Ijumaa, 02 Shawwal 1447 | 2026/03/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mkutano wa Cairo Unathibitisha Usaliti wa Watawala wa Kiarabu kwa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina

Mkutano huo wa dharura wa Waarabu ulifanyika jijini Cairo katikati ya mazingira machungu ambayo Umma wa Kiislamu unapitia, hasa hujuma za Kiyahudi mjini Gaza, na shinikizo la kimataifa linaloongezeka kuhusu kadhia ya Palestina. Kama ilivyotarajiwa, mkutano huo ulitoa taarifa ya mwisho ambayo ilikuwa na maneno ya kulaani na kukashifu, na kutaka masuluhisho ya viraka ambayo hayashughulikii mizizi ya mgogoro huo. Je, tunautazamaje mkutano huu? Na ni upi msimamo juu ya matokeo yake?

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Kongamano la kila Mwaka la Khilafah: “Kujenga Mustakabali pamoja na Khilafah kutoka Istanbul hadi Al-Qudsi!”

Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 104 Hijria ya kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah (miaka 101 M), Hizb ut Tahrir/Wilayah Uturuki iliandaa Kongamano la kila mwaka la Khilafah kwa ushiriki mpana chini ya kichwa: “Kujenga Mustakabali pamoja na Khilafah kutoka Istanbul hadi Al-Qudsi!”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Ramadhan ya Mwaka Huu, ni Wakati wa Ukombozi (Tahrir) kutoka kwa Ukoloni wa Kijeshi!

Shirika la habari la Reuters liliripoti mnamo Februari 21, 2025 kwamba “Marekani imetoa dolari milioni 397 kusaidia mpango wa kijeshi katika chini ya Pakistan yenye silaha za nyuklia, huku msaidizi mmoja wa bunge akisisitiza kwamba matumizi ya F-16 ya Marekani katika operesheni za kukabiliana na ugaidi yatafuatiliwa isipokuwa dhidi ya India.” Huu ndio uhalisia wa ukoloni wa kijeshi: kuyafanya majeshi ya Waislamu kupigana wao kwa wao, huku wakiyazuia kupigana jihad dhidi ya India, umbile la Kizayuni, na majeshi ya Msalaba!

Soma zaidi...

Ramadhan, Fursa ya Kutafakari na Kubadilika

Ramadhani ni mwezi wa kheri na baraka, na fursa adhimu ya kujitahidi kupata mafanikio ya duniani na akhera. Ni msimu wa utiifu, na uwanja wa kushindana katika mambo ya kheri na kufikia uchamungu ili kupata radhi za Mwenyezi Mungu, ambayo ndio mafanikio ya kweli. Ni mwezi maalum wa fadhila, si kwa sababu tu ni mwezi wa saumu na ibada, bali pia kwa sababu ni fursa adhimu ya kutafakari uhusiano wetu na Mwenyezi Mungu na kutathmini upya mwenendo wa maisha yetu ili kubadilika na kuwa bora zaidi, na kuzingatia malengo yetu ya kweli na kufafanua fahamu ya mafanikio katika maisha yetu, si kwa mtazamo wa Kidunia, bali kwa mtazamo wa kidini, kiroho na kiakhlaqi.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu