkuti cha Syria: Kati ya Ukosefu wa Utambuzi na Tumaini la Kweli

Baada ya miaka 14 ya vita na ukandamizaji, Syria inaonekana iko tayari kwa mabadiliko huku utawala wa Bashar al-Assad ukianguka na vikosi vya upinzani, vinavyoongozwa na Abu Mohammad al-Julani, vikichukua Damascus. Hata hivyo, matumaini ya mustakabali mzuri zaidi yanavurugwa na ushawishi mkubwa wa dola za nje kama vile Marekani na Uturuki, ambao zinaongoza njia ya Syria chini ya mifumo ya kisekula, inayoungwa mkono na Magharibi kama vile Azimio 2254 la Umoja wa Mataifa. Hili linazua maswali muhimu sana kuhusu iwapo tumaini la kweli linaweza kuwepo bila kukataa utawala wa kigeni na kuzipa kipaumbele kanuni za Kiislamu.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu