Jumatano, 27 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/17
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Muungano na Amerika hauruhusiwi kwa Pakistan, wala Muungano na India hauruhusiwi kwa Afghanistan

Waziri wa Ulinzi wa Pakistan Khawaja Asif mnamo Jumatatu (20 Oktoba 2025) alitupilia mbali madai ya Afghanistan kwamba Islamabad inatenda kwa niaba ya Marekani ili kuunda mabadiliko ya serikali jijini Kabul, akielezea madai hayo kama “upuuzi mtupu”. Islamabad imesema kwa muda mrefu kwamba India, hasimu wake wa muda mrefu, inafanya kazi pamoja na Afghanistan kusaidia Tehreek-e-Taliban Pakistan (TTP), ambayo inajulikana kama Taliban ya Pakistan, na wanamgambo wengine dhidi ya Pakistan. New Delhi inakanusha madai hayo.

Soma zaidi...

Watu Wapendao Uislamu wa Nchi Wameukataa Mkataba wa Julai, ambao umejengwa juu ya Msingi wa Usekula na Demokrasia Batili ya Magharibi, Na Wanataka Mkataba wa Madina uliojengwa juu ya Msingi wa Imani yao Safi ya Kiislamu

Mnamo 17 Oktoba 2025, kipote cha wanasiasa wenye uchu wa madaraka nchini humu walitia saini ‘Mkataba wa Julai - suluhisho la kisiasa lililoandikwa kwa kuzingatia imani potofu za kidemokrasia ya kisekula na mfumo wa Wakoloni makafiri wa Magharibi hasa Marekani-Uingereza, na kuweka mfano mwengine wa kuchukiza wa usaliti kwa Uislamu na Waislamu, na utiifu kwa nchi za Magharibi. Mfumo huu wa kisekula wa kibepari uliotungwa na wanadamu umefeli katika nchi zote duniani. Jambo hili ni la kweli mithili ya mwangaza wa mchana kwamba, mfumo huu wa ukandamizaji unalinda maslahi ya tabaka tawala, mabepari wachache na wakoloni wa Magharibi, na kuwanyonya watu wengi zaidi. Mnashuhudia kwamba kizazi cha vijana (Gen-Z) katika nchi nyingi wanaasi tabaka tawala la kibepari moja baada ya jengine na kuwaangusha watawala.

Soma zaidi...

Mfuko wa Fedha wa Kimataifa wafikia Kukaba Uchumi wa Yemen ili Kukamata Rasilimali Zetu za Kiuchumi

Mnamo tarehe 15/10/2025, Gavana wa Benki Kuu ya Aden, Ahmed Al-Maabqi, alikutana jijini Washington D.C., na mkuu wa ujumbe wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) nchini Yemen, Esther Pérez Ruiz, na mwakilishi wa IMF, Mohamed Maait, akiandamana na Naibu Waziri wa Fedha Hani Wahab na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Waziri Msaidizi wa Fedha Abdul Qader Amin. Hii ilifuatiwa na mkutano kati ya Waziri wa Mipango na Ushirikiano wa Kimataifa na Gavana wa Yemen kwa Benki ya Dunia, Waed Badhib, na Riccardo Puliti, Makamu wa Rais wa Shirika la Fedha la Kimataifa wa Kanda ya Mashariki ya Kati, pamoja na ushiriki wa Naibu Waziri wa Mipango Nizar Basuhaib, Naibu Waziri wa Fedha Hani Wahab, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Abdul Qader Amin, kwa uwepo wa Stefan G. G. Reimbert, Mkurugenzi wa Kanda wa Benki ya Dunia katika Mashariki ya Kati, na Dina Abu Ghaida, Meneja wa Benki ya Dunia nchini Yemen.

Soma zaidi...

Mafunzo Kutokana Na Jinsi Nchi Kubwa Zaidi ya Kidemokrasia Duniani Inavyowafelisha Wanawake wa Kiislamu

Gazeti la ‘The Indian Express’ limechapisha makala yenye kichwa “Pindi kutokuwepo kukizungumza kwa sauti ya juu zaidi kuliko uwepo: Wanawake wa Kiislamu na Bunge la India”. Yanazungumzia ukosefu mkubwa wa uwakilishi wa wanawake wa Kiislamu katika afisi yake. Tangu Lok Sabha ya kwanza (Bunge la Kidemokrasia la India) mnamo 1952, ni wanawake kumi na nane pekee Waislamu ambao wamekuwa wachangamfu ndani bunge. Uwakilishi mdogo umerekodiwa katika kitabu kipya kilichoandikwa na waandishi wa habari Rasheed Kidwai na mwanasayansi wa siasa Ambar Kumar Ghosh chenye kichwa “Kukosekana Bungeni: Wanawake wa Kiislamu katika Lok Sabha”, kilichochapishwa na Juggernaut (2025). Waandishi hawajali katika utambuzi wao wa jinsi uwakilishi kama huo ulivyokuwa mara nyingi. Kwa vyama vingi vya kisiasa, ugombezi wa mwanamke wa Kiislamu ulifanya kazi kama ishara tu badala ya athari na ushawishi halisi.

Soma zaidi...

Kuwakataa Wanariadha wa ‘Israel’: Kipimo Halisi cha Msimamo Madhubuti wa Indonesia?

Indonesia: Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) ilikataa rufaa ya Shirikisho la Michezo ya Viungo (Gymnastics) la ‘Israel’ (IGF) kuruhusu wanariadha wake kushiriki Mashindano ya Dunia ya Sanaa za Gymnastiki jijini Jakarta, Indonesia, kuanzia Oktoba 19–25, 2025. Serikali ya Indonesia iliwanyima viza wachezaji sita wa mazoezi ya viungo wa ‘Israel’, ikionyesha uungaji mkono kwa Wapalestina na shinikizo la ndani. IGF ilkata rufaa kwa CAS na Shirikisho la Kimataifa la Gymnastiki (FIG), ikiomba hatua za kuhakikisha ushiriki au kubatilisha michezo hiyo. CAS ilitupilia mbali rufaa zote mbili, na FIG ilisema haina mamlaka juu ya maamuzi ya visa. Indonesia ilithibitisha tena msimamo wake, ikiegemea katika sera yake ya kigeni na hisia za umma.

Soma zaidi...

Ukamatwaji wa Wanachama wa Hizb ut Tahrir jijini Beirut!

Katika marudio ya mbinu na hatua za ukamataji holela wa vyombo vya usalama bila msingi wowote wa kisheria, wa watu—baadaye waliotambuliwa kuwa wanachama wa chombo cha usalama chenye mfungamano na serikali—wakiwa kwenye pikipiki waliwakamata wanachama wawili wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Lebanon walipokuwa wakigawanya taarifa moja ya kulaani kuendelea kwa uvamizi wa Kiyahudi dhidi ya Lebanon na watu wake. Kukamatwa huku kulitokea jana, 17/10/2025, baada ya Swala ya Ijumaa mbele ya Msikiti wa Imam Ali katika eneo la Tariq al-Jadida jijini Beirut.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu