Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 548
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Bila kujali ubwana wa nchi, serikali ya mpito inaendelea na mchakato wa kukabidhi huduma na mabohari mbalimbali ya Bandari ya Chittagong muhimu kimkakati na kiuchumi kwa wageni kwa jina la kuongeza uwezo wa bandari kwa kisingizio cha uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni (FDI). Kama sehemu ya hili, mchakato wa kukabidhi Bohari Kuu la Kontena la New Mooring (NCT) la Bandari ya Chittagong linalojitosheleza na la juu zaidi la kuzalisha mapato kwa kampuni ya DP World uko katika hatua zake za mwisho (Daily Jugantor, Mei 6, 2025).
Mnamo siku ya Jumanne,13/5/2025, vikosi vya usalama vya Mamlaka ya Palestina vilimuua kijana Rami Zahran kutoka kambi ya wakimbizi ya Al-Far'a huko Tubas. Kisha wakafuatilisha hili kwa kumuua mzee mmoja (Abu Khalil al-Saba'neh) kutoka mji wa Jenin. Huu ni mwendelezo wa jinai zake dhidi ya watu wa Palestina, zikiwemo za mauaji, uchomaji moto, ukamataji, uvamizi wa misikiti, na unyang'anyaji mali ya Wapalestina kinyume cha sheria, kula mali zao kwa njia ya dhambi na fujo.
Kwa kuanguka kwa dhalimu Hasina na tangazo rasmi la kupigwa marufuku kwa shughuli zote za chama kiovu cha Awami League, enzi ya giza ya siasa za chama kikuu cha kisekula -Awami League imekamilika. Kuangamia huku kwa Awami League, mrithi wa 'All India Muslim League' iliyoanzishwa mwaka wa 1906, hakutokani na mlingano wa kisiasa wa mamlaka ya kundi lolote la kisiasa, bali ni ukweli wa kihistoria na usioepukika. Hamu ya Waislamu wa India ni kuishi chini ya utawala wa Kiislamu-Khilafah.
Trump alitangaza kwa mshangao jana, Jumamosi, katika chapisho kwenye jukwaa lake la Ukweli wa Kijamii (Truth Social platform), kwamba "Baada ya usiku mrefu wa mazungumzo yaliyopatanishwa na Marekani, ninafurahi kutangaza kwamba India na Pakistan zimekubali kusitishwa kwa mapigano kamili na mara moja, "na kuzisifu nchi zote mbili kwa kutumia busara na akili kubwa." (Al Jazeera, 11/5/2025) ... ni upi ukweli katika uhasama na mzozo huu? Je, Mkataba wa Maji wa Indus ni nini haswa ambao India imeusitisha kwa muda? Je, Marekani inahusika katika kuanzisha shambulizi hilo na pia kulisitisha?
Mabadilishano ya makombora kati ya Pakistan na India yanaendelea katika njia nyingi za kusitisha mapigano huko Kashmir baada ya India kushambulia kwa mabomu maeneo tisa ndani ya Pakistan usiku wa Mei 6, ambayo ilisema ni "miundombinu ya kigaidi iliyohusika na shambulizi la silaha huko Kashmir" mwezi uliopita. Suluhisho la kivitendo la kusonga mbele haliwezi kuwa mzozo mdogo, lakini lazima liwe ukombozi wa kina wa maeneo yanayokaliwa kimabavu.
Ufalme wa Oman, ambao unaendesha upatanishi katika mazungumzo ya Marekani na Iran, ulitangaza mnamo Alhamisi (kuakhirishwa kwa raundi ya nne ya mazungumzo ambayo yalipangwa kufanyika mnamo Jumamosi katika mji mkuu wa Italia, Roma, "kwa sababu za kiufundi," bila kutaja tarehe mpya. Al-Sharq, 1/5/2025). Mazungumzo ya awali yasiyo ya moja kwa moja kati ya Marekani na Iran yalianza mnamo tarehe 12 Aprili 2025 katika mji mkuu wa Oman, Muscat, kwa upatanishi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Badr Al-Busaidi.
Neno “dola ya kina” (deep state) limetumika sana miongoni mwa wanasiasa na katika vyombo vya habari. Hata hivyo, katika kuchunguza kauli hizi, inadhihirika kwamba ziko tofauti. Je, unaweza kufafanua zaidi uwezekano wa maana ya suala hili ili tuweze kuelewa uhalisia wa kisiasa kuhusiana na neno hili, na kutoa baadhi ya mifano kwa ufafanuzi zaidi?
Kwenye Mswada wa Fedha wa 2025/26 uliowasilishwa bungeni, uliosifiwa na serikali iliyoko madarakani kama kichocheo kikubwa cha kiuchumi kwa kuwa hautatoza ushuru mpya au kuongeza uliopo katika mapendekezo ya bajeti ya mwaka huu, serikali inaweka mikakati zaidi katika usimamizi wa kodi na kujaribu kuziba mianya hiyo na kufanya ukusanyaji wa kodi kwa ufanisi. Mswada huu unalenga kupunguza hatua za kuongeza kodi na umependekeza msamaha kutoka kwa VAT ya litania ya bidhaa ambazo kwa sasa hazijakadiriwa.
Mnamo Mei 5, 2025, balozi wa umbile la Kiyahudi nchini India, Reuven Azar, akitoa maoni yake juu ya shambulizi la Bahalkam, lililotokea mnamo 22 Aprili, alisema, "Tumedhamiria kusonga mbele kutetea misingi yetu, kanuni zetu na maadili yetu, na nina hakika kwamba India itafanya vivyo hivyo."